BBC: Tanzania imezuia uzinduzi wa ripoti ya Human Rights Watch

Hawa human right watch nao wehu tatizo limetokea Oman halafu ripoti mnazindulia Tanzania kwa kiswahili hao waoman wataelewa kweli
Waathirika wa tukio ni watanzania na wapo Tanzania. Huko Oman watamzindulia nani mwenye uchungu na muathirika (ngozi nyeusi)?
 
Labda mimi niulize wadau. Wanaonyanyaswa ni wafanyakazi wa kitanzania pekee au wote wenye asili ya Africa? Kama na nchi zingine wananyanyaswa kwa nini repoti ijielekeze kwa Tanzania pekee? Naona kuna ukakasi katika kuzuia ripoti sawa na ukakasi ulioko kwenye ripoti.
Uelewa wa namna hii unashangaza sana,una uhakika nchi zingine hawajafika?umeona kwenye ripoti ya awali wanazungumzia waafrica wa Kenya?
 
Labda kama hufwatilii mambo. Nchi nyingine Nyingi tu zimeishatoa ripoti hizi kwa jinsi nchi za kiarabu zinavyo nyanyasa wafanyakazi wa kiafrika.
Mfano; wa hizi ripoti ni ile iliyotolewa Nigeria
Aksante mkuu. Sikujua hili kiongozi.
 
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote. Nchi yangu Tanzania jina lako ni tamu sana. Tanzania umekosa nini hapa? Ripoti hii ni ya wapi kwa nini izinduliwe hapa? Watu wameteswa Arabuni aliyewatesa hasemwi wala hahojiwi. Ripoti inahoji Costech badala ya Arabuni. Wazungu na wasaliti wako wanakuandama Tanzania wewe mhanga uliyeteswa badala ya mtesi kuandamwa. Kwa nini hii ripoti isizinduliwe Arabuni? Niamkapo nakuota wewe niamkapo ni heri mama weee. Tanzania Tanzania ninapokwenda safarini.
 
Ni aibu sana....sasa hapo wanakataza ili kumlinda nani labda...hao mabalozi wetu huko ghuba au?
 
Kwa mwenendo wa awamu hii ya tano sitarajii wao kukubali watu huru kutolea maelezo yoyote juu ya mwenendo wa haki za binadamu hapa nchini na wananchi wake kwa ujumla.
Hapa nchini? Nani kateswa hapa nchini? Kateswa na nani? Kwa nini isizinduliwe Oman?
 
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote. Nchi yangu Tanzania jina lako ni tamu sana. Tanzania umekosa nini hapa? Ripoti hii ni ya wapi kwa nini izinduliwe hapa? Watu wameteswa Arabuni aliyewatesa hasemwi wala hahojiwi. Ripoti inahoji Costech badala ya Arabuni. Wazungu na wasaliti wako wanakuandama Tanzania wewe mhanga uliyeteswa badala ya mtesi kuandamwa. Kwa nini hii ripoti isizinduliwe Arabuni? Niamkapo nakuota wewe niamkapo ni heri mama weee. Tanzania Tanzania ninapokwenda safarini.
Watanzania nyie watu wa ajabu sana...hii report inatetea watoto wenu na dada zenu wanaoonewa huko uarabuni still hamtaki kusikia....
Kwa nn serikali isitumie report hii kama base ya kutafuta ukweli kama amuwaamini hao walioiandaa?
 
Mkuu unategemea nini kutoka Serikali dhalimu isiyowajali wananchi wake?

Mamlaka nchini Tanzania imezuia uzinduzi wa ripoti kuhusu unyanyasaji wa wafanyikazi wanawake kutoka taifa hilo wanaofanya kazi katika mataifa ya Uarabuni.

Shirika la Human Wrights Watch limedai katika matokeo yake kwamba wafanyikazi wa nyumbani kutoka nchini Tanzania walikuwa wakibakwa , kuteswa na kulipwa mishahara duni na waajiri wao katika mataifa ya Uarabuni.

Ripoti yenye kurasa 100 inayodai kuteswa kwa wafanyikazi wa nyumbani wa Tanzania nchini Oman na muungano wa mataifa ya Emirata UAE ilitarajiwa kutolewa leo kwa waandishi wa habari mbele ya waathiriwa lakini hilo halikufanyika.

Katika hatua isiokuwa ya kawaida ,afisa mmoja kutoka shirika linalofadhiliwa na serikali la Sayansi na Teknolojia COSTEC William Kindekete alifutilia mbali mkutano huo katika mji mkuu wa Dar es Salaam akisema kuwa wanaharakati wa shirika hilo la haki za kibinaadamu hawakufuata sheria katika kufanya utafiti wao.

Hatahivyo matokeo ya utafiti huo wa HRW unaonyesha kuwa takriban wanawake 50 walihojiwa wakati wa utafiti huo ambao wanadai kwamba walilazimishwa kufanya kazi kwa kati ya saa 15 na 21 kwa siku huku wakipokonywa pasipoti zao na waajiri wao punde tu walipowasili katika mataifa hayo.

Ripoti hiyo ilibaini zaidi kwamba zaidi ya nusu yao hawakulipwa huku wengine wakisema kuwa hawakulipwa kabisa.

Wawili kati ya watano walidai kupigwa mbali na kunyanyaswa kijinsia.

Ripoti hiyo ya HRW pia inasema kwamba balozi za Tanzania katika eneo la Ghuba hazikutoa usaidizi wowote kwa waathiriwa wakati walipotaka usaidizi

Juhudi za kupata majibu kutoka kwa serikali ya Tanzania hazikufanikiwa kwa kuwa maafisa wengi hawakuwa tayari kuzungumzia swala hilo
 
Report ikizunduliwa huwekwa kwenye Lugha zote isitoshe kampuni zinazowapeleka wafanyakazi Oman zipo Tanzania na baada ya Uzinduzi ingesaidia Ubalozi wa Tanzania Nchini Oman kuzinduka na kuanza kuwasaidia watanzania wanaotaabika huko majumbani mwa waarabu.
Tanzania ina kosa gani hapa? Kama Oman wananyanyasa Burkina Fasona Somalia na Wakenya na Nigeria kwa nini wasizindue Umoja wa Mataifa au AU au Oman kwenyewe? Hii ripoti watazindua kila nchi waliyoteswa? Kama Costec hawataki kwa nini wasiende kyzindulia COSTEGH Accra au COSSWEC Sweden, si wote wabateswa? Maadui wa Tanzania hawachagui tusi, tukana tu.
 
Tanzania ina kosa gani hapa? Kama Oman wananyanyasa Burkina Fasona Somalia na Wakenya na Nigeria kwa nini wasizindue Umoja wa Mataifa au AU au Oman kwenyewe? Hii ripoti watazindua kila nchi waliyoteswa? Kama Costec hawataki kwa nini wasiende kyzindulia COSTEGH Accra au COSSWEC Sweden, si wote wabateswa? Maadui wa Tanzania hawachagui tusi, tukana tu.
Kumbe tatizo lako ni mahali pa uzinduzi!haaaa haaaa ila nini response ya Tz na balozi zake
 
Waathirika wa tukio ni watanzania na wapo Tanzania. Huko Oman watamzindulia nani mwenye uchungu na muathirika (ngozi nyeusi)?
Muathirika kama yuko Tanzania ameathirikaje? Kaathirika mtu, si nchi, kwa nini Tanzania ilaumiwe? Lengo la Ripoti ni kuzuia lisitokee tena, kwa nini ripoti iditolewe Oman kwa lugha zote halafu ikatolewa UN? Kuna wanaoteswa na kuuliwa Ulaya na Marekani hawa ripoti yao itatolewa na nani lini? HRW ni taasisi ya Amerika, kwa nini isizindue ripoti yake huko?
 
Watanzania nyie watu wa ajabu sana...hii report inatetea watoto wenu na dada zenu wanaoonewa huko uarabuni still hamtaki kusikia....
Kwa nn serikali isitumie report hii kama base ya kutafuta ukweli kama amuwaamini hao walioiandaa?
Kutumia ripoti sawa, tumeiona. Kwa nini izinduliwe hapa? Kwani wameteswa hapa? Kama kuna uonevu hii ni kazi ya polisi. Hivi serkali ina madaraka gani na watu binafsi? Juzi ilipiga marufuku kuvusha mahindi tu kuuza Kenya, kesho wakisema marufuku msafiri kuvuka mpaka kwenda Kenya si itakuwa rais dikteta uchwara?
 
Back
Top Bottom