Ben Mtobwa "tutarudi na Roho zetu" afariki dunia

Mkuu Phillemon Mikael Musiba nae ni mtu wa kugandamizia sana soma vitabu vitatu James hadley chase kisha niambe, hivyo usimfananishe na Marahemu Mtobwa (RIP).
 
R.I.P Ben!

Philemon Mikael mastaa wao ni : Ben (Joram Kiango, Neema Idd), vs Musiba (Willy Gamba, Maselina)
 
Eeeh Jamani nilikuwa napenda hadithi zake.........Bwana Mungu ametoa na Sasa ametwaa, Jina lake libarikiwe.... RIP Ben Mtobwa
 
RIP Ben Mtobwa ... We will truly miss you...
==
Dying is like getting out of a car.You leave a shell behind, but you are the same person as ever..==
 
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi~AMEN.
 
R.I.P Ben!

Philemon Mikael mastaa wao ni : Ben (Joram Kiango, Neema Idd), vs Musiba (Willy Gamba, Maselina)


exactly, I see! RIP Ben, nilikuwa nikishika kitabu cake sikiweki chini hadi kimemalizika

Sijui kama vinapatikana bookshops jamani tustock library zetu huenda hiki kizazi cha sasa kikapenda kusoma vitabu!
 
May you find Peace in the afterlife... Through your works and what you have managed to engrave in our hearts, forever you will live.

RIP.
 
Copies za vitabu vyake tafadhali ambavyo vimeorodheshwa hapo chini:
-Malaika wa Shetani
-Tutarudi na Roho zetu
-Salam toka Kuzimu
-Dar-es-Salaam Usiku
-Najisikia Kuua Tena

Mwanakijiji tufanyie mipango tupate soft copies za hivyo vitabu ambao hatukupata bahati ya kuvisoma au utuelekeze namna ya kuvipata kwa manunuzi lakini soft copies word or pdf first priority.
 
Cheka Kwa Uchungu na Uncle Ben!

Column yake katika gazeti la Heko wakati likiwa lipo katika fomu miaka ya 90.
 
I remember was even stealing some money from my parents to buy is books!!!

RIP Ben, you have done what you were supposed to do "to add value of life of other people"
 
Taifa limepoteza kinara mwingine wa kutumia fasihi andishi kufunda jamii yetu. Majumaa kadhaa yaliyopita nilimwona Ben Mtobwa aka Joram Kiango pale kwenye Mkahawa wa Vitabu wa Soma akipanga mikakati ya uandishi na uchapishaji. Kwa wale mnaohitaji vitabu vyake basi msiwe na shaka maana vinapatikana kwa wingi kwenye maduka ya vitabu hasa ukizingatia kuwa Ben alikuwa anatoa matoleo mapya ya vitabu hivyo kupitia kampuni yake ya uchapishaji ijulikanayo kama Heko Publishers. Tumuenzi kinara huyu kwa kuvirejea vitabu vyake na kuvisoma 'katikakati ya mistari' tuvumbue nini hasa kiko 'nyuma ya mapazia' aliyokuwa anajaribu kuyafunua!

"Mpenzi Leo Nitakuletea Nunda" - Joram Kiango akimwambia Binti Mrembo aliyemchunuku na ambaye kumbe alikuwa ndio Nunda Mwenyewe!Kweli Kikulacho Ki Kinguoni Mwako!
 
Tumpe Ben Mtobwa 'Zawadi ya Ushindi' kwa kusoma kwa undani vitabu vyake ili tutambue ni nini hasa amejaribu kutufunulia 'Nyuma ya Mapazia' ya jamii yetu iliyozingirwa na 'Malaika wa Shetani' na mafisadi wenye 'Roho ya Paka' wanaomsulubisha 'Mhariri Msalabani' na kudiriki kusema 'Najisikia Kuua Tena' kupitia mikataba mibovu wanayoisaini 'Dar-es-Salaam Usiku' pasipo kumwaambia mwekezaji uchwara 'Peza Zako Zinanuka' na tena bila kuogopa 'Salamu Kutoka Kuzimu' au kilio chetu cha 'Tutarudi na Roho Zetu?'
 
Taifa limepoteza kinara mwingine wa kutumia fasihi andishi kufunda jamii yetu. Majumaa kadhaa yaliyopita nilimwona Ben Mtobwa aka Joram Kiango pale kwenye Mkahawa wa Vitabu wa Soma akipanga mikakati ya uandishi na uchapishaji. Kwa wale mnaohitaji vitabu vyake basi msiwe na shaka maana vinapatikana kwa wingi kwenye maduka ya vitabu hasa ukizingatia kuwa Ben alikuwa anatoa matoleo mapya ya vitabu hivyo kupitia kampuni yake ya uchapishaji ijulikanayo kama Heko Publishers. Tumuenzi kinara huyu kwa kuvirejea vitabu vyake na kuvisoma 'katikakati ya mistari' tuvumbue nini hasa kiko 'nyuma ya mapazia' aliyokuwa anajaribu kuyafunua!

"Mpenzi Leo Nitakuletea Nunda" - Joram Kiango akimwambia Binti Mrembo aliyemchunuku na ambaye kumbe alikuwa ndio Nunda Mwenyewe!Kweli Kikulacho Ki Kinguoni Mwako!

Mkuu Companero, vinapatikana katika maduka gani? Tafadhali tutajie maduka hayo.
 
Mkuu Companero, vinapatikana katika maduka gani? Tafadhali tutajie maduka hayo.

Majina ya maduka ya katikati ya mji sijayashika, ila majuzi niliviona kwenye Mkahawa wa Vitabu wa Soma (Soma Book Cafe) ambao uko Mikocheni Reagent pembeni ya ofisi ya zamani ya Oxfam. Ni maeneo ya nyuma ya hospitali ya AAR pale Ally Hassan Mwinyi Road/Chato Street. Ukifika tu pale utaona kibao cha Soma Book Cafe kinachokuelekeza ufuate hiyo barabara ya Chato kisha ukate kushoto mbele ya shule ya chekechea kisha ukienda mbele zaidi kushoto utaona Mlingotini Closure. Mwisho kabisa kulia ndipo ulipo huo mkahawa.
 
Nimemsoma na nimebahatika kukutana nae katika ile ofisi yake pale jirani na mnazi mmoja hivi miaka ya karibuni.

Ni mwandishi mahiri na mwenye uthubutu! aliwahi kuwekwa ndani huyu,

ana kitabu chake cha ZAWADI YA USHINDI kinatumiwa kama kitabu cha kufundishia!achilia mbali vingine vingi sana.

LAKINI BADO SIJAFURAHIA NAMNA AMBAVYO KIFO CHAKE KIMETANGAZWA!!!WACHACHE SANA WANAJUA , licha ya kuwa mtu muhimu sana ambaye alitoa mchango katika habari na taaluma ya uandishi kwa ujumla!!

Umpumzike kwa Amani Ewe Ben. R. Mtobwa!!
 
Back
Top Bottom