Bei ya vyakula "Kilimanjaro Fast Food" pale Mombo si rafiki

Watu hatujielewi tu, we usihangaike na mtu muache na vyakula vyake.
Cha kufanya ukijua unasafiri mwambie mama watoto akutayarishie dry food kama halfcakes, maandazi, kuna vidude flani wanaita vikokoto safi sana kwa safari, usisahau kununua soda yako au hata juice ya azam mango hapo mtaani kwenu maana ukinunua hoteli ya njian bei yake ni balaa.

Tutawanyoosha wauza vyakula njiani tuache kuwalea wanapandisha bei kiholea ili kupata super profit kwa kua wanajua hatuna option.

Tujipange ukienda safarini kula kwenye hotel zao acha.
...Yeah hata mimi nikisafiri na familia ndivyo tunavyofanya chinja kuku home jioni, nunua nusu kilo viazi, wife anakaanga funds kwenye foil,then kwa food container with fruits, juice & water..
 
Nilipita hapo saa 6 nikitokea iringa na gari la mby to arusha , nikiwa na mama mmoja aliniagiza kumnunulia chipsi nyama (akinipa10,000) nikamletea sahani yake 1 na chenchi ya sh:3000 alipanic na roho ikamuhuma hatari sana: nikamwambia mama huku siyo uyole au mbeya kuwa ukiwa na buku wanakupa ungo mzima wa chipsi na chenchi ibaki.
 
Mbona bei ya kawaida sana iyo??hata rock hill ni same price...unataka chips nyama kwa 3000??mburaaa nuchelya ikite
...Haha bwanaa omba mungu usiwe kwenye wale elfu kumi aliowapiga panga JPM leo..plus wategemezi wao..
 
Inakera sana. Hii sio kwa ubora Wa chakula wala ubora Wa hotel Bali ni wizi na unyonyaji Wa wazi kwa wasafiri. Juzi tumepelekwa pale Liverpool napo ni vituko, kaportion ka nyama 6000 ni finyango tano!!!
Mkuu apo pia chai ya rangi 1000 andazi 1000 sasa sijui vina uwiano gani.
NB: chai ya rangi haina viungo hiyo
 
Kilimanjaro, Arusha ni kwa ma fogo (Mabillioner) wanauza bei kulingana na quality ya chakula halafu mbona n bei ya kawaida..... nenda KFC Ukaulize bei ya vyakula kule.......

Au kama bei ni ghali panda magari ya kuelekea Chato bei za hotel za huko ni sawa na bure
Acha kutudhalilisha we mtoto , kwa nini mnamchukia Magu hivi !! Jifunzeni adabu.
 
Bei ya kawaida sana hiyo..wote mnaolalamika humu nyie ni wapitaji tu na sio wachaga,wachaga hatulalamikii bei ya chakula bhana sisi tunajali ubora wa chakula na usafi...unataka nile mataputapu kama hotel zenu za chato ili nisumbuliwe na tumbo la kuhara kisa nini??
Tunajali afya hata magari yanakuja kuja kaskazn ni mazuri sio kama mikweche yenu uko kanda ya ziwa (CCM).gari zetu ni daraja la juu,hatutaki ujinga ukishindwa bei beba vitumbua vyako na maji ya kiroba
 
Ka
Ukiwa njiani kuelekea Arusha-Dsm/ Dsm-Arusha .. sasa Magari Mengi yanapita Pale Hotel Mpya Ya Kilimanjaro.

Hakika Bei ya Vyakula waliyoweka Si Rafiki kabisa Kwa msafiri na nnadhani wanakomoa kwa Vile Msafiri anakua hana Option Mbadala.

COUPON YA CHIPS KUKU POTION /NYAMA FINYANGO TANO NI Tsh 7000/=

Kumbuka Kuku wanamgawa mara nne.

MISHKAKI YENYE VINYANGO NNE HAFIFU NI TSH 2000/=.

SAMBUSA/MAANDAZI NI TSH 2000/=
Utaishia kicheka ukiziona.
Imepelekea mpaka wale jamaa wanaouza matunda maeneo yale nao kua na Bei Juu .
Kamfuko ka Machungwa ni Tsh 5000/= . ...
Ipo haja ya Bei hizi kuingiliwa na mamlaka husika , wakiachiwa ipo siku tutauziwa andazi Tsh 5000/=
Na wasipolitizama Hili kwa Haraka , italeta Athari mpaka kwnye magari yanayopita pale.
087cbc8680fe2ac39dd9750bcbd15b69.jpg
Kaka Mandela, wenye hotel barabarani huzani abiria wa mabasi wametoka au wanaenda Migodini! Bei ya chakula Na vinywaji ni ghali kuliko Dar japo raw materials zinapatikana huko kiurahisi. Matunda wanauza ghali kuliko mjini. Wengine tunasimama tu pale kujisaidia. Pesa ithaminishe na ununuacho how comes Robo broiler anauzwa 7000 hotel isiyo ya kitalii? Roho Dar buku 2 tuu tena fresh kapikwa vizuri. Waache wizi
 
Naam, bei yapo ipo juu kutokana na ubora pamoja na uhakika wa vyakula vyao.

Mimi huwa nikipita pale nakula huku najiamini kabisa. Nachukua Coupon yangu ya kule kwenye vyakula mchanganyiko, napiga pyuu alafu napanda kwa gari kupumzika. Sina wasiwasi kabisa...

Kama KILIMANJARO MOTORWAY FAST FOOD ni ghali, jaribu kwingine.
Mkuu, hebu badili id yako basi. Jiite Fisadi Sugu. Andazi 2000? Sambusa 2000? Wali finyango 7000? Aaaaa tuache utani. Tunatofautiana kipato. Karibu huku kwetu andazi 100 na Sambusa 200!!
 
Kuna comments hua zinatolewa hapa jf zinaashiria kila mtu ana uchumi wa kati au ni tajiri kabisa cha ajabu ukienda jukwaa la nafasi za kazi unakuta kaanzisha uzi anatafuta kazi yoyote halali.

Ni vema tutambue taifa lina watu wenye uchumi tofauti tofauti sasa tukisema nenda KFC hivi watanzania wangapi wanaweza kwenda? Au wenzetu mliopata pesa mnaona tusio nazo ni uzembe?

Maslahi ya wengi ndio maslahi yanayopaswa kuzungumziwa sio maslahi ya watu wachache wenye pesa nyingi.
KFC yenyewe huwa naiona kwenye video kwa jirani yangu.
 
Bei ya kawaida sana hiyo..wote mnaolalamika humu nyie ni wapitaji tu na sio wachaga,wachaga hatulalamikii bei ya chakula bhana sisi tunajali ubora wa chakula na usafi...unataka nile mataputapu kama hotel zenu za chato ili nisumbuliwe na tumbo la kuhara kisa nini??
Tunajali afya hata magari yanakuja kuja kaskazn ni mazuri sio kama mikweche yenu uko kanda ya ziwa (CCM).gari zetu ni daraja la juu,hatutaki ujinga ukishindwa bei beba vitumbua vyako na maji ya kiroba
Naona unajaribu kuzungumzia ukabila, unazungumzia kabila lipi ni bora lipi sio bora, unazungumzia gari za wapi ni bora wapi sio bora, tena unahakikisha kwamba watu wa kanda ile wanakula mataputapu, kama mtanzania nakuita mjinga wa kiwango cha rami, uzuri wa mabasi ya kilimanjaro unatuhusu nini sisi?, utajiri wako unatuhusi nini sisi?, uzuri wa mkoa wako unatuhusu nini sisi?

Mada ni bei za vyakula kua juu, hayo ya ukabila ni utoto wako binafsi, kuna makabila mangapi Tanzania? Kila mtu aanze kutaja kabila lake ili iweje?.

Nakuhakikishia kichwa chako unafugia nywele na kama kina kitu cha ziada basi mifupa ndio mingi kichwani kuliko contents za ubongo
 
Ila vyakula vyao ni classic,ni vizuri alafu wasafi,wanastahili kuweka hio bei jamani,tusiwaonee,elfu 7,pesa ndogo sana hio.mim hua napanda gari inayosimama hio hotel.
 
29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom