Beijing ina kila la kujivunia kwa maandalizi yake kabambe ya michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya 2022

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,003
1,024
VCG111355131017.jpg
Julai 31 mwaka 2015 mji wa Beijing China ulijawa na furaha, shamrashamra, nderemo na vifijo baada ya Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa kuutangaza kuandaa michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi pamoja na michezo ya Olimpiki ya walemavu ya majira ya baridi mwaka 2022, kwenye kinyang’anyiro kilichoifanya Beijing iondoke kifua mbele ikiushinda mji wa Almaty kwa kura 44 kwa 40. Mji wa Beijing ukiwa umeandaa michezo ya Olimpiki ya mwaka 2008, utakuwa mji wa kwanza kuandaa michezo yote miwili ya Olimpiki ya majira ya joto na baridi.

Beijing ilikuwa na kila sababu ya kujivunia kwa kutunukiwa kuandaa michezo hii, kwani inafaa kwa ajenda yake mpya ya "kuzingatia zaidi uendelevu, urithi, na uwazi" na kama ilivyofanya mwaka 2008, tunaamini kuwa na mwaka 2022 italeta miujiza mikubwa kwenye maandalizi yake na kuendesha kwa mafanikio michezo hii.

Rais wa Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa IOC Thomas Bach Oktoba 26 alisifu juhudi za Beijing katika maandalizi yake ya michezo hii katika hafla ya kuanza kuhesabu siku 100 hadi ifanyike michezo ya Beijing 2022.

Hadi sasa Beijing imeshafanya maandalizi makubwa na ya aina yake ya Olimpiki ambapo kwa mara nyingine tena tunasubiri kuona ikiandika historia. Bila shaka Beijing itaipeleka michezo hii kwenye ngazi mpya na viwango vipya kwa kushirikisha watu wa China milioni 300 kwenye michezo ya barafu na theluji. Na hii itafanya kuwe na michezo ya majira ya baridi duniani kabla ya michezo ya Olimpiki ya Beijing 2022 na baada ya michezo hii.

Hivi sasa tumeshaanza kushuhudia kauli mbiu ya michezo hii ikitekelezwa yaani “Pamoja kwa ajili ya mustakabali wa pamoja” na mustakabali huu wa pamoja utakuwa kama tochi inayomulika michezo ya olimpiki ya majira baridi duniani. Mara nyingi China inapokabidhiwa jukumu la kuwa mwenyeji huwa inazingatia zaidi umoja na mshikamano wa sehemu mbalimbali duniani, hivyo hata kauli mbiu hii ya mwaka huu pia inaonesha umoja na juhudi za pamoja, zinazojumuisha maadili na ndoto ya msingi ya Olimpiki, pamoja na lengo la kutafuta umoja, amani na maendeleo duniani.

Sambamba na kauli mbiu hii, Beijing pia imezindua medali mpya kwa ajili ya michezo ya Olimpiki. Tunafahamu kuwa medali ni sehemu muhimu ya michezo na ni ishara ya ushindi kwenye michezo, na kama kawaida medali za safari hii pia zimekidhi matarajio ya watu. Ubunifu wa medali hizi sio tu unaakisi utamaduni na moyo wa nchi mwenyeji, bali pia unajumuisha mawazo ya uvumbuzi na ubunifu wa kuvutia wa wasanii. Labda nidokeze kidogo tu kuhusu muundo wa medali hizi. Kwanza medali za michezo yote miwili ya Olimpiki ya majira ya baridi zina dhana moja na kuwa na usanifu wa aina moja.

Kwa mujibu wa Kamati ya Olimpiki ya Beijing, medali hizi zimepewa jina la "Tong Xin," likimaanisha "pamoja tukiwa kama kitu kimoja." Medali hizi pia zina duara kubwa la kuchonga na katikati yake kuna nakshi ya maduara matano ya Olimpiki.

Kwa kuzingatia kuwa sasa tupo kwenye kipindi cha janga la virusi vya Corona, waandaaji hawakufumbia macho hata kidogo suala hili. Beijing imetangaza kwamba kutakuwa na usimamizi mkali wa kupima na kuendesha michezo ili kulinda afya ya umma. Pia washiriki wa michezo wanaruhusiwa kwenda kwenye maeneo waliyopangiwa tu, yakiwemo viwanja vya michezo na vituo vya kulala ambapo watachukuliwa na magari maalumu. Wakati huohuo hali ya afya ya wanariadha itafuatiliwa kwa makini na wanariadha kupimwa kila siku. Wanaruhusiwa kufanya mazoezi kwenye viwanja maalumu walivyopangiwa ambapo waandishi wa habari wataweza kufika.

Ikiwa sasa ujenzi wa viwanja vyote 12 umekamilika na kuthibitishwa na mashirikisho ya michezo duniani, jumla ya michezo 10 ya kimataifa na wiki tatu za mazoezi imeanza mapema Oktoba, ambayo itaendelea hadi Disema. Tunatarajia kuwa michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ambayo itafunguliwa rasmi Ijumaa ya tarehe 4 Februari mwaka 2022, itavunja rikodi na kuandika historia kwenye vitabu vya michezo.
 
Back
Top Bottom