Beda baada ya ukabila sasa umehitimisha kwa kumweka Eric mwanao kuila UCC?

Mjadala huu hauna tofauti na ule wa TRA na mingine ya aina hii tuliyowahi kuiona hapa JF.

Mleta hoja na wengine wanaomuunga mkono wametoa ushahidi wa kuwepo wahaya wengi hapo UCC kuwa ni ushahidi unaojitosheleza kuhitimisha kuwa pale pana ukabila. Hiki ni kigezo kimoja mhimu, lakini nadhani hakiwezi kujitosheleza kuhitimisha kuwepo kwa ukabila bila ya kuwa na vidokezo vingine vinavyokijengea nguvu.

Mimi ningependa tupewe ushahidi unaoonyesha kwamba kuna watu walionyimwa haki yao ya kuajiliwa au kupewa huduma kwa sababu tu ya ukabila uliojijenga pale UCC.

Inaudhi na inachukiza sana kama watu bado wanafanya upendeleo kwa misingi hii ya kiukabila na kiaina nyingine yoyote.

Kufanya kazi kwa bidii, au kusifika kwa umahiri wa kiongozi hautoshi kama kiongozi huyo anayo roho ya kibaguzi. Watu aina hiyo hawafai kuongoza.
 
Mpaka hapo hujajibu hoja za msingi za Prof Lunyungu kuhusu ukabila. Yeye haja-protest kwamba Beda kafanya yote hayo, wala hajabisha kwamba Beda ni mwalimu wako wa production engineering; anachosema ni kwamba pale UCC kumejaa inshomile mno kuliko kawaida na hapo ndio hoja ya ukabila ilipoingia. Yote uliyoeleza hayapangua hoja za msingi za Prof Lunyungu.Sasa tupe data, hii issue ya ukabila kwa mujibu wa statitics za mtoa hoja hii ni kweli au siyo? Ingekuwa ni essay hapo, pamoja na maelezo marefu, tungekuandikia ooops!

Idadi ya "nshomile" inayoruhusiwa au inayostahili kuwapo kwenye idara hiyo ni watu wangapi? Kwa kigezo kipi?
 
Hapo awali ulianza ukabila kwa mawazo na matendo,ukapungua nguvu kivitendo na sasa kuna viashiria vinaonyesha unarudi kwa kasi kimawazo na bila shaka kimatendo.Watu wanaujadili si hapa JF pekee,bali hata huku mitaani tuishiko.Si ajabu kumsikia mtu akisema yule mkurugenzi,mkuu wa kitengo au bosi katika ofisi fulani ni ndugu yangu na ameaniahidi kazi.Ukiuliza undugu ukoje,anakwambia natoka nae eneo moja!

Ulikifikirika Udini,ukristo na uislam,sina uzoefu wa athari zake kwenye sehemu za kazi.Lakini nafikiri sehemu nyingi za hapa kwetu hazijaathirika saana.Mungu aendelee kuepusha balaa hili.Watu kwa sasa wanaongelea Udini,inawezekana kasi ya kuongelea swala hili inaongezeka kuliko kinavyofikiriwa.

Haya mawili hapo juu si mapya yamekuwepo na baadhi wamekuwa na wengine wanaendelela kuwa wahanga wa dhana hizo mbili.

Siku za hivi karibuni umeibuka ukabila wa aina yake ambao nauweka kwenye makundi mawili

Nilisoma nae(ushule)
Ni mwana mtandao(ushirika wa upekee wenye kutimiza lengo furani)

Hayo mawili kwa mtazamo wangu naona yanakuwa mabaya zaidi kwa sababu watu kwenye makundi haya hupeana vyeo,nafasi za kazi,tenda na mambo mengine muhimu kwa sababu tu walisoma wote,walisoma na baba/mama/ndgu zao.Au hupeana majukumu mkubwa kwa sababu tu wanaushirika/mtandao furani tena wenye makubaliano kwamba wewe ukipata nafasi furani lazima uyalinde masirahi yetu.

Tumeona watu wanashindwa kuwajibishana sababu tu ni marafiki au washirika.Tumeona kinachotokea BOT watoto wa wawakubwa walioajiliwa wale wote si kabila moja lakini watu wa aina moja ambayo haigusiki.Nadhani hata walioko madarakni leo watashindwa kupangua ile safu siku moja ikifanya kosa.Wangekuwa wachaga.wahaya,wasukuma,wanyanyukyusa pekee ingekuwa rahisi kwa mtendaji kushughulikia na hasa kama huyo mtendaji asingekuwa wa kabila husika.

Nafikiri ni wakati sasa tukawa na fikira mbadala na endeleevu,turejee misingi ya utendaji bora.Tuajiri watu kwenye sehemu zetu kwa kuzingatia elimu na utendaji kazi sawia.kama kuna utata wa uwakirishi,basi tuweke idadi sawa kwamba tuajiri kutoka kila la eneo,wingi wa kabila furani uwepo tu tukikosa kabila lingine.Si busara kuacha kuajiri kabila furani kwa sababu ya wingi wa watu waliopo katika sehemu husika na kuajiri watu kutoka kenya au nchi nyingine ya nje sabbu ya ukabila.

Natanguliza samahani kama nimechanganya hoja

Nawasilisha
 
Lunyungu,
..yaani badala ya kufanya kazi mnataka Prof.Muta ahangaike na tribal balancing ktk kitengo chake?

..mimi nadhani tuangalie ufanisi, na matokeo ya kazi, siyo mambo ya kabila gani wanafanya kazi hiyo.

..mbona Marekani asilimia 33 ya wahandisi wa NASA ni Wahindi? Wamarekani wanajisifia kwa hilo, hawalalamiki.

..Wahaya wamesoma ndiyo maana inawezekana kuwajaza ktk vitengo mbalimbali. Sasa tuelekeze bongo na nishati zetu ktk kuhakikisha makabila mengine nayo yanakwenda shule kama Wahaya.
 
If there is something for a discussion let it be discussed and that is the real meaning of Freedom of Speech. Lakini pia msijifanye kuvaa miwani ya Chumba na kuweka zege masikio huku laana na dhambi ya kubaguana kwa namna moja ama nyingine inamea baadaye mtashindwa kujenga hoja hapa. Jambo la msingi ni kwamba kuna hoja mezani chunguza na ujue kwa nini watu wanalalamikia UCC then tuendelee kujadili ni kwa ajili ya Tanzania na si Wazungu . Kumbuka US cannot be compared na Tanzania .
 
Nami nakubali kwamba tanzania kuna ukabila sana,umeshamiri sana.Binafsi niliwahi kuwa victim ya hiyo kitu,kwamba unanyimwa nafasi ya kazi kisa ni kabila lako,au kutokuwa kibaraka kwenye mtandao fulani.Its a big problem that should be seriously adressed.
 
Lunyungu,
ilibainika hapa jamboForums kwamba kuna madaktari wengi bingwa wa Kichaga kuliko makabila mengine. Kwa mtizamo wako Watanzania tulipaswa tulaani suala hilo.

Pia kuna nakala ya utafiti ilitoka ktk gazeti la majira. Nakala hiyo inaelezea kuhusu wananchi wa Kisarawe Pwani wasivyopenda elimu kiasi cha kuelekeza mambo ya ushirikina dhidi ya Waalimu.

Makala hiyo ilieleza tukio ambalo wananchi wanaamini kuna Mwalimu wa Kichaga ambaye "alirogwa" kutokana na juhudi zake za kufuatilia wazazi wa watoto watoro shuleni.

Sasa katika mazingira kama hayo wanakuja wananchi wa Pwani na kulalamika kwamba Wachaga,Wahaya,...wanawanyima elimu na nafasi za kazi.

Sasa hayo malalamiko yako yanaweza kuwa ya kweli lakini ktk mazingira ya mwamko wa elimu Tanzania hayapaswi kuwa kipaumbele cha mjadala wetu.

NB:
Kuna matukio ambapo an applicant with the best qualifications ameachwa kutokana na kuhofia malalamiko ya ukabila. Sasa ktk zama hizi za Sayansi na Teknolojia wenzetu they just go for the best in the market. Sisi watanzania tunahangaika na tribal balancing.
 
If there is something for a discussion let it be discussed and that is the real meaning of Freedom of Speech. Lakini pia msijifanye kuvaa miwani ya Chumba na kuweka zege masikio huku laana na dhambi ya kubaguana kwa namna moja ama nyingine inamea baadaye mtashindwa kujenga hoja hapa. Jambo la msingi ni kwamba kuna hoja mezani chunguza na ujue kwa nini watu wanalalamikia UCC then tuendelee kujadili ni kwa ajili ya Tanzania na si Wazungu . Kumbuka US cannot be compared na Tanzania .

Mzee uliyoandika hapa ni mambo nilishayasikia kuwa yapo pale kwa huyu bwana nafikiri ni just matter of time tutapata majibu yake. Lakini may be hayana tofauti na mambo yaliyopo Tanzania nzima.

Labda cha kuuliza hivi UCC haiko chini ya UDSM?
 
Bado sijajibiwa. Nimeuliza katika nchi yetu tuna idadi maalumu ya watu wa kabila fulani inayopaswa kuwa karika idara fulani? Hicho ndicho kingekuwa kigezo cha kutamka maneno kama "wahaya wamezidi" n.k Lakini kwa ufahamu wangu, idadi hiyo haipo. Kwa hiyo huwezi tu kudai kwamba mahali fulani kuna ukabila ati tu kwa kuwa watu wa kabila fulani ni wengi mahali pale, pengine ndiyo wanaopenda hiyo kazi au wenye sifa hiyo n.k. Kule Moshi kuna shamba la miwa linaitwa TPC, na idadi kubwa ya wakata miwa, nadhani zaidi ya nusu ni wasafwa. Mbona sijasikia malalamiko ya ukabila? Majeshi yetu (polisi na JWTZ) kwa miaka mingi yamekuwa na idadi kubwa ya wakurya hadi ikafikia hatua lafudhi ya kikurya ndiyo inayotumika kumzungumzia askari katika hali ya utani, kama "haroo, unafanya mucheso na cheshi ra porish!" Kuna wakati tulifanya hata masikhara kwamba askari wote wanaitwa "afande chacha" Sijasikia malalamiko ya ukabila huko. Hivi mtu akianzisha kampuni ya ulinzi pale Dar, na ukakuta walinzi 90% ni wamasai huo pia utakuwa ukabila? Sasa ukabila ni nini?

Kwa ufahamu wangu, tunaweza kuzungumzia ukabila iwapo kabila la mtu linatumiwa kama ndio sifa ya kwanza, na kama exclusion criteria katika kumpa mtu manufaa fulani ambayo watu wote wengine wa makabila mengine wana haki sawa ya kuyapata. Nimesema "exclusion" na si "inclusion" criteria, kwa uangalifu. Inapokuwa exclusion criteria, maana yake mtu nje ya kabila hilo hatapata nafasi hiyo. Sasa kuna mwenye ushahidi kwamba kwenye kitengo kinachozungumziwa hapa uhaya ndiyo sifa ya kupata kazi mahali hapo? Kwamba unapoandika cv lazima utaje kwamba wewe ni mhaya, vinginevyo hutapata kazi? Au kwamba kuna mhaya asiye na sifa za kitaaluma na msumbwa mwenye sifa zote zinazotakiwa kitaaluma, walipofika kwenye interview yule mhaya akapewa tu kwa kuwa ni mhaya? Walioleta mada hii, wana hoja gani kuthibitisha madai haya?
 
Bado sijajibiwa. Nimeuliza katika nchi yetu tuna idadi maalumu ya watu wa kabila fulani inayopaswa kuwa karika idara fulani? Hicho ndicho kingekuwa kigezo cha kutamka maneno kama "wahaya wamezidi" n.k Lakini kwa ufahamu wangu, idadi hiyo haipo. Kwa hiyo huwezi tu kudai kwamba mahali fulani kuna ukabila ati tu kwa kuwa watu wa kabila fulani ni wengi mahali pale, pengine ndiyo wanaopenda hiyo kazi au wenye sifa hiyo n.k. Kule Moshi kuna shamba la miwa linaitwa TPC, na idadi kubwa ya wakata miwa, nadhani zaidi ya nusu ni wasafwa. Mbona sijasikia malalamiko ya ukabila? Majeshi yetu (polisi na JWTZ) kwa miaka mingi yamekuwa na idadi kubwa ya wakurya hadi ikafikia hatua lafudhi ya kikurya ndiyo inayotumika kumzungumzia askari katika hali ya utani, kama "haroo, unafanya mucheso na cheshi ra porish!" Kuna wakati tulifanya hata masikhara kwamba askari wote wanaitwa "afande chacha" Sijasikia malalamiko ya ukabila huko. Hivi mtu akianzisha kampuni ya ulinzi pale Dar, na ukakuta walinzi 90% ni wamasai huo pia utakuwa ukabila? Sasa ukabila ni nini?

Kwa ufahamu wangu, tunaweza kuzungumzia ukabila iwapo kabila la mtu linatumiwa kama ndio sifa ya kwanza, na kama exclusion criteria katika kumpa mtu manufaa fulani ambayo watu wote wengine wa makabila mengine wana haki sawa ya kuyapata. Nimesema "exclusion" na si "inclusion" criteria, kwa uangalifu. Inapokuwa exclusion criteria, maana yake mtu nje ya kabila hilo hatapata nafasi hiyo. Sasa kuna mwenye ushahidi kwamba kwenye kitengo kinachozungumziwa hapa uhaya ndiyo sifa ya kupata kazi mahali hapo? Kwamba unapoandika cv lazima utaje kwamba wewe ni mhaya, vinginevyo hutapata kazi? Au kwamba kuna mhaya asiye na sifa za kitaaluma na msumbwa mwenye sifa zote zinazotakiwa kitaaluma, walipofika kwenye interview yule mhaya akapewa tu kwa kuwa ni mhaya? Walioleta mada hii, wana hoja gani kuthibitisha madai haya?

Mkuu chukua tano hapo, umemaliza kila kitu
 
Hakuna Ubishi kwamba UCC ni kwa Wahaya!!! hilo liko wazi, ulizia watu waliopitia idara ya Hisabati, na Idara ya Kompyuta...pale mlimani
 
Kuna jamaa mmoja( Siyo Mhaya) aliomba kazi pale ya kufundisha, akafanya interview pamoja na wengine. Akapigiwa simu kuwa kafaulu interview.
Ninapoandika hapa alishindwa kuanza kazi kwani ilikuwa kila akienda, anaambiwa (not Friendly) fulani hayupo subiri arudi; rudi baada ya siku kadhaa.

Hali iliendelea kuwa hivyo hadi jamaa akakata tamaa, akaona hatakiwi licha ya kufaulu interview.
Was it because hakuwa mhaya? I dont know au labda maafsa wa chini walikuwa na mtu wao, I cant tell!
 
wee Musbobo hii mada ulipenda iwe kwenye thread ipi kama si hapa ? Hizi ndiyo siasa zeneywe ati !!!!!
 
Ninavyofahamu mimi kwenye sheria ya TAKUKURU ya sasa, hii ni aina ya Rushwa kwa maana(corruption) na sio Bribe[Rushwa iliyozoeleka zamani],,, kwa hiyo Hosea and Team wanatakiwa wapewe taarifa na waende pale wakaangalie kuna nani... yaani qualified ni Wahaya tu!!!

Wenye jamaa zenu wanafanya PCCB, kamatisha mbwa... wakanuse!!! ile ni taasisi ya umma bwana....
 
Madhali hizi taarifa zimefika hapa na nafikiri watu wa UCC, nao wanazo hizi habari basi tunawaomba watoe taarifa ya kujitakasa au kujisafisha na hii allegation, ili watu wawe fair kwao, hata kama sio wanachama wa jambo forum wanaweza kujitakasa kipitia vyombo vya habari kama magazeti na web sites kama ya "Michu" etc.
 
Kwi kwi kwi kwi kwi kwi Duhhh, Kaaaazi kweli kweli!!! Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito kumbe alikosea kusema Tanzania haina dini na hata Ukabila haupo Tanzania!!!!
 
mchangiaji wa mwisho nakusifu sababu umetoa maneno mazuri sana kuhusu ukabila unaosemwa ucc, kama ukabila upo ucc si kiwango cha kusema wakijitokeza wahaya kwenye interview basi wengine wanatupwa kushoto na wahaya ndo wanachukuliwa ila tukubali ukweli kuwa ukija kwenye issue ya masomo ya engineering wahaya ni wengi na ndio hao hao wanahitajika na ucc, kingine wahaya wameenda shule jamani na wanajua vitu vingi sasa watu wengine mnabaki kufanya majungu yatawapeleka wapi na wakati shuleni uliogopa umande wenzako wakaendelea kukandamiza na shule? acheni negative issues tu angalieni na mafanikio.
 
mie nitoe ushauri tu kwa prof beda kuwa yeye huruma yake imezidi sana tu baba wa watu kwani kuna baadhi ya ndg zake wapo pale hawana elimu ya kutosho ila wapo na ndo wanjifanya kiburi kisa ni ndugu wa prof beda. nadhani mzee beda kabla ajampa mtu kazi ambae ni ndugu yake ampatie masharti ya kazi kuwa asifanye kiburi na kuwa mvivu kisa ni ndg yake, nyie mnasema ukabila umezidi ucc mbona hamsemi wizara ya fedha unyakusya na uiringa umezidi?watu wanaajiliwa kwa vimemo kila siku?mnawaona wahaya tu.
 
kilitime ujatulia hiyo sio oja hakuna pccb hapo wala nini acha mizengwe, wambie pccb waende mhasibu mkuu wa serikali na wizara ya fedha kwa ujumla kumeoza wanyakyusa na iringa tupu vimemo we umeona ucc
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom