johnmashilatu
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 718
- 703
Wilaya ya Ngara mkoani Kagera inakumbana na changamoto ya ukosefu wa bidhaa ambapo sasa lita moja ya Petrol inauzwa tsh 5000.
Wakati hayo yakijiri, mitambo ya kusuma maji imezimwa kwa siku tano sasa kutokana na upungufu wa umeme.
Kwa upande wa mafuta ya magari, vituo rasmi vya kuuza bidhaa hiyo havina petrol tangu juzi, hivyo wajanja wamechukua fursa hiyo kujineemesha.
Wafanyabiashara wajanja wameyafuata Burundi na kuyauza wilayani ngara kwa bei ya tsh 5000 kwa lita.
Wauzaji wa mafuta wanadai kuishiwa bidhaa hiyo wakidai yatafika Jumapili wiki hii.
Aidha, mamlaka ya maji ya Mjini Ngara imetoa tangazo kupitia Radio Kwizera kuwa haiwezi kusukuma maji kutokana na umeme mdogo usioweza kusukuma mitambo hiyo
Kadhalika TANESCO kama kawaida hawajatoa taarifa ingawa inadaiwa kuwa kuna hitilafu katika mitambo yake
Wakati hayo yakijiri, mitambo ya kusuma maji imezimwa kwa siku tano sasa kutokana na upungufu wa umeme.
Kwa upande wa mafuta ya magari, vituo rasmi vya kuuza bidhaa hiyo havina petrol tangu juzi, hivyo wajanja wamechukua fursa hiyo kujineemesha.
Wafanyabiashara wajanja wameyafuata Burundi na kuyauza wilayani ngara kwa bei ya tsh 5000 kwa lita.
Wauzaji wa mafuta wanadai kuishiwa bidhaa hiyo wakidai yatafika Jumapili wiki hii.
Aidha, mamlaka ya maji ya Mjini Ngara imetoa tangazo kupitia Radio Kwizera kuwa haiwezi kusukuma maji kutokana na umeme mdogo usioweza kusukuma mitambo hiyo
Kadhalika TANESCO kama kawaida hawajatoa taarifa ingawa inadaiwa kuwa kuna hitilafu katika mitambo yake