Ben Mtobwa "tutarudi na Roho zetu" afariki dunia

Kizuri sana....humu utaona wazalendo wanavyojitolea uhai wao kwa maslahi ya taifa kama kina KANDA WA KAMKANDA huku vibopa wakila maisha kama kina KANDILI ,lakini pia utayaona "mapenzi" na falsafa zake hasa kuhusu "kupenda kusiko na sababu" ,muhusika Dora anampenda kijana fukara ,hohehahe masikini kabisa ,lakini pia mwandishi ameonesha namna wanawake wanavyokosea kwa kuitumia vibaya huruma waliyopewa. Kandili alidhalilishwa shuleni na aliazimia kwenda kujiua, Dora katika kwenda kumnasihi asijiue akaona bora gauni lake lipande juu na suruali ya kandili ishuke chini(alimpa "utamu wote"hatimae akapata mimba). Kosa hilo hilo akarudia kulifanya akapata mimba ya pili......ni kitabu kizuri sana tena kinakwenda na wakati utadhani kimeandikwa jana tu mana yaliyomo humo hayatofautiani na haya ya "escrow"n.k lakini pia "mapenzi bwerere" yanayofanywa na vijana leo hii bila kujua athari yake.kitafute cha kiswahili kina "ladha nzuri" kuliko kile kilichofasiriwa kwa lugha ya malkia.

Mkuu Xie xie (Asante) can you do me a favour? Nisaidie namna gani naweza kupata hii copy. Xie xie!
 
Upumzike wa Amani Ben...

Riwaya ya Dar Es Salaam Usiku unikumbusha mbali sana...
Kaka na Dada wana-do bila kujua!!!!
 
Dah !! Nakumbuka manguli ya utunzi wa vitabu: Musiba alitunga Njama, Kikosi cha kisasi, Hofu. Ben R Mtobwa nilisoma kazi yake ya tutarudi na roho zetu. Hivi aliyetunga Hiba ya wivu na Zawadi ya ushindi ni nani?

Zawadi ya ushindi ni Ben.......hiba ya wivu sina uhakika kama ni yeye au Elvis........
Nimekumbuka ngoja niingie chimbo niibue nakala zangu..........jamaa hawana mfano hawa......
 
Duh.. this is very sad..

Nimesome hadithi zake nyingi sana na vitabu vyake na kwa hakika ni miongoni mwa watu ambao kupitia kazi zao walinishawishi sana kuanza kuandika hadithi.

Nakumbuka:

Malaika wa Shetani
Tutarudi na Roho zetu
Salam toka Kuzimu
Dar-es-Salaam Usiku
Najisikia Kuua Tena

N.k kwa kweli nitamiss sana kazi zake. I need to get a collection of his books.

RIP patner..!
Duu...r.I.p mkongwe....hakika katika watu walionivutia kusoma vitabu alikuwapo Ben mtobwa....na musiba...hawa jamaa hatari sana...mkuu wapi nitapata vitabu vyao?kwa msaada tu...ili niviweke home library
 
R.I.P alikuwa akikimbizana na ELVIS MUSIBA kwa kutunga hadidhi za kusisimua za kipelelezi....nilizipenda sana hadidhi zao...na kila mara wakati nasoma nilisubiri vitabu vyao vipya.......huwezi kumfananisha hawa na watungaji wa sasa kina shigongo ..ambao wana copy and paste!!!....mnawakumbuka ma sterling wa mtobwa na musiba??
Willy Gamba
 
Poster_Mtobwa_500B.jpg
 
Back
Top Bottom