Bei za mashamba Karatu na fursa za kilimo

maroon7

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
11,050
14,931
Wakuu 'Posuta'

Mi ni mdau ninaetaka kuhamia Karatu hivi karibuni kikazi..ila pamoja na hayo mi ni mjasiliamali kwenye kilimo na ufugaji hivyo nataka kujua bei za mashamba kwa huko zipoje kwa ekari na pia fursa zingine za kilimo na ufugaji kwa huko.
 
Taitu kalesa mkombe....!

Inaonekana wadau wa karatu humu hawapo.
 
Wakuu 'Posuta'

Mi ni mdau ninaetaka kuhamia Karatu hivi karibuni kikazi..ila pamoja na hayo mi ni mjasiliamali kwenye kilimo na ufugaji hivyo nataka kujua bei za mashamba kwa huko zipoje kwa ekari na pia fursa zingine za kilimo na ufugaji kwa huko.
Saita Khae...
Kwanza hongera kwa mawazo na fikra pevu za ujasiriamali. Kusema ukweli bei za mashamba karatu hasa maeneo 'along the main road' arusha-Ngorongoro ni kubwa sana. Labda uende vijiji vya ndani ndani unaweza kupata kwa bei nafuu. Lakini kwa maeneo kama rhotia, endarofta, ganako, sumawe, bashai, njiapanda, changarawe na kwingine bei ziko juu sana kwasababu maeneo hayo kuna wawekezaji wakubwa wa mahoteli wamenunua..
 
Saita Khae...
Kwanza hongera kwa mawazo na fikra pevu za ujasiriamali. Kusema ukweli bei za mashamba karatu hasa maeneo 'along the main road' arusha-Ngorongoro ni kubwa sana. Labda uende vijiji vya ndani ndani unaweza kupata kwa bei nafuu. Lakini kwa maeneo kama rhotia, endarofta, ganako, sumawe, bashai, njiapanda, changarawe na kwingine bei ziko juu sana kwasababu maeneo hayo kuna wawekezaji wakubwa wa mahoteli wamenunua..
Mkuu asante kwa kunipa mwanga...hata vijiji vya ndani ntatafuta tu mkuu mradi panafikika vizuri...maana kaskazini kweli sio kama mikoa mingine mingi ambako unapata ardhi bei chee mno tena ndani ya manispaa...ni changamoto kwa sisi wenye vimitaji vidogo
 
Karatu mashamba sio rahisi upate kule kuna uhaba sana wa Aridhi, Na Waambulu hawauzi mashanba hovyo kama wengine. Wambulu by Natuture ni wakulima sana na wanalima mno so kupata shamba sahau labda kukodishiwa.
 
Saita Khae...
Kwanza hongera kwa mawazo na fikra pevu za ujasiriamali. Kusema ukweli bei za mashamba karatu hasa maeneo 'along the main road' arusha-Ngorongoro ni kubwa sana. Labda uende vijiji vya ndani ndani unaweza kupata kwa bei nafuu. Lakini kwa maeneo kama rhotia, endarofta, ganako, sumawe, bashai, njiapanda, changarawe na kwingine bei ziko juu sana kwasababu maeneo hayo kuna wawekezaji wakubwa wa mahoteli wamenunua..
Tatizo sio hoteli ila bya Nature Waambulu hawauzagi Aridhi hovyo. ukiona kaauza basi ujue kapata shida sana mimi nimekaa kule sana najua hilo. Ukienda wakati wa kilimo ndo utaelewa hili make Wilaya nzima huwa imepambwa kwa mahindi. so Jamaa sio wauzaji wa Aridhi.
 
Furusa kule labda ulime mboga za majani zina soko sana n zinaliwa mno na zina demand sana na zina bei sana. Ila sasa uwe na maji ya kuchimba chini na kule kupata maji lazima uende muta za kutosha chini sio chini ya 100 na kuendelea.
Ukiweza kupata maji yako basi, kwa sababu Karatu pia inakuwaga na uhaba sana wa maji kipindi cha kiangazi. mimi ninashamba ukiwa unaingia karatu mjini baada ya Rhotia natafuta nguvu ni drill maji
 
Tatizo sio hoteli ila bya Nature Waambulu hawauzagi Aridhi hovyo. ukiona kaauza basi ujue kapata shida sana mimi nimekaa kule sana najua hilo. Ukienda wakati wa kilimo ndo utaelewa hili make Wilaya nzima huwa imepambwa kwa mahindi. so Jamaa sio wauzaji wa Aridhi.
Haaaa wazaramo nao wangekuwa kama wambulu ardhi DSM isingesgikika,wao kila ngoma (Akitoa mwali) anauza shamba.
 
Wakuu 'Posuta'

Mi ni mdau ninaetaka kuhamia Karatu hivi karibuni kikazi..ila pamoja na hayo mi ni mjasiliamali kwenye kilimo na ufugaji hivyo nataka kujua bei za mashamba kwa huko zipoje kwa ekari na pia fursa zingine za kilimo na ufugaji kwa huko.

Kuna shamba heka 2 maeneo ya Qurus linauzwa 10 mil..
 
Wakuu 'Posuta'

Mi ni mdau ninaetaka kuhamia Karatu hivi karibuni kikazi..ila pamoja na hayo mi ni mjasiliamali kwenye kilimo na ufugaji hivyo nataka kujua bei za mashamba kwa huko zipoje kwa ekari na pia fursa zingine za kilimo na ufugaji kwa huko.
Posuta qurtama goloayo, mkuu wanakuja na Mimi pia nlitaka kujua...
 
Asante mkuu mi nimehamishiwa kule kikaz natakiwa kureport wiki ijayo I hope tunaweza meet kama upo huko karatu tukashare experience
 
Karibu!, mashamba hawauzi hata ukipata utauziwa kwa ghari sana...yaani ekari moja su chini ya 3mil alafu ni pembezoni sana. Kukodisha kwa msimu wanafanya laki na nusu had I laki tatu kwa ekari moja bei hizi hutegemeana na shamba lenyewe(productivity). Watu wa huku hutegemea sana Kilimo kwahiyo hawashawishiki kabisa kuuza maeneo wala huwezi sikia mahali panauzwa kwa kipindi nilichokaa Mimi.....welcome sana kumbuka kujiheshimu pia kuja na mkeo hiyo ni tahadhari!....wewe ni yule wa VFT?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom