BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Umeme wazua balaa
• CHADEMA, wasomi, wanaharakati wapinga bei mpya
na Mwandishi wetu
Tanzania Daima
BEI mpya ya umeme iliyotangazwa juzi na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (Ewura), imezua balaa kubwa baada ya makundi ya kijamii na kisiasa kuipinga kwa madai kuwa itasababisha ugumu wa maisha kwa wananchi.
Makundi hayo kwa nyakati tofauti jana, yalionyesha kukerwa kwao na jinsi serikali ilivyoamua kukosa na huruma kwa watu wake ambao wanakabiliwa na ugumu wa maisha.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, John Mnyika (CHADEMA), pamoja na kuahidi kutoa tamko rasmi wakati wowote, alisema ongezeko hilo ni matokeo ya serikali kudharau maoni ya kambi ya upinzani yaliyotolewa wakati wa kikao cha Bunge mwaka jana.
Mnyika alisema Ewura haijaonyesha kwa ukamilifu iwapo njia zote zimetumika katika kupunguza gharama za uendeshaji za Tanesco mpaka kufikia hatua ya kupandisha gharama za huduma ya umeme kwa kiwango cha asilimia 40.29.
Alisema akiwa waziri kivuli wa wizara hiyo, alitarajia kwamba serikali ingefunga mkanda na kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima ikiwemo ya posho za vikao na kupanua wigo wa mapato ikiwemo katika sekta ya madini na kuingozea fedha Tanesco bila kubebesha mzigo mkubwa kwa wananchi wa kawaida kama CHADEMA ilivyopendekeza bungeni Julai 15 na Agosti 13, 2011.
Pamoja na matatizo ya kifedha ya Tanesco ambayo serikali inapaswa kuyashughulikia kwa njia mbadala katika kipindi hiki cha mpito gharama kubwa za uzalishaji zinazolikabili shirika zinachangiwa na ufisadi wa muda mrefu katika mikataba ikiwemo ya uzalishaji wa gesi na ukodishaji wa mitambo ya kufua na pia maamuzi ya kukopa kibiashara katika kutekeleza mpango huo.
"Wananchi wakumbuke kwamba hii ni mara ya pili katika kipindi cha takriban mwaka mmoja kwa Tanesco kupandisha bei ya umeme; mara ya kwanza ikiwa mwezi Januari 2011 ambapo umeme ulipanda kwa asilimia 18.5 na kuchangia katika kupanda kwa gharama za uzalishaji katika nchi na kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi," alisema Mnyika.
Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo alisema serikali kabla ya kuongeza bei ya umeme kwa Watanzania wa kawaida, ingewaeleze wananchi imewapunguzia mzigo kiasi gani kwa kupitia upya mikataba ya kifisadi inayolinyonya Shirika la Umeme Tanzania kama ilivyopendekezwa kwenye ripoti mbalimbali ikiwemo maazimio ya Bunge ya mwaka 2008 juu ya mkataba wa ukodishaji wa mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Richmond Develepment Company LLC ambapo orodha ya mikataba na makampuni mengine ilitajwa ambayo mpaka sasa inaendelea kuipa mzigo Tanesco ikiwemo ya Songas na Pan African Energy Tanzania.
Alikumbusha jinsi alivyoionya serikali kuepuka uamuzi wa kuchukua mikopo ya kibiashara yenye riba kubwa ambayo imeongeza zaidi gharama za uzalishaji wa umeme na hivyo kuifanya Tanesco iongeze zaidi bei ya umeme kwa wateja.
"Uamuzi huu wa kupandisha kwa kiwango kikubwa bei ya umeme utasababisha ongezeko la ziada la mfumko wa bei hali ambayo ni tishio kwa usalama na uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa ujumla.
"Serikali izingatie kwamba mfumko wa bei nchini umeongezeka na bidhaa zinazochangia mfumko huo kwa kiwango kikubwa ni vyakula, mafuta na umeme.
Kupanda kwa bei kwenye sekta ya nishati pekee kumechangia kwa kiwango kikubwa kupanda kwa gharama za maisha, sasa viongozi wajiulize itakuwaje baada ya kupanda kwa umeme?"
Profesa Baregu: Ni maumivu kwa mwananchi
Mmoja wa wasomi na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha SAUT, Profesa Mwesigwa Baregu, alisema ongezeko hilo la umeme licha ya kupingana na kampeni ya utunzaji wa mazingira, litachangia ongezeko la bei kwa mtumiaji wa kawaida ambaye ni mwananchi.
Alisema kutokana na nishati hiyo ya umeme kuzidi kuwa aghali wananchi watarudi nyuma na kuanza kutumia kuni na hivyo kuharibu vyanzo vya maji na kusababisha kutopatikana kwa mvua kwa wakati.
Baregu alisema serikali ingepaswa kueleza kwa ufasaha hasa ni sababu gani iliyosababisha kupandisha bei kwa nishati hiyo na itakuwa kwa muda gani kwa kuwa kwa sasa imekuja kama zima moto na kuongeza kwamba inahitajika mabadiliko ya sera katika suala zima la nishati ya umeme.
Naye mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Uchumi na Takwimu, Profesa Morisi Mbago, alisema ongezeka la asilimia iliyotangazwa na Ewura limekuwa kubwa mno ukilinganisha na kipato halisi cha wananchi.
Profesa Mbago alisema bei ya umeme ya sasa, wananchi hawaimudu na ongezeko hilo jipya litawaumiza zaidi na kufanya maisha yao kuwa magumu kwao.
"Kwa sasa kila bidhaa sokoni iko juu sasa hiyo bei mpya ya umeme itakapoanza kutumika rasmi kesho ni wazi kwamba hali itazidi kuwa mbaya kwa wananchi ambao wengi wanaishi kwa mlo mmoja," alisema.
Huko Dodoma, baadhi ya wananchi wamepinga vikali kupanda kwa gharama za umeme kwa madai kuwa kutasababisha gharama za maisha kuwa juu.
Mmoja wa wafanyabiashara maarufu mjini hapa Peter Olomi alisema kuwa kwa sasa maisha bora kwa Mtanzania ni kitendawili na kwamba kitendo cha kupanda kwa gharama ya umeme kitayaathiri makundi yote ya kijamii.
Olomi alidai Watanzania wategemee kuona mfumko wa bei, ukosefu wa ajira ikiwa ni pamoja na makampuni mengi kufilisika.
"Fikiria kwa sasa maisha yako juu, mafuta yanauzwa kwa bei kubwa wakati shilingi yetu haina thamani na sasa angalia umeme umepanda bei unategemea wananchi kuishi maisha gani?
"Kwa sasa kila kitu kitapanda bei na atakayeumia zaidi ni mlaji wa mwisho," alisema Olomi.
• CHADEMA, wasomi, wanaharakati wapinga bei mpya
na Mwandishi wetu
Tanzania Daima
BEI mpya ya umeme iliyotangazwa juzi na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (Ewura), imezua balaa kubwa baada ya makundi ya kijamii na kisiasa kuipinga kwa madai kuwa itasababisha ugumu wa maisha kwa wananchi.
Makundi hayo kwa nyakati tofauti jana, yalionyesha kukerwa kwao na jinsi serikali ilivyoamua kukosa na huruma kwa watu wake ambao wanakabiliwa na ugumu wa maisha.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, John Mnyika (CHADEMA), pamoja na kuahidi kutoa tamko rasmi wakati wowote, alisema ongezeko hilo ni matokeo ya serikali kudharau maoni ya kambi ya upinzani yaliyotolewa wakati wa kikao cha Bunge mwaka jana.
Mnyika alisema Ewura haijaonyesha kwa ukamilifu iwapo njia zote zimetumika katika kupunguza gharama za uendeshaji za Tanesco mpaka kufikia hatua ya kupandisha gharama za huduma ya umeme kwa kiwango cha asilimia 40.29.
Alisema akiwa waziri kivuli wa wizara hiyo, alitarajia kwamba serikali ingefunga mkanda na kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima ikiwemo ya posho za vikao na kupanua wigo wa mapato ikiwemo katika sekta ya madini na kuingozea fedha Tanesco bila kubebesha mzigo mkubwa kwa wananchi wa kawaida kama CHADEMA ilivyopendekeza bungeni Julai 15 na Agosti 13, 2011.
Pamoja na matatizo ya kifedha ya Tanesco ambayo serikali inapaswa kuyashughulikia kwa njia mbadala katika kipindi hiki cha mpito gharama kubwa za uzalishaji zinazolikabili shirika zinachangiwa na ufisadi wa muda mrefu katika mikataba ikiwemo ya uzalishaji wa gesi na ukodishaji wa mitambo ya kufua na pia maamuzi ya kukopa kibiashara katika kutekeleza mpango huo.
"Wananchi wakumbuke kwamba hii ni mara ya pili katika kipindi cha takriban mwaka mmoja kwa Tanesco kupandisha bei ya umeme; mara ya kwanza ikiwa mwezi Januari 2011 ambapo umeme ulipanda kwa asilimia 18.5 na kuchangia katika kupanda kwa gharama za uzalishaji katika nchi na kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi," alisema Mnyika.
Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo alisema serikali kabla ya kuongeza bei ya umeme kwa Watanzania wa kawaida, ingewaeleze wananchi imewapunguzia mzigo kiasi gani kwa kupitia upya mikataba ya kifisadi inayolinyonya Shirika la Umeme Tanzania kama ilivyopendekezwa kwenye ripoti mbalimbali ikiwemo maazimio ya Bunge ya mwaka 2008 juu ya mkataba wa ukodishaji wa mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Richmond Develepment Company LLC ambapo orodha ya mikataba na makampuni mengine ilitajwa ambayo mpaka sasa inaendelea kuipa mzigo Tanesco ikiwemo ya Songas na Pan African Energy Tanzania.
Alikumbusha jinsi alivyoionya serikali kuepuka uamuzi wa kuchukua mikopo ya kibiashara yenye riba kubwa ambayo imeongeza zaidi gharama za uzalishaji wa umeme na hivyo kuifanya Tanesco iongeze zaidi bei ya umeme kwa wateja.
"Uamuzi huu wa kupandisha kwa kiwango kikubwa bei ya umeme utasababisha ongezeko la ziada la mfumko wa bei hali ambayo ni tishio kwa usalama na uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa ujumla.
"Serikali izingatie kwamba mfumko wa bei nchini umeongezeka na bidhaa zinazochangia mfumko huo kwa kiwango kikubwa ni vyakula, mafuta na umeme.
Kupanda kwa bei kwenye sekta ya nishati pekee kumechangia kwa kiwango kikubwa kupanda kwa gharama za maisha, sasa viongozi wajiulize itakuwaje baada ya kupanda kwa umeme?"
Profesa Baregu: Ni maumivu kwa mwananchi
Mmoja wa wasomi na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha SAUT, Profesa Mwesigwa Baregu, alisema ongezeko hilo la umeme licha ya kupingana na kampeni ya utunzaji wa mazingira, litachangia ongezeko la bei kwa mtumiaji wa kawaida ambaye ni mwananchi.
Alisema kutokana na nishati hiyo ya umeme kuzidi kuwa aghali wananchi watarudi nyuma na kuanza kutumia kuni na hivyo kuharibu vyanzo vya maji na kusababisha kutopatikana kwa mvua kwa wakati.
Baregu alisema serikali ingepaswa kueleza kwa ufasaha hasa ni sababu gani iliyosababisha kupandisha bei kwa nishati hiyo na itakuwa kwa muda gani kwa kuwa kwa sasa imekuja kama zima moto na kuongeza kwamba inahitajika mabadiliko ya sera katika suala zima la nishati ya umeme.
Naye mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Uchumi na Takwimu, Profesa Morisi Mbago, alisema ongezeka la asilimia iliyotangazwa na Ewura limekuwa kubwa mno ukilinganisha na kipato halisi cha wananchi.
Profesa Mbago alisema bei ya umeme ya sasa, wananchi hawaimudu na ongezeko hilo jipya litawaumiza zaidi na kufanya maisha yao kuwa magumu kwao.
"Kwa sasa kila bidhaa sokoni iko juu sasa hiyo bei mpya ya umeme itakapoanza kutumika rasmi kesho ni wazi kwamba hali itazidi kuwa mbaya kwa wananchi ambao wengi wanaishi kwa mlo mmoja," alisema.
Huko Dodoma, baadhi ya wananchi wamepinga vikali kupanda kwa gharama za umeme kwa madai kuwa kutasababisha gharama za maisha kuwa juu.
Mmoja wa wafanyabiashara maarufu mjini hapa Peter Olomi alisema kuwa kwa sasa maisha bora kwa Mtanzania ni kitendawili na kwamba kitendo cha kupanda kwa gharama ya umeme kitayaathiri makundi yote ya kijamii.
Olomi alidai Watanzania wategemee kuona mfumko wa bei, ukosefu wa ajira ikiwa ni pamoja na makampuni mengi kufilisika.
"Fikiria kwa sasa maisha yako juu, mafuta yanauzwa kwa bei kubwa wakati shilingi yetu haina thamani na sasa angalia umeme umepanda bei unategemea wananchi kuishi maisha gani?
"Kwa sasa kila kitu kitapanda bei na atakayeumia zaidi ni mlaji wa mwisho," alisema Olomi.