Zogwale
JF-Expert Member
- Jul 10, 2008
- 15,287
- 10,842
Ingekuwa na leseni TCRA wameshachukua na wazee wa kazi waneshaingia studio au ofisini kuchukua vifaa kama laptop, camera n.k na kuweka chini ya ulinzi kuanzia mmiliki, watendaji wote hasa Chief Editor. Hakika Mungu tunakushukuru mno. Hatutasahau March 2021.Sasa hivi kuna uhuru wa vyombo vya habari hadi raha.ITV wameirusha hii clip kwenye taarifa ya habari.Ingekuwa kipindi cha Mwenyekwenda zake ,walahi wasingethubutu kurusha!!
Mungu mlinde Kila hatua Rais wetu mpendwa SSH. Yaani aishi miaka mingi. Legacy ya kiongozi siyo Barabara bali ni alichofanya kwa mioyo ya wananchi bila kufutika. Uhuru kurejea na kumaliza udikteta ni Legacy haitasahaulika. Ninaamini mambo mazuri zaidi yanakuja ikiwemo kurejesha mahusiano na majirani na dunia.