Mdau, Yafuatayo ni maoni yangu kwa haraka haraka,ambayo ni jibu kwa wadau fulani walioniuliza kwanini bei ya gari fulani ipo juu. Naomba kwa pamoja tuchangie kwa manufaa ya wote.
Najua, Watanzania wengi ni wazuri wa kulialia, kulalamika na kutafuta visababu vidodo vidogo ili wapunguziwe bei au wauziwe kwa bei ya chini sana( Mwisho wanaishia kununua vitu fake).
Pia imekuwa kama hulka yetu kudharau biashara za wenzetu, kuzikandia, kuponda, kusengenya na kuzidharirisha. Tumekuwa na tabia ya kushusha hadhi na bei ya bidhaa/biashara za wenzetu huku tukijifanya tunajua mazingira na mzunguko wa biashara hiyo wakati hatujui. Tunasahau ya kuwa tunaharibu biashara za watu mwingine (hii husababisha biashara nyingi kufa).
Kwa kifupi, Bei ya bidhaa hutokana na mazingira yanayoizunguka biashara hiyo, ubora na hadhi ya bidhaa, upatikanaji, ukubwa wa biashara/ kampuni, usafirishaji, umuhimu wa bidhaa, kodi, malengo ya muuzaji na mambo mengine mengi.
Kuhusu bei za magari yatokayo Japan, Siku za mwanzo watu wengi walikuwa wanaship magari ya wizi hivyo ilifanya kushusha bei halisi ya magari.
Pia kunawafanya biashara wengi( Hasa wakubwa) ambao wanakwepa kodi au wanatumia exemption fake, hawa wanasababisha kushuka kwa bei halisi ya magari , pia wanachangia kushuka kwa pato la serikali kwa kukwepa kodi.
Kutokana na kuyumba kwa uchumi wa dunia, Wajapan wengi walikosa kazi za kuajiliwa na kuamua kujiajiri katika sekta Magari used. Ikumbukwe ya kuwa Wajapan wengi wanauwezo wa kupata magari ya bure (Dumping cars) au magari ya bei nafuu yenye migogoro au yaliyopata ajari kwa bei ya chini kabisa hivyo kuwafanya wawe kwenye nafasi nzuri ya kuuza kwa bei ya chini.
Siku za nyuma, ambapo magari yalikuwa bei rahisi kuna baadhi ya makampuni makubwa ya kijapan yalinunua magari mengi na kuyaweka kwenye stock. Haya makampuni kwa sasa wanayauza haya magari kwa bei ya chini mno, ndo maana magari ya miaka ya nyuma ni bei rahisi sana kulinganisha na magari ya miaka ya hivi karibuni.
Kuna magari yaliyo athirika na mafuriko ya tsunami, active radiator, Nuclear, haya huuzwa kwa bei ya chini Mno na madhara yake kiafya ni makubwa mno ( KANSA NI ZA KUFIKIA). Pia injini zake ndo kama zinavyo waharibikia kila siku.
Kuna magari yanaitwa accedental/broken cars haya ni magari yaliyopata ajari, damped, damaged, yenye matatizo ya injini, na matatizo mengine mbalimbali na kuwa solved. Haya magari bei yake ni nafuu sana. Ukweli ni kwamba ongezeko la haya magari, limesababisha ongezeko la kushamili kwa biashara ya spare parts. Wabongo wengi wamenunua Magari haya na hata kabla ya mwaka mmoja kuisha wanajikuta wameingia katika biashara ya manunuzi ya spare parts. wanakwepa bei halisi ya magari au wanakwepa tofauti ya USD 1,000/ lakini ukichambua gharama za kufix hilo gari miaka miwili baada ya kulinunua utakuta ni sawa na gharama za kununua magari mawili kwa bei inayokubarika. Na ndio maana magari mengi bongo baada ya miaka miwili mitatu utayakuta juu ya mawe.
Anyway, kuna mazingira mengi yanayofanya magari ya japan kuwa bei chini na juu, unatakiwa kuwa makini, na kunamambo mengi sana yakujadili katika biashara hii, kuliko mtu kukurupuka na kuanza kushambulia biashara za watu hasa wajasiriamali wadogo wadogo.
Lakini pia mwisho wa yote, wewe kama Mtanzania unayependa maendeleo na usiokwisha kuilaumu serikali ya CCM au unayetaka Chadema ilete mabadiliko, Unatakiwa kununua magari/ bidhaa kutoka kwenye makampuni ya watanzania wazalendo wenzako na sio kusujudu makampuni ya kigeni. Ukweli ni kwamba ukinunua magari kwenye kampuni ya kijapan utakuwa umesaidia kukuza uchumi wa taifa la japan, na kuwaongezaa ajira na kipato, na ukinunua kutoka kwenye kampuni la mzalendo mwezako utakuwa umesaidia kuongeza ajira na kipato kwa vijana wetu, umesaidia kuongeza pato la serikali kwa kupata kodi, utakuwa umesaidia maendeleo ya nchi na jamii yetu kwa sababu wamiliki wengi wa haya makampuni hutuma remmitances nyumbani, ambazo zinasaidia familia, zinajenga majumba, zinalipia karo na huduma za afya, pia wamiliki wengi wa haya makambuni wanatabia ya kuwekeza katika shughuri balimbali za kijamii na kimaendeleo.
Nina mengi sana ya kusema ila kwa sasa aksanteni !
Najua, Watanzania wengi ni wazuri wa kulialia, kulalamika na kutafuta visababu vidodo vidogo ili wapunguziwe bei au wauziwe kwa bei ya chini sana( Mwisho wanaishia kununua vitu fake).
Pia imekuwa kama hulka yetu kudharau biashara za wenzetu, kuzikandia, kuponda, kusengenya na kuzidharirisha. Tumekuwa na tabia ya kushusha hadhi na bei ya bidhaa/biashara za wenzetu huku tukijifanya tunajua mazingira na mzunguko wa biashara hiyo wakati hatujui. Tunasahau ya kuwa tunaharibu biashara za watu mwingine (hii husababisha biashara nyingi kufa).
Kwa kifupi, Bei ya bidhaa hutokana na mazingira yanayoizunguka biashara hiyo, ubora na hadhi ya bidhaa, upatikanaji, ukubwa wa biashara/ kampuni, usafirishaji, umuhimu wa bidhaa, kodi, malengo ya muuzaji na mambo mengine mengi.
Kuhusu bei za magari yatokayo Japan, Siku za mwanzo watu wengi walikuwa wanaship magari ya wizi hivyo ilifanya kushusha bei halisi ya magari.
Pia kunawafanya biashara wengi( Hasa wakubwa) ambao wanakwepa kodi au wanatumia exemption fake, hawa wanasababisha kushuka kwa bei halisi ya magari , pia wanachangia kushuka kwa pato la serikali kwa kukwepa kodi.
Kutokana na kuyumba kwa uchumi wa dunia, Wajapan wengi walikosa kazi za kuajiliwa na kuamua kujiajiri katika sekta Magari used. Ikumbukwe ya kuwa Wajapan wengi wanauwezo wa kupata magari ya bure (Dumping cars) au magari ya bei nafuu yenye migogoro au yaliyopata ajari kwa bei ya chini kabisa hivyo kuwafanya wawe kwenye nafasi nzuri ya kuuza kwa bei ya chini.
Siku za nyuma, ambapo magari yalikuwa bei rahisi kuna baadhi ya makampuni makubwa ya kijapan yalinunua magari mengi na kuyaweka kwenye stock. Haya makampuni kwa sasa wanayauza haya magari kwa bei ya chini mno, ndo maana magari ya miaka ya nyuma ni bei rahisi sana kulinganisha na magari ya miaka ya hivi karibuni.
Kuna magari yaliyo athirika na mafuriko ya tsunami, active radiator, Nuclear, haya huuzwa kwa bei ya chini Mno na madhara yake kiafya ni makubwa mno ( KANSA NI ZA KUFIKIA). Pia injini zake ndo kama zinavyo waharibikia kila siku.
Kuna magari yanaitwa accedental/broken cars haya ni magari yaliyopata ajari, damped, damaged, yenye matatizo ya injini, na matatizo mengine mbalimbali na kuwa solved. Haya magari bei yake ni nafuu sana. Ukweli ni kwamba ongezeko la haya magari, limesababisha ongezeko la kushamili kwa biashara ya spare parts. Wabongo wengi wamenunua Magari haya na hata kabla ya mwaka mmoja kuisha wanajikuta wameingia katika biashara ya manunuzi ya spare parts. wanakwepa bei halisi ya magari au wanakwepa tofauti ya USD 1,000/ lakini ukichambua gharama za kufix hilo gari miaka miwili baada ya kulinunua utakuta ni sawa na gharama za kununua magari mawili kwa bei inayokubarika. Na ndio maana magari mengi bongo baada ya miaka miwili mitatu utayakuta juu ya mawe.
Anyway, kuna mazingira mengi yanayofanya magari ya japan kuwa bei chini na juu, unatakiwa kuwa makini, na kunamambo mengi sana yakujadili katika biashara hii, kuliko mtu kukurupuka na kuanza kushambulia biashara za watu hasa wajasiriamali wadogo wadogo.
Lakini pia mwisho wa yote, wewe kama Mtanzania unayependa maendeleo na usiokwisha kuilaumu serikali ya CCM au unayetaka Chadema ilete mabadiliko, Unatakiwa kununua magari/ bidhaa kutoka kwenye makampuni ya watanzania wazalendo wenzako na sio kusujudu makampuni ya kigeni. Ukweli ni kwamba ukinunua magari kwenye kampuni ya kijapan utakuwa umesaidia kukuza uchumi wa taifa la japan, na kuwaongezaa ajira na kipato, na ukinunua kutoka kwenye kampuni la mzalendo mwezako utakuwa umesaidia kuongeza ajira na kipato kwa vijana wetu, umesaidia kuongeza pato la serikali kwa kupata kodi, utakuwa umesaidia maendeleo ya nchi na jamii yetu kwa sababu wamiliki wengi wa haya makampuni hutuma remmitances nyumbani, ambazo zinasaidia familia, zinajenga majumba, zinalipia karo na huduma za afya, pia wamiliki wengi wa haya makambuni wanatabia ya kuwekeza katika shughuri balimbali za kijamii na kimaendeleo.
Nina mengi sana ya kusema ila kwa sasa aksanteni !