Bei ya dhahabu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Tanzania imengia mkataba na Barrick ili kuiruhusu kampuni hiyo kuchimba dhahabu. Barrick imeingia mkataba huo kwa niaba ya shareholders wake wakiwemo watu binafsi na makampuni mbali mbali ulimwenguni. Wakati bei ya dhayabu 'inandelea kupaa' katika soko la dunia jana ilifikia $900 kwa ounce moja na kuongeza profit ya kampuni hiyo ambayo pia inawatajirisha shareholders wa kampuni hiyo, Tanzania hainufaiki na chochote kutokana na ongezeko hilo la bei ya dhahabu katika soko la dunia. Na hadi hii leo baadhi ya mikataba hiyo iliyosainiwa awamu ya fisadi Mkapa bado ni siri kubwa. Wakati tunasaini mkataba na Barrick bei ya dhahabu iliyowekwa inasemekana ilikuwa $238 ambayo sasa hivi imeshaongezeka mara tatu zaidi.

Thanks kwa Watanzania wenye uchungu wa nchi yao walioamua kuvujisha mkataba wa Buzwagi au vinginevyo na mkataba huo ungekuwa bado ni siri kali. Katika recommendations zitakazotolewa na kamati ya madini inabidi hii ya Tanzania kupewa 5% au zaidi ya ownership ya Barrick iwe moja ya recommendations hizo na kuongeza royalties kutoka 3% tunayopata sasa pamoja na kulipa kodi ili tuwe tunanufaika kila wakati bei ya dhahabu inapoongezeka.

Kuna wanauchumi wanadai kwamba kama uchumi wa Marekani ukiendelea kusuasua na currency yao kuendelea kuwa dhaifu kwa muda mrefu basi bei ya dhahabu inaweza kufikia hata $2,000 per ounce. Wakati ni huu tusikubali rasilimali zetu ziendelee kuwatajirisha wageni.
 
5% of ownership ni matusi makubwa. We should have at leas 50-60% ownership.
 
Mie nadhani ownership inabidi iwe 50% kwetu sisi wenye nchi, na wao wabakie na 50%. Kama hawataki waanze wao Karamagi na timu yote ilohusika kuandika mikataba ya Kikarl Peters.
 
Kwa maoni yangu binafsi. Watanzania vile vile tunaweza kuwa-share holder wa makampuni yanayoweka Tanzania.

Haya makampuni ni lazima yaanze kuuza share zao katika soko letu (Dar es salaam Stock Exchange )na hii inaweza kutupa faida kubwa zaidi.
 
Bin Maryam,'
Hiyo hatua ya kuwa shareholder ingekuwa item number 1 kwenye negotiations hata kabla ya koleo kuramba mchanga. Lakini ninavyosikia, wale waliofanya majadiliano, walijiwekea wenyewe shares pamoja na watoto wao, Tanzania ikibaki na zero.
 
Bin Maryam na Jasusi, point zenu znito sana. Katika harakati za kupambana na umaskini nchini, inabidi tuwe na sheria kuwa kampuni yoyote inayofanya biashara Tanzania kwa mtaji unaozidi kiwango fulani lazima iwe listed DSE.
 
Bin Maryam na Jasusi, point zenu znito sana. Katika harakati za kupambana na umaskini nchini, inabidi tuwe na sheria kuwa kampuni yoyote inayofanya biashara Tanzania kwa mtaji unaozidi kiwango fulani lazima iwe listed DSE.

Hii itasaidia sana kuinyanyua DSE ndani na nje ya Tanzania. Unataka kufanya biashara Tanzania basi lazima shares zako ziwe available kwa Watanzania kupitia DSE, vinginevyo funga virago vyako.
 
Hello Wana JF wenye uchungu.

Naomba niweke wazi kwanza sipingani na hoja zenu.Ila najaribu kusema nachojua.
Wakati Barrick wanaanzisha mgodi wao wa Kahama waliipa tanzani asilimia 15 ya hisa za company(mgodi) tena bure(free).Mwaka 2005 tanzania yenyewe ikawa zirudisha asilimia hizo kwenye mgodi.

Just imagine..ila kama unakumbukua vyema tanzania ilisha sema yenyewe haifanyo biashara..na dhahabu ni biashara vile tena soko lao liko New york Stock Exchange.Yenyewe inasema inakusanya kodi tu.

Sasa kama 15% walizirudisha hamsini wangeweza ku manage kweli?
Asilimia 50 mwanzijua....pesa mingi sana sio kwamba ni kitu lele mama tu.Kama wananunua Track za kuja kubebe mchanga kwa milioni 500 moja unajua tanzania inatakiwa kuchangia ngapi hapo kwa track hilo?Sio mwekezaji tu atakuwa analeta hayo magari sie tumelala tu.

Kuwa share holder si mchezo....lazima kuwe na pesa....kama viwanda vya nguo tumeshidwa kuendesha itawezekana mgodi?Mashimo yanayo chimbwa kwa ajiri tu ya utafiti,shimo moja linaweza cost badget ya wizara moja selikarini.Na uliza mashimo mangapi yanachibwa...kwa mwaka ni mashimo zaidi ya 600(200M)deep.
Wanajui Biashara na hisa pamoja na kuwa shareholder wanaweza eleza vyema.

Wizarani kwenyewe tukizungumzia katibu mkuu wa wizara ya madini...hajui hata site(mgodi)unajengwaje...upeo mdogo wa kuelewa.Unazungumza na katibu mkuu,au mkaguzi wa madini..unaona kabisa hajui kitu kama vile anafanya Homework.

Kinacho toke serikarini ni kuwa most of information zinakuwa ni siri kubwa migodi inalipa kodi zote ikiwa ni pamoja na Mrahaba(Royality),PAYE(Pay as you Earn),Na zile milioni 250 za kila wilaya...nani anajua haya?Vimefichwa ili wasije ulizwa baadae hizi kodi zinakwenda wapi?

Asubuhi njema.
 
Kwa maoni yangu binafsi. Watanzania vile vile tunaweza kuwa-share holder wa makampuni yanayoweka Tanzania.

Haya makampuni ni lazima yaanze kuuza share zao katika soko letu (Dar es salaam Stock Exchange )na hii inaweza kutupa faida kubwa zaidi.

..ungekuwa unagombea urais kwa agenda hii,kura yangu na za wale wote ambao ningeweza kuwashawishi ungepata!
 
Hii itasaidia sana kuinyanyua DSE ndani na nje ya Tanzania. Unataka kufanya biashara Tanzania basi lazima shares zako ziwe available kwa Watanzania kupitia DSE, vinginevyo funga virago vyako.

..kuna siku JK aliongelea hili sehemu,ila nadhani inawezekana liliishia palepale au jamaa hawakulifanyia kazi baada ya pale.
 
..ungekuwa unagombea urais kwa agenda hii,kura yangu na za wale wote ambao ningeweza kuwashawishi ungepata!

Siasa za Tanzania zina mambo mengi na nisingependa kujiingiza huko. Lakini makosa makubwa yanayofanyika sasa ni kuwanyima nafasi watanzania wa kawaida haki ya ku-access capital.
 
Mimi Mpaka Sasa Hivi Hakuna Kinachonifurahisha Ktk Mikataba Ya Aina Yoyote Ambayo Ilifanyika Ktk Kipindi Cha Utawala Wa Mkapa Na Tukisema Tuvunje Hii Mikataba Inakuwa Ni Ngumu Maana Yanaweza Kutukuta Yale Yaliyoikuta Zimbabwe Ya Leo Lakini Pia Nina Mbinu Moja Nzuri Je?ni Kwanini Tusianzishe Japo Vita Hapo Tanzania Kati Ya Wahindi Na Waswahili Kwa Madai Kuwa Wanatuibia Na Kuhamisha Pesa Zetu Na Wizi Ktk Benk Zetu Maana Ushahidi Si Tunao Halafu U.n Wataona Kuwa Ni Kweli Maana Kwa Ninavyojua Mimi Nchi Ikishakuwa Na Vita Mikataba Mingi Huwa Inakufaga Au Kama Kuna Mwenye Mtizamo Tofauti Juu Ya Kufuta Hii Mikataba Ya Kizandiki Atoe
 
Mimi kwa mawazo yangu Tanzania inatakiwa kuchukua royalities kwenye gold na siyo cash. Tax ya 25% wachukue cash kwasababu huwezi kuchagua ni namna gani ulipwe tax lakini royalities please tanzania chukua hiyo 3% kwenye gold kwani inapanda thamani na itasaidia kupandisha thamani ya pesa kama canada.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom