Amoeba
JF-Expert Member
- Aug 20, 2009
- 3,289
- 781
C/O Mwenyekiti wa E.K
Shule ya Msingi Mtakuja
S.L.P 76
Makelenge Stendi
Mpendwa Belinda, Shule ya Msingi Mtakuja
Makelenge Stendi
Kwanza salamu,ama baada ya salam mimi ni mzima wa afya, hofu na mashaka ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu. Dhumuni la barua hii ni kutaka kukuuliza swali moja tu linaloniumiza nafsi yangu, mpaka nashindwa kula wala kulala, nikinywa maji najiona kwenye glasi! Hivi hiyo midomo (lipsi) uliyotumia kama avatar yako inachuruzika vitu gani vile?
Asante sana, salamu kwa mjomba, Kaka na Bi Mkubwa.
Wasalaam,
Amoeba