BBC: Dr. Ulimboka yuko ICU (yuko kwenye koma) anasaidiwa na mashine

kwa uweza wa jina kuu lipitalo majina yote nakemea roho ya mauti, ishindwe kwa jina la yesu! tuna imani yesu u mkuu bwana, nakuomba sasa tenda muujiza wako kwa ndugu yetu huyu, anakwenda kuamka sasa, mapafu na figo zinawekwa mpya! oooh jesus, your doing it! isee, jesus! jesus! jesus! yes yes! dot it for us our lord! nguvu za giza za watawala wa dunia zinakwenda kushindwa sasa, ooh! karaboooo sarabaine &*(&(((*&&*( jesus! asante yesu kwa kunisikia!!!!!!
 
Kova Acha Unafiki. Kila mtu anajua serikali ya Ccm kupitia polisi ndio mmemfanyia huo unyama.
 
bahari nzuri nimerekodi hiyo taarifa ya bbc na ninayo hapa...

Ali mtasa mtangazaji wa bbc alikwenda hosp.moja huko africa ya kusini alokolazwa dr ulimboka.alipofika alienda maulizo na kuonyeshwa chumba alicholazwa. wakati akielekea huko alikutana n ndugu wa ulimbo walioko hapo hosp na yeye alimuona ulimboka kupitia kwenye vioo na wala hakuingia chumbani kabisa.

alipojitmbulisha kwa ndugu wa ulimboka, mara moja walimuambia aondoke hosp hapo maana hawahitaji mtu na wala asifatilie lolote kuhusu maendeleo ya ulimboka.alipoulizia hali yake inakwendaje hakujibiwa kitu isipokuwa aliambiwa aondoke mara moja. na akaondoka....

hiyo ya kusema kuwa dr uli yuko kwenye koma ameipika mwenyewe maana dr uli alikuwa amepumzika na wala hakunandugu hata mmoja aliyemwambia kuwa yuko kwenye koma..

Bila shaka unasumulia na yawezekana ulikuwa usingizini kama umerekodi anza mwanzo mwisho then urudi ufute usemi wako
 
SASA HUO UCHUNGUZI AU TUME ILIYOUNDWA NA POLISI UHALALI WAKE HUKO WAPI MAANA WAO NI WATUHUMIWA. KATIKA NCHI YETU HAPAJAWAHI TOKEA POLISI WAKACHUNGUZI SWALA LOLOTE LINALOWAGUSA NA MATOKEO YAKAWA FAIR. BASI TUMWOMBE MUNGU NDG YETU APATE KUPONA MAANAKE IKITOKEA IKAWA VINGINEVYO KUNASITOFAHAMU KWA WAPENZI, NDUGU , MARAFIKI NA WAPENA HAKI. MATAMUSHI YA WATAWALA YANAONYESHA ''Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyohakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo,lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemeavizuri zaidi kuliko wao wenyewewalioajiriwa na Serikali.'

Polisi/tume iliyoundwa unataka ichunguze nini wakati Rais ameshatoa tamko la serikali eti kutohusika?
 
Mbona hali ya huyu bwana haistabilize?? huenda watesaji wake walimuumiza sana! watu wote wapenda haki na wenye mapenzi mema tumuombee apone haraka! mungu amuwekee mkono wake wa uponyaji aweze kupona na kuungana na familia na watanzania kwa jumla!!

kama ulisha wahi ngoa jino kwa ganzi still utakua na maumivu utakayo yapata, Sembuse mwenzetu alie umizwa kikatili kwa kungolewa kucha na jino!!! Hapa ni Mwenyenzi Mungu tu asimame.

Tunazidi kukuombea ndugu yetu mpendwa Dr Ulimboka.
 
BBC.... Tuwe makini nao sio wasemaje wa familia ya Dr Ulimboka, jeshi la polisi wala serikali...

Taarifa ambazo hazijachujwa kutoka chanzo kimoja zinaweza kutugombanisha ndani na nje ya JF...

Tutafute ukweli zaidi kutoka vyanzo vingine ili kujiridhisha.
 
Dr ulimboka amewekewa mashine ya kupumulia na yuko mahututi (koma), mwandishi alimtembelea SA.
Source: BBC idhaa ya kiswahili

Luckily, the Ulimboka we LOVE is NOT in South Africa. However, I feel sorry for your Ulimboka!



Wednesday, 04 July 2012 21:54



TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI, RAFIKI YAKE ATOA USHUHUDA MPYA WA JINSI ALIVYOTEKWA

Waandishi wetu

WAKATI ikielezwa kwamba Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka anatibiwa Afrika Kusini, kuna taarifa kwamba amelazwa katika hospitali moja ya huko Ujerumani.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa Dk Ulimboka alipelekwa Afrika Kusini lakini alikaa kwa muda mfupi tu kabla ya kupelekwa Ujerumani anakoendelea na matibabu yake sasa.

Awali, jopo la madaktari waliokuwa wanamtibu Dk Ulimboka hapa nchini lilieleza kuwa baada ya hali yake kuendelea kuwa mbaya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, waliamua kumpeleka Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

“Ni kweli alikwenda kwanza Afrika Kusini, lakini hapo alipita tu. Ndege ilitua na akaunganisha ndege nyingine kwenda Ujerumani,” kilisema chanzo kimoja cha habari.
Hata hivyo wakati chanzo hicho kikieleza hivyo, mmoja wa wanafamilia yake, alisema: “Sisi katika level (ngazi) ya familia tunajua yuko Afrika Kusini lakini hii haiwazuii madaktari kumhamishia kwenye hospitali nyingine wanayoona inafaa.”

Mwanafamilia huyo ambaye hakutaka kutajwa gazetini, alisema suala la Dk Ulimboka kuhamishiwa Ujerumani si la ajabu kwani anachotafuta ni matibabu ya uhakika.

Alipoulizwa kuhusu habari hizo, Kiongozi wa Jopo la Madaktari waliokuwa wakimtibu, Profesa Joseph Kahamba alisema: Mimi ndiyo kwanza nasikia, lakini kwa nature (aina) ya tukio lake, si vyema ikaanikwa amepelekwa wapi. Pia si vizuri ikaelezwa yuko wapi ingawa tayari watu wanajua yuko Afrika Kusini.”

“Kama kiongozi wa jopo la madaktari wanaomtibu Dk Ulimboka ninajua kwamba yuko Afrika Kusini ingawa hata hiyo taarifa tusingependa watu waijue kwa jinsi tukio lilivyokuwa.”

Mmoja wa madaktari ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alipoulizwa juu ya suala hilo alipinga na kusema; “Habari za aina hiyo mtakuwa mnazipata nyingi, najua mtaandika, ndiyo maana mnaandika madaktari Muhimbili wanafanya kazi wakati si kweli”.

Alisisitiza kuwa Dk Ulimboka yupo Afrika Kusini anakopatiwa matibabu na kusisitiza kuwa habari alizokuwa nazo tangu juzi jioni ni kwamba anaendelea vizuri.

Katibu wa Chama cha Taifa cha Madaktari (MAT), Dk Rodrick Kabangila alipoulizwa juu ya hali ya Dk Ulimboka alisema kwa mujibu wa taarifa za juzi jioni alikuwa anaendelea vizuri.

Alipoulizwa juu ya taarifa za kupelekwa Ujerumani aliguna kisha akasema: “Naomba ieleweke kuwa yupo Afrika ya Kusini kwa matibabu.

Rafiki asimulia mkasa

Rafiki wa karibu wa Dk Ulimboka aliyekuwa naye wakati mkasa wa kutekwa ukitokea, Dk. Deogratius Michael ameelezea tukio zima lilivyotokea na kusema ulikuwa wa kitaalamu na ulifanywa na watu wenye ujuzi na mambo hayo.

Dk Deogratius alisema jana kwamba siku ya tukio walikuwa wametokea kwenye msiba wa ndugu wa mwalimu wao Profesa Yongolo na baada ya msiba walikwenda Viwanja vya Leaders saa moja usiku kuangalia taarifa ya habari na mambo mengine.

Huko walikutana na madaktari wengine na ilipofika saa 4:00 usiku, Dk Ulimboka aliwaambia kwamba kuna jamaa alikuwa akimtafuta hivyo angependa kwenda kukutana naye.
“Tukamwuliza anamtafutia nini? Akatueleza kuwa kwa siku tatu huyo jamaa anamtafuta. Wenzangu wakasema asiende mwenyewe na mimi ndiyo nikamsindikiza. Mara ya kwanza huyo jamaa alisema anaitwa Abeid na alisema yuko Sterio, tukaenda huko hatukumkuta tukaenda Hugo hatukumkuta lakini baadaye tukakutana naye maeneo ya Barabara ya Tunis karibu na Ofisi za Ultimate Security.”

Dk Deogratius alisema wakati wakiendelea na mazungumzo, Abeid alikuwa akitaka kujua nini kinachotakiwa ili kutatua mgogoro uliopo wa madaktari.

“Wakati tunamalizia mazungumzo nilikwenda msalani, niliporudi Abeid alikuwa akizungumza na simu kila wakati, tuliendelea na mazungumzo hadi tukamaliza na kuanza kuagana,” alisema.

Alisema wakati wakiagana bado walikuwa wamekaa katika viti pamoja na Abeid... “Ghafla kuna watu walifika na kusema kuwa wanamtaka Dk Ulimboka. Walimchukua na kwenda naye katika gari. Walikuwa watano, walikuwa ‘giant’ (miili mikubwa) na ‘very skilled’ ( wenye uzoefu) wakamchukua Dk Ulimboka wakaenda naye kwenye gari,” alisema Dk Deogratius.

Alisema wakati huo Abeid alikuwa anakimbia hivyo akamkimbilia ili ampe namba yake ya simu ambayo ingemsaidia kwa mawasiliano.

“Alinipa namba yake nikampigia muda huohuo lakini nilipokuja kumpigia tena sikumpata na mpaka leo hapatikani,” alisema.

Alisema baada ya tukio hilo alimpigia mke wa Dk Ulimboka na kumweleza na pia alipiga simu polisi kuwaeleza.

“Nilikwenda polisi kutoa maelezo na nikawapa namba zangu za simu zote ili wanipigie kama watapata chochote, lakini mtu wa kwanza kunipigia asubuhi (kesho yake) alikuwa Juma Mgaza (aliyemwokota Dk Ulimboka) ambaye alinieleza kuwa kuna rafiki yangu amempa hiyo namba na kwamba yuko hoi amepigwa.”

Alisema baada ya kupata simu hiyo aliwasiliana na watetezi wa haki za binadamu ambao walimtaka waende pamoja na kwamba walipokuwa njiani kuelekea Kituo cha Polisi Bunju alipigiwa simu na polisi wa kituo hicho.

Kutokana na hali hiyo aliomba iundwe tume huru ikijumuisha wanasheria, madaktari na watu wengine ili ukweli ujulikane.

Upelelezi wa Polisi
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema jopo la upelelezi aliloteua hivi karibuni kushughulikia tukio zima la kutekwa kwa Dk Ulimboka litaendelea na kazi yake hadi mwisho na hatasikiliza kelele za wanaodai kutokuwa na imani nalo.

Alisema madai yanayotolewa na watu mbalimbali akiwemo Dk Ulimboka mwenyewe kuwa hana imani na jopo hilo hazitabadili chochote kwani kinachofanyika hivi sasa ni kazi ya kawaida ya upelelezi ya jeshi hilo... “Hao wanaosema hawana imani na jopo hilo hawana hoja isipokuwa waliache jeshi la polisi lifanye kazi yake.

Kiongozi huyo wa mgomo wa madaktari alitekwa na kisha kujeruhiwa vibaya na baadaye kutelekezwa katika Msitu wa Pande.

Habari hii imeandikwa na Geofrey Nyang’oro, Boniface Meena na Joseph Zablon
 
Kumbe hali imekuwa mbaya namna hiyo. jamaa inawezekana bado wanamfuatilia hadi huko ili wammalize.
 
Thread hii imeletwa hapa kupima joto la mgomo wa madaktari.

kuna taarifa kwamba taasisi za nje zina mkono wao katika mgomo huo....BBC....BBC....BBC
 
"BBC Swahili~ Mwenyekiti wa chama cha
madaktari nchini Tanzania
Steve Ulimboka anaendelea
kupokea matibabu katika
hospitali moja mjini
Johanesburg Afrika Kusini alikolazwa katika chumba cha
wagonjwa mahututi.
1 hour ago"

Mwisho wa kunukuu

Source:BBC PAGE FB.

mbona tumeambiwa yukop ujerumani???
 
MUNGU MFARIJI WA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI, TUNA IMANI YA KWAMBA MAUTI HAINA MAMLAKA JUU YAKO MUNGU WETU,TUREHEMU NA HUYU MWENZETU APONE NA KURUDI NYUMBANI SALAMA SALIMINI MUNGU WETU!
Roho mauti tunaitupilia mbali ktk jina lake YESU KIRSTO BWANA aliyehai sasa na hata milele!
Tunaenda kinyume kbs na roho ya mauti kwani tuna Imani yupo MUNGU aliyewaepusha wale mafisadi kutomtoa roho huyu ndg yetu ktk ule msitu na leo hata huko alipo ataturudishia salama salimini.

Kwa kuwa MUNGU upo tuna Imani ya kwmb Dr Ulimboka utaturudishia salama kabisa.

Amen!
 
Ritz, fahamu kwamba ya jana si ya leo. Now yuko ICU, tumwombee.

Mungu atashindwa kujua tunachoomba kati ya maombi ya kuponya au maombi ya kutekwa


suala la kumuombea ni letu wote lakini tusiongeze chumvi kama njia ya kuchonganisha sio wakati wake huu.
 
Hii habari imenisikitisha sana asubuhi na jinsi alivyoripoti Mutasa kwa sababu kashuhudia kwa macho, Waandishi wa udaku Bongo wameeandika hali ya ulimboka imezidi kuimarika sijui source ya information zao wanapata wapi.
 
vyombo vya habari vyote vya Tanzania havina maana, njaa inavimaliza, vimekuwa vinaendesha tu propaganda kuhusu huu mgomo. Hii serikali naishangaa sana, pesa za kuhonga vyombo vyote vya habari wanazo lakini kutengeneza mazingira bora ya kufanyia kazi hawana. Huu ni ujuha wa dhaifu na serikali yake.

Mimi binafsi nimemsikia mtangazaji wa BBC aliyemtembelea Uli hospitali akisema ulimboka yuko kwenye 'coma, na anapumua kwa kusaidiwa na mashine, wao wanasema hali yake inaimarika. Kweli Propaganda mpaka kwenye uhai wa mtu?.

Angalia Jambo leo linavyoripoti kwe kejeli hali ya Afya ya ulimboka. Angalia jinsi Umma unavyopotoshwa kuhusu mgomo. Mgomo unaendelea ingawa kuna baadhi ya madaktari wa MOI walisaini mahudhurio na kuondoka, hakuna daktari anaefanya kazi, msiwadanganye watu wakatoka mikoani kwenda Muhi2.

La kushangaza hata wanataaluma kama Prof Museru na Mwafongo nao wameingia kwenye usaliti wa taaluma na kuendelea propaganda za serikali. Hivi kufikia kumnyima hata ambulance colleague kwa sababu ya cheo au pesa ni ujuha au ni nini. Mwafongo, Museru na wengine Muhimbili, kumbukeni serikali hii ya kifisadi na kigaidi haina rafiki wa kudumu, itakapowageuka mtakumbuka ubaya mnaowafanyia wanataaluma wenzenu.
pesa mdau,,,,,,pesaa acha tu
 
mbona tumeambiwa yukop ujerumani???

pia tuliambiwa alitekwa Leaders Club kumbe ni Club iliyo mkabara na ofisi za Ultermate security zilizopo mtaa wa Tunisia Kinondoni hatua takribani mia 200 kutoka Leaders club.


chanzo ni Dr Deo alipokuwa anahojiwa na Radio clouds jana. Dr Deo alikuwa na Dr Ulimboka siku ya tukio....
 
clip ya omari mtasa hiyo hapo..wewe mleta mada sikiliza halafu uniambie ni wapi (kama utasikia) ndugu wa dr ulimboka wakimwambia kuwa ulimboko yuko kweye koma....yale yalikuwa mawazo yake hakuna aliyemwambia
 

Attachments

  • taarifa ya omari mtasa.mp3
    3.5 MB · Views: 138
Bila shaka unasumulia na yawezekana ulikuwa usingizini kama umerekodi anza mwanzo mwisho then urudi ufute usemi wako

mkuu saa tisa nilikuwa niko macho nimeshaoga ..nimekuwekea clipi hapo juu isikilize tena ...hakuna ndugu aliyempa taarifa ya maendeleo ya mgonjwa .alitolewa mkuku
 
Back
Top Bottom