Deus F Mallya
JF-Expert Member
- Jul 28, 2011
- 705
- 440
Tanzania itakwama kabla ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 2015 kwa sababu nyingi lakini kwa leo tuiangalie hii:
Mchakato wa Katiba Mpya:
Itakumbukwa kuwa Serikali imeamua kuanzisha mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya ambapo Waziri Mkuu alikaririwa akisema kuwa ifikapo mwaka 2014 katiba hiyo itakuwa tayari. Hata hivyo kuna vikwazo vikubwa vya kisheria na vya kisiasa kwenye sheria yenyewe iliyoweka huo utaratibu wa kuandikwa kwa katiba hiyo. Vikwazo hivyo vina nguvu ya Kuiangusha Serikali nzima kabla ya mwaka 2015; Kwanza, Sheria hiyo pamoja na mambo mengine inataka wazanzibari zaidi ya 50% wapige kura kuikubali Rasimu hiyo ya katiba itakapokuwa tayari na kadhalika huko Tanzania bara.
Ukweli ulio wazi ni kuwa suala la Muungano limekuwa hadithi inayokosa tafsiri halisi kwa miaka kadhaa sasa. Hata hivyo Muungano umeendelea kukosa tafsiri halisi na ya Ukweli kutokana na usiri mkubwa unaoendelea kufichwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ama kwa kuogopa kuutibu muungano ama kwa sababu zao za 'Kiintelijensia'..
Wakati huu fukuto la Wazanzibari kudai muundo mpya wa Muungano limeshamiri hasa kwenye mchakato huu wa katiba unaoendelea hata wengine kudai kuwa Muungano uvunjwe tuanze upya.Serikali kwa sasa haina namna ya kukwepa wajibu huu wa kuwapa wananchi wake uhuru wa kuamua na kuchagua kama wanataka Muungano au la: na kama wanautaka, wanautaka Muungano wa Sura ipi. (Muungano wa sasa ni kama 'Shombeshombe'). Wazanzibari hawako tayari kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia zinazotakiwa kama bado Tanganyika itakuwa haina Katiba yake na Suala la muungano kurekebishwa.
Kukwamishwa huko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutakuwa ni kukwama kwa Serikali mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kulinusuru hili; hata kama Serikali itaamua kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika bado itakuwa imekwama kabla ya mwaka 2015 kwa sababu itabidi kiwepo kipindi cha mpito ambapo nchi inaweza kuongozwa na Jaji Mkuu kwa Siku 90 kabla ya uchaguzi Mkuu (Si ule wa 2015). Baada ya uchaguzi ndipo Rais ajaye aanzishe mchakato wa kuandikwa kwa Katiba ya Tanganyika na baadaye referendum ya Muungano na kisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa hapa Serikali ilipo ikienda Mbele itakwama;Ikirudi nyuma itakwama. No way Out.
Naomba kutoa hoja.
Mchakato wa Katiba Mpya:
Itakumbukwa kuwa Serikali imeamua kuanzisha mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya ambapo Waziri Mkuu alikaririwa akisema kuwa ifikapo mwaka 2014 katiba hiyo itakuwa tayari. Hata hivyo kuna vikwazo vikubwa vya kisheria na vya kisiasa kwenye sheria yenyewe iliyoweka huo utaratibu wa kuandikwa kwa katiba hiyo. Vikwazo hivyo vina nguvu ya Kuiangusha Serikali nzima kabla ya mwaka 2015; Kwanza, Sheria hiyo pamoja na mambo mengine inataka wazanzibari zaidi ya 50% wapige kura kuikubali Rasimu hiyo ya katiba itakapokuwa tayari na kadhalika huko Tanzania bara.
Ukweli ulio wazi ni kuwa suala la Muungano limekuwa hadithi inayokosa tafsiri halisi kwa miaka kadhaa sasa. Hata hivyo Muungano umeendelea kukosa tafsiri halisi na ya Ukweli kutokana na usiri mkubwa unaoendelea kufichwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ama kwa kuogopa kuutibu muungano ama kwa sababu zao za 'Kiintelijensia'..
Wakati huu fukuto la Wazanzibari kudai muundo mpya wa Muungano limeshamiri hasa kwenye mchakato huu wa katiba unaoendelea hata wengine kudai kuwa Muungano uvunjwe tuanze upya.Serikali kwa sasa haina namna ya kukwepa wajibu huu wa kuwapa wananchi wake uhuru wa kuamua na kuchagua kama wanataka Muungano au la: na kama wanautaka, wanautaka Muungano wa Sura ipi. (Muungano wa sasa ni kama 'Shombeshombe'). Wazanzibari hawako tayari kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia zinazotakiwa kama bado Tanganyika itakuwa haina Katiba yake na Suala la muungano kurekebishwa.
Kukwamishwa huko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutakuwa ni kukwama kwa Serikali mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kulinusuru hili; hata kama Serikali itaamua kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika bado itakuwa imekwama kabla ya mwaka 2015 kwa sababu itabidi kiwepo kipindi cha mpito ambapo nchi inaweza kuongozwa na Jaji Mkuu kwa Siku 90 kabla ya uchaguzi Mkuu (Si ule wa 2015). Baada ya uchaguzi ndipo Rais ajaye aanzishe mchakato wa kuandikwa kwa Katiba ya Tanganyika na baadaye referendum ya Muungano na kisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa hapa Serikali ilipo ikienda Mbele itakwama;Ikirudi nyuma itakwama. No way Out.
Naomba kutoa hoja.