BBC, habari za moto Mlima Kilimanjaro anaripoti mwandishi kutoka Kenya, ni sahihi?

hayaland

JF-Expert Member
May 4, 2012
712
399
Nilikuwa nafuatilia habari za BBC London katika television. Cha kushangaza habari ya mlima Kilimanjaro na harakati za nchi kuzima moto katika mlima huo mkubwa barani Afrika ameripoti mwandishi Emmanuel Igunza kutoka nchini Kenya. Nimejiuliza sana kwa nini habari za Tanzania aripoti mwandishi kutoka nchi jirani?

Haya matukio ya mwandishi kuripoti habari za nchi nyingine tumezoea kuziona katika nchi ambazo zina vita. BBC wakiripoti habari za Somalia mwandishi wa habari lazima atoke nchini Kenya.

Nimejiuliza kwa nini mwandishi wa BBC aliye Tanzania hakuripoti habari hii na kuripotiwa na mwandishi kutoka Kenya?

Inaumiza sana
 
Ngoja tuunde tume ya uchunguzi, tujue chanzo kwanza halaf tuuzime kwa nguvu zote CCM hatupangiwi
 
Watu kweli mna issues za ajabu. Yaani tatizo lako ni aliye toa ripoti na uraia wake wala sio habari zenyewe? Anyways Emmanuel Igunza licha ya kuwa raia wa Kenya ni mwandishi wa BBC. Pili, mlima Kilimanjaro upo TZ ila view ya mlima huo ukiwa upande wa Kenya haswa Amboseli ni breathtaking.

Eti inaumiza sana, kwa hivyo alipaswa kunyamaza hata kama ameliona tukio?
 
Huyo Emmanuel Igunza kama mwandishi au reporter wa BBC unafikiri anatakiwa kuripoti habari za Kenya tu?
Salim Kikeke huwa anaripoti za wapi?

Kuna mioyo inachoka sana sababu ya kubeba chuki na ubaguzi
 
Swali fikirishi hili. Sema mbona na sisi tuna waandishi wetu huko kenya na uganda wanaturipotia habari za Afrika Mashariki kila wanapozipata na kuzituma kwenye Tv zetu?
 
Wamefikia wapi juhudi za kuuzima?
Aisee mpaka tunapoongea hivi sasa moto unawaka sana sana, na pia unazidi kuongezeka distance wakati wa usiku kwasababu ya upepo, Mimi nimekaribia hata ukikaa mita kadhaa joto ni kali mno.

Halafu pale ni Kilimanjaro National Park (KINAPA) sio mlimani hasa

Na wakati huohuo kwenye mlima wa usangi pia kuna moto unaonekana kwa mbali na pia ni mkubwa kweli.

Sijui ni nini hiki
 
Back
Top Bottom