Bei ya mafuta ya petroli, dizeli toka Urusi sasa ni $30 kwa pipa. China na India wachangamkia fursa. Kwanini Tanzania isifanye hivyo pia?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,952
4,326
Wahenga walisema, 'Kufa kufaana'. Kwenye kila tatizo linalotokea hapa duniani huwa linafungua fursa kwa baadhi kufaidika nalo. Badala ya kukaa tunalialia linapotokea tatizo, tunapaswa kutazama upande wa pili wa shilingi kwamba tutafaidikaje na hilo tatizo. Hata lile tatizo kubwa la mlipuko wa covid 19, yapo makampuni na nchi zilizopiga pesa ile mbaya wakati wengine wakiwa wameji lockdown na zingependa mlipuko huu wa covid 19 uendelee kudumu!

Hii vita ya Urusi na Ukraine, mara tu ilipoanza nchi kama za Saudi Arabia na zingine zote za OPEC ziliona ni fursa, na zikaanza kupandisha bei ya mafuta yao. Nchi za Ulaya na Amerika walipoamua kususa mafuta ya Russia, nchi za OPEC na Saudia zikachangamkia fursa hiyo kwa kasi zaidi ya kuendelea kupandisha bei ya mafuta yao na hadi sasa yamefikia zaidi ya $ 120 kwa pipa. Kabla ya vita hii pipa lilikuwa linauzwa si zaidi ya $ 70. Nchi zingependa vita hii iendelee kudumu!

Russia ni mzalishaji mkubwa duniani wa mafuta haya ya petroli/ diseal na na gesi kwa kiwango cha theluthi moja ya mafuta yote duniani. Baada ya vita hii na nchi za Ulaya na Amerika kuanza kususia mafuta yake, Urusi imeteremsha sana bei ya mafuta yake hadi sasa kufikia $ 30 kwa pipa! Uchina na India wamechangamkia fursa hii, wananunua mafuta haya kutoka Russia na wangelipenda vita hii iendelee kudumu! Tukumbuke kuwa population ya China na India ni zaidi ya watu billion 3, yaani theluthi moja ya population ya dunia hii. Wao hawafungamani na upande wo wote kama sisi.

Sasa kwa nini na sisi tusichangamkie fursa hii ( na kupenda iendelee kudumu) kwa kununua mafuta haya toka Russia? Kuna tatizo gani tukifanya hivyo? Tunaogopa nini? Au watalaamu wety wa uchumi mnasemaje?

 
Nakumbuka Mzalendo #1 aliwahi kusema tutumie fulsa ya kuuza chakula kwenye nchi zilizokuwa na njaa watu wakamjia juu na kusema huwezi kuombea mwenzio apate njaa ili wewe unufaike.

Sasa wewe naona unaombea vita iendelee ili tununue mafuta kwa bei ya dezo!

Kibiashara kweli hiyo ni strategy nzuri, tena mnawekeana na mkataba kabisa wa muda maalumu. Ingewezekana kwa urahisi zaidi kama tungekuwa tunanunua mafuta toka Russia kabla hata ya vita.
 
Hapana hili hawataweza. Ligumu kwao! Urahisi ni kuwakamauwa sisi mazombi ambao tuko kama ng’ombe wa maziwa, sababu hatutalalamika wala kubisha, hata kama hatulishwi tutoe maziwa!😡🤬🤐
 
Unataka kusema mchonga jeneza anawaombea waliohai vifo?
Ndiyo hapo sasa, mleta mada anaombea vita iendelee ili tununue mafuta kwa bei nafuu!

Lakini, kama USA wanaombea vita iendelee ili wauze silaha kwa Ukraine, na ili uchumi wa Russia udhoofike zaidi, kwa nini sisi tusitumie hiyo fulsa kupata mafuta kwa bei nafuu? Yani hapo iwe kama mbuzi kufia kwa muuza supu!
 
Tuanze na upanuzi wa matumizi ya gesi yetu wenyewe ktk mitambo, usafiri na usafirishaji, majumbani, vyuoni nk!
Makaa ya mawe tunayo halafu tumeduwaa!

Kila siku utalii utalii na kufukuzana na Wamaasai Ngorongoro!
Mara uchumi wa bluu! Na huku kugombania mitumba ya ulaya!

Mswahili akiiba kura na kujipa ulaji, akivaa visuti na kuendeshwa kwenye V8 basssss! Humwambii kitu.
 
Mleta mada unaongelea Crude oil "Mafuta ambayo hayajasafishwa" Hao India na China wanazo Refinery za kusafisha hiyo Crude oil,
Sasa Bongo wakinunua hizo Crude oil watasafishia wapi? ni lazima uwe na Refinery.
 
Mwamba wa Dunia USA wakisikia tutapigwa ban IMF, WORLD BANK, na kuzuiwa kuuza chochote duniani
Waulize ma Ayattollah wa Iran nchi yao inavyoteseka

Hapo unazungumzia crude Oil. Sasa sisi tukinunua hiyo crude oil tutaiweka wapi. Hatuna refinery wala nini. Sisi tupambane na petroli zetu tu

Tunaweza kununua kupitia Marafiki zetu China na India, hakuna vikwazo

Wao wanayo refinery, na watatupa unafuu

Makamba afufue TIPER , refinery yetu
 
Marafiki zetu China watatusaidia
Mleta mada unaongelea Crude oil "Mafuta ambayo hayajasafishwa" Hao India na China wanazo Refinery za kusafisha hiyo Crude oil,
Sasa Bongo wakinunua hizo Crude oil watasafishia wapi? ni lazima uwe na Refinery.


Tufufue refinery yetu TIPER

Tunajusifu kuwa walemavu?
 
Tuanze na upanuzi wa matumizi ya gesi yetu wenyewe ktk mitambo, usafiri na usafirishaji, majumbani, vyuoni nk!
Makaa ya mawe tunayo halafu tumeduwaa!

Kila siku utalii utalii na kufukuzana na Wamaasai Ngorongoro!
Mara uchumi wa bluu! Na huku kugombania mitumba ya ulaya!

Mswahili akiiba kura na kujipa ulaji, akivaa visuti na kuendeshwa kwenye V8 basssss! Humwambii kitu.
Wazo zuri,

Watanzania tuache kulia Lia

Russia ana export makaa ya mawe, sisi tunayo, tunashindwa kutumia

Gesi tunayo, hatutaki kutumia

Na gesi asili ya Russia ni cheaper than LNG

TUFUFUE REFINERY YETU TIPER , ilijengwa Kwa ubia na Italy, tuwaite Italy warudu
 
Wahenga walisema, 'Kufa kufaana'. Kwenye kila tatizo linalotokea hapa duniani huwa linafungua fursa kwa baadhi kufaidika nalo. Badala ya kukaa tunalialia linapotokea tatizo, tunapasw...
Huku wanawaza kupiga pesa, husikii wameshatangaza kupandisha bei hata kabla
 
Back
Top Bottom