Behind the Scene: Serikali itakwama Kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015

Deus F Mallya

JF-Expert Member
Jul 28, 2011
705
440
Tanzania itakwama kabla ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 2015 kwa sababu nyingi lakini kwa leo tuiangalie hii:

Mchakato wa Katiba Mpya:

Itakumbukwa kuwa Serikali imeamua kuanzisha mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya ambapo Waziri Mkuu alikaririwa akisema kuwa ifikapo mwaka 2014 katiba hiyo itakuwa tayari. Hata hivyo kuna vikwazo vikubwa vya kisheria na vya kisiasa kwenye sheria yenyewe iliyoweka huo utaratibu wa kuandikwa kwa katiba hiyo. Vikwazo hivyo vina nguvu ya Kuiangusha Serikali nzima kabla ya mwaka 2015; Kwanza, Sheria hiyo pamoja na mambo mengine inataka wazanzibari zaidi ya 50% wapige kura kuikubali Rasimu hiyo ya katiba itakapokuwa tayari na kadhalika huko Tanzania bara.

Ukweli ulio wazi ni kuwa suala la Muungano limekuwa hadithi inayokosa tafsiri halisi kwa miaka kadhaa sasa. Hata hivyo Muungano umeendelea kukosa tafsiri halisi na ya Ukweli kutokana na usiri mkubwa unaoendelea kufichwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ama kwa kuogopa kuutibu muungano ama kwa sababu zao za 'Kiintelijensia'..

Wakati huu fukuto la Wazanzibari kudai muundo mpya wa Muungano limeshamiri hasa kwenye mchakato huu wa katiba unaoendelea hata wengine kudai kuwa Muungano uvunjwe tuanze upya.Serikali kwa sasa haina namna ya kukwepa wajibu huu wa kuwapa wananchi wake uhuru wa kuamua na kuchagua kama wanataka Muungano au la: na kama wanautaka, wanautaka Muungano wa Sura ipi. (Muungano wa sasa ni kama 'Shombeshombe'). Wazanzibari hawako tayari kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia zinazotakiwa kama bado Tanganyika itakuwa haina Katiba yake na Suala la muungano kurekebishwa.

Kukwamishwa huko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutakuwa ni kukwama kwa Serikali mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kulinusuru hili; hata kama Serikali itaamua kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika bado itakuwa imekwama kabla ya mwaka 2015 kwa sababu itabidi kiwepo kipindi cha mpito ambapo nchi inaweza kuongozwa na Jaji Mkuu kwa Siku 90 kabla ya uchaguzi Mkuu (Si ule wa 2015). Baada ya uchaguzi ndipo Rais ajaye aanzishe mchakato wa kuandikwa kwa Katiba ya Tanganyika na baadaye referendum ya Muungano na kisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa hapa Serikali ilipo ikienda Mbele itakwama;Ikirudi nyuma itakwama. No way Out.

Naomba kutoa hoja.
 
Kukwamishwa huko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutakuwa ni kukwama kwa Serikali mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kulinusuru hili; hata kama Serikali itaamua kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika bado itakuwa imekwama kabla ya mwaka 2015 kwa sababu itabidi kiwepo kipindi cha mpito ambapo nchi inaweza kuongozwa na Jaji Mkuu kwa Siku 90 kabla ya uchaguzi Mkuu (Si ule wa 2015). Baada ya uchaguzi ndipo Rais ajaye aanzishe mchakato wa kuandikwa kwa Katiba ya Tanganyika na baadaye referendum ya Muungano na kisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

HApo kwenye red: naomba ufafanuzi. Ni utaratibu wa kwenye katiba au??
 
Pia Jaji Sinde Warioba mwenyekiti wakamati ya katiba mpya alisistiza katiba mpya kwa vyovyote vile lazma izinduliwe April 2014. nimeipenda hii... " mtu kati" hakuna kwenda kulia wala kushoto! hapo tamu!
 
Pia Jaji Sinde Warioba mwenyekiti wakamati ya katiba mpya alisistiza katiba mpya kwa vyovyote vile lazma izinduliwe April 2014. nimeipenda hii... " mtu kati" hakuna kwenda kulia wala kushoto! hapo tamu!

Mkuu hao wanaokazana kusisitiza pengine wanajaribu kujisahaulisha ukweli huu. Hakuna katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila Katiba ya Tanganyika.
 
...kwa majaji hawa tulionao aina ya akina siju "Mbaruku"...kuna haja ya watanzania kutafakali kwa kina hatma ya nchi yetu...sioni tofauti ya hii serikali dhaifu na huu muhimili feki wa sheria...
 
...kwa majaji hawa tulionao aina ya akina siju "Mbaruku"...kuna haja ya watanzania kutafakali kwa kina hatma ya nchi yetu...sioni tofauti ya hii serikali dhaifu na huu muhimili feki wa sheria...

Ifuatwe sheria au isifuatwe bro!.. Mambo mengine hayakwepeki.
 
Ni ukweli usiopingika, hili suala la Muungano serikali haitaki kulitafutia ufumbuzi wa kudumu, lazima litaleta shida sana. Tatizo si kulikimbia, ni kulikabili na kulitafutia njia ya kulitatua. Muungano lazima ujadiliwe kwa marefu na mapana na hatua za makusudi lazima zichukuliwe kulitatua hili, hatuwezi kulitatua kwa ujanja ujanja na kauli nyepesi. Mizengo Kayanza Pinda alijaribu kuligusia lakini naona nae kafyata mkia baada ya watu kuja juu.
Kwa Maoni yangu, muungano mzuri ni wa serikali Moja au Tatu, huu wa sasa ni kujidanganya tu!
 
Mkuu hao wanaokazana kusisitiza pengine wanajaribu kujisahaulisha ukweli huu. Hakuna katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila Katiba ya Tanganyika.

Mkuu Deus,
Mimi wasiwasi wangu ni kuwa tutarejea katika ile katiba ya zamani. Kwani rasimu ya katiba iliyopitishwa inasema kuwa endapo itashindikana kupatikana kwa katiba mpya, basi katiba ya zamani itaendelea. Sijui hili unalizungumzia je?
 
Mkuu Deus,
Mimi wasiwasi wangu ni kuwa tutarejea katika ile katiba ya zamani. Kwani rasimu ya katiba iliyopitishwa inasema kuwa endapo itashindikana kupatikana kwa katiba mpya, basi katiba ya zamani itaendelea. Sijui hili unalizungumzia je?

Kwa kukusahihisha ni kuwa iliyopitishwa ni Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na si Rasimu ya Katiba.

Kuhusu kurudi kwenye katiba hii ya sasa bado ni hatari kubwa sana kwa watawala wetu kwa sababu wananchi watapoteza Political Legitimacy kwa serikali kwa sababu yapo mambo zaidi ya 200 ambayo ni lazima yabadilishwe kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015.. Hapo naona maandamano makubwa kuishinikiza Serikali itekeleze madai ya Wazanzibari juu ya Muungano baada ya kuikwamisha Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... Wengine tupo pia tutakaoandamana kudai Katiba ya Tanganyika.
 
Ni ukweli usiopingika, hili suala la Muungano serikali haitaki kulitafutia ufumbuzi wa kudumu, lazima litaleta shida sana. Tatizo si kulikimbia, ni kulikabili na kulitafutia njia ya kulitatua. Muungano lazima ujadiliwe kwa marefu na mapana na hatua za makusudi lazima zichukuliwe kulitatua hili, hatuwezi kulitatua kwa ujanja ujanja na kauli nyepesi. Mizengo Kayanza Pinda alijaribu kuligusia lakini naona nae kafyata mkia baada ya watu kuja juu.
Kwa Maoni yangu, muungano mzuri ni wa serikali Moja au Tatu, huu wa sasa ni kujidanganya tu!

Hilo la Serikali moja nakubaliana nalo lakini bado sijaona Mzanzibari aliye tayari kulikubali. Kwa mfano: Rais wa Zanzibar anaapa kwa kutumia katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;Lakini anailinda katiba ya Zanzibar.. Uhalali wa Katiba ya Zanzibar nao ni 'Shombeshombe' kwa sababu wala haijulikani na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Kwakuwa Bunge ndicho chombo cha kutunga sheria).. Bado napata utata wa Jamhuri yenye Katiba Mbili;Zimetoka wapi?
 
Kama haya unayoyasema yatakuwa hivyo basi uchaguzi hautafanyika 2015

Mkuu ndicho ninachomaanisha; Tatizo wakuu wetu hadi wakwame kabisa ndipo wanafanya maamuzi.. Huku wanakoelekea ni kukwama watakakoshindwa kujinasua na badala yake ni kuanguka.
 
Tanzania itakwama kabla ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 2015 kwa sababu nyingi lakini kwa leo tuiangalie hii:

Mchakato wa Katiba Mpya:
Itakumbukwa kuwa Serikali imeamua kuanzisha mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya ambapo Waziri Mkuu alikaririwa akisema kuwa ifikapo mwaka 2014 katiba hiyo itakuwa tayari. Hata hivyo kuna vikwazo vikubwa vya kisheria na vya kisiasa kwenye sheria yenyewe iliyoweka huo utaratibu wa kuandikwa kwa katiba hiyo. Vikwazo hivyo vina nguvu ya Kuiangusha Serikali nzima kabla ya mwaka 2015; Kwanza, Sheria hiyo pamoja na mambo mengine inataka wazanzibari zaidi ya 50% wapige kura kuikubali Rasimu hiyo ya katiba itakapokuwa tayari na kadhalika huko Tanzania bara.

Ukweli ulio wazi ni kuwa suala la Muungano limekuwa hadithi inayokosa tafsiri halisi kwa miaka kadhaa sasa. Hata hivyo Muungano umeendelea kukosa tafsiri halisi na ya Ukweli kutokana na usiri mkubwa unaoendelea kufichwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ama kwa kuogopa kuutibu muungano ama kwa sababu zao za 'Kiintelijensia'..

Wakati huu fukuto la Wazanzibari kudai muundo mpya wa Muungano limeshamiri hasa kwenye mchakato huu wa katiba unaoendelea hata wengine kudai kuwa Muungano uvunjwe tuanze upya.Serikali kwa sasa haina namna ya kukwepa wajibu huu wa kuwapa wananchi wake uhuru wa kuamua na kuchagua kama wanataka Muungano au la: na kama wanautaka, wanautaka Muungano wa Sura ipi. (Muungano wa sasa ni kama 'Shombeshombe'). Wazanzibari hawako tayari kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia zinazotakiwa kama bado Tanganyika itakuwa haina Katiba yake na Suala la muungano kurekebishwa.

Kukwamishwa huko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutakuwa ni kukwama kwa Serikali mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Kulinusuru hili; hata kama Serikali itaamua kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika bado itakuwa imekwama kabla ya mwaka 2015 kwa sababu itabidi kiwepo kipindi cha mpito ambapo nchi inaweza kuongozwa na Jaji Mkuu kwa Siku 90 kabla ya uchaguzi Mkuu (Si ule wa 2015). Baada ya uchaguzi ndipo Rais ajaye aanzishe mchakato wa kuandikwa kwa Katiba ya Tanganyika na baadaye referendum ya Muungano na kisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa hapa Serikali ilipo ikienda Mbele itakwama;Ikirudi nyuma itakwama. No way Out.

Naomba kutoa hoja.
madhara ya bangi za gerezani.
 
Back
Top Bottom