Bedroom diplomacy is urgently needed!!!

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Katika baadhi ya mijadala nimeshawishika kuamini kuwa watu wengi kwenye mahusiano wana mapungufu ya jinsi ya kuwasiliana. Kwa hiyo kuna ulazima wa kuwa na kungwi au wataalamu wa kutusaidia katika hili. Mimi siyo mmoja wao lakini naamini naweza kuwa na ushuhuda wa maisha yangu!

Inaeleweka kabisa katika jamii zetu kwamba wanaume hunogesha maongezi yao wakati wanapata moja baridi na moja ya moto. Katika kikao cha namna hiyo hata mambo makubwa yanaweza kujadiliwa bila kuzua jazba. Je wanawake hongea mambo yao wapi na lini? Je mambo ya ndani (katika mahusiano) yanaweza kuongelewa wakati wowote na kwa lugha (pamoja na tune) yoyote?
 
Wanawake wanaongelea mambo yao kwenye saluni za nywele, na huwa si kwa nia ya kujenga, bali kuweka petroli kwenye moto!...

Pamoja na juhudi zote za kuandaliwa wakati wa kuyaingia maisha ya unyumba, hii haisaidii kitu, maana shughuli hizo(kitchen party, send-off etc etc) pia zinakuwa na dalili zote za kimeta!

Kwa wanaume, ndugu yangu DarkCity, si wote wanahudhuria kwenye maeneo uliyotaja, labda tuseme tu kuwa wanaume wamejaliwa kipawa hicho cha uongozi toka mwanzo, na wanaweza kumaliza mambo mengi pasipo kucharurana.
 
haya wazoefu!TWENDE KAZI...!mi nikichangia hapo nitakuwa mzushi
 
[
Wanawake wanaongelea mambo yao kwenye saluni za nywele, na huwa si kwa nia ya kujenga, bali kuweka petroli kwenye moto!...

Pamoja na juhudi zote za kuandaliwa wakati wa kuyaingia maisha ya unyumba, hii haisaidii kitu, maana shughuli hizo(kitchen party, send-off etc etc) pia zinakuwa na dalili zote za kimeta!


Itabidi waje wenyewe watueleze. Kwa nini wanaendekeza hicho kimeta!!

Kwa wanaume, ndugu yangu DarkCity, si wote wanahudhuria kwenye maeneo uliyotaja, labda tuseme tu kuwa wanaume wamejaliwa kipawa hicho cha uongozi toka mwanzo, na wanaweza kumaliza mambo mengi pasipo kucharurana.


Hapo ndugu yangu umeongea kama Bishop. Naamini mjadala haujafungwa.
 
Katika baadhi ya mijadala nimeshawishika kuamini kuwa watu wengi kwenye mahusiano wana mapungufu ya jinsi ya kuwasiliana. Kwa hiyo kuna ulazima wa kuwa na kungwi au wataalamu wa kutusaidia katika hili. Mimi siyo mmoja wao lakini naamini naweza kuwa na ushuhuda wa maisha yangu!

Inaeleweka kabisa katika jamii zetu kwamba wanaume hunogesha maongezi yao wakati wanapata moja baridi na moja ya moto. Katika kikao cha namna hiyo hata mambo makubwa yanaweza kujadiliwa bila kuzua jazba. Je wanawake hongea mambo yao wapi na lini? Je mambo ya ndani (katika mahusiano) yanaweza kuongelewa wakati wowote na kwa lugha (pamoja na tune) yoyote?
Unajua hii breakdown ya communication kwenye ndoa inaanzia wapi, nyingine ni hapa JF watu wamezoea kuambiwa asante hata kwa jambo la kipumbavu kabisa kwahiyo akienda nyumbani anataka mke au mume ammpe treatment kama za uku kwenye mtandao ambako unapewa asante saa nyingine hata na ibilisi maaanake bwana tusidanganyane hii ni mitandao tu kwahiyo chukua yale bora ya kipuuzi achana nayo na wengine comments zao za kifreemasons na watu wengine kwa upofu wao wa kuwaza wanazichukua hizo na kwenda kuziapply makwao, imekula kwenu.

Kwa walionielewa wamenielewa kwa wasionielewa ooh! ooh! kidedea
 
Unajua hii breakdown ya communication kwenye ndoa inaanzia wapi, nyingine ni hapa JF watu wamezoea kuambiwa asante hata kwa jambo la kipumbavu kabisa kwahiyo akienda nyumbani anataka mke au mume ammpe treatment kama za uku kwenye mtandao ambako unapewa asante saa nyingine hata na ibilisi maaanake bwana tusidanganyane hii ni mitandao tu kwahiyo chukua yale bora ya kipuuzi achana nayo na wengine comments zao za kifreemasons na watu wengine kwa upofu wao wa kuwaza wanazichukua hizo na kwenda kuziapply makwao, imekula kwenu.

Kwa walionielewa wamenielewa kwa wasionielewa ooh! ooh! kidedea

Nimejaribu kukuelewa lakini bado naona vinyota nyota. Bahati mbaya wadau wameshaanza mipango ya week end. Ngoja tusubiri labda tutapata mtu wa kutusaidia.
 
haya wazoefu!TWENDE KAZI...!mi nikichangia hapo nitakuwa mzushi

Hebu rudi basi, mbona umetokomea? Bado tunahitaji vitu vyako, hata kama ni theory, uwanja wa kwenda kufanyia mazoezi siku hizi hulipii!!
 
Nimejaribu kukuelewa lakini bado naona vinyota nyota. Bahati mbaya wadau wameshaanza mipango ya week end. Ngoja tusubiri labda tutapata mtu wa kutusaidia.
uko mnjini ndio mnaanza weekend sio kwahiyo brain zimekaa kiweekend pia, ni jambo jema pia kwa afya ya mwili na akili
 
Ah mie wangu tunaongelea popote jikoni, bafuni na hata tukiwa tunacheza wenywe! hihi ihiih ihiihi
 
Back
Top Bottom