Brigedia Chan-ocha
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 1,353
- 2,842
Kuna nini viwandani? kama uzalishaji umepungua Serikali iruhusu vifaa vya ujenzi kama bati na saruji kutoka nje kuingizwa nchini. Bati za Simba Dumu zilizokuwa zikiuzwa bundle 1 bati 16 shilingi 325,000/= hadi kufikia juzi bei ilikuwa imefika shilingi 400,000/= kwa bundle 1 la bati za simba dumu, kwa ujumla bei za mabati yote zimepanda kwa tofauti kubwa sana kwa muda mfupi, hata saruji imepanda maradufu, serikali iingilie kati na kuona tatizo ni nini?