Msaada: Nahitaji kujua bei za mashine za kusaga na kukoboa unga

DavieMchomvu

New Member
Jan 22, 2016
3
5
Wakuu habari ya muda huu,

Samahani ningependa kujua gharama au bei ya kununua mashine ya kusagana kukoboa Unga wa mahindi.

Asanteni sana
 
Mwelekeze atafuta motor ya hp ngapi kwa ajili ya kukobolea na ya hp ngapi kwa ajili ya kusaga Mkuu!
 
Mlleta mada kuna jamaa mmoja hivi alileta uzi kama huo umu ndani kuna jmaa mmoja akasema wapo temeke wanatengeza wao wenyew mashine ila ni zaid ya milion 30, nikipata jina la huo uzi nitakuungnisha
 
Jamani msibahatishe kwa kukadilia inaweza ikafika 5m. Huku chenye being Mimi nadhani NI motor ambayo inaweza ikafika hadi 2m...kwa mpya au chini ya halo kwa motor za mtumba
 
nimependa kichwa cha habari " kusaga na kukoboa unga"
sijui unga ukisagwa unakuwaje na unga ukikobolewa unakuwaje, sijawahi ona. Ndo yale yale ya sheli ya BP
Kusaga na kukoboa ni vitu viwili tofauti ila angeandika Mahindi badala ya unga lakini tumemuelewa ila umeangalia mbali
 
Yanayosagwa na kukobolewa ni mahindi.

Unga ni zao linalotokana na kusagwa kwa mahindi.

Mleta mada anatafuta mashine ya kukoboa na kusaga mahindi.
 
Back
Top Bottom