BAVICHA yamtaka Makamu wa Rais kuomba radhi kwa kusema uongo kuhusu Maji ya Maiti na Samaki Kanda ya Ziwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
116,441
215,215
Mwenyekiti wa Bavicha , ambayo ni Taasisi bora kabisa ya vijana barani Africa , John Pambalu , akizungumza na vijana wenzake huko Geita kwenye vikao vya ndani , bila kumung'unya maneno wala kuona aibu , amemtaka Makamu wa Rais wa Tanzania Mh Philipo Mpango , kujitokeza hadharani na KUOMBA RADHI KUTOKANA NA KUTELEZA KWA ULIMI WAKE NA KUONGEA UONGO KUHUSU MAJI YA MAITI KUTUMIKA KUHIFADHIA SAMAKI wanaovuliwa Ziwa Victoria .

Pambalu amedai kwamba ni muhimu sana kwa Makamu wa Rais kuwapigia magoti wananchi , kwa vile kauli yake ile iliyopingwa na bunge la Tanzania imepunguza ama kuua kabisa soko la Sangara , Sato na dagaa wa Mwanza , huku njia pekee na fupi sana ya kurudisha Soko la samaki hao duniani ni kwa Makamu wa Rais kusimama hadharani na kukiri kwamba alikurupuka .
 
Aisee, Kazi ipo !

20220921_223611.jpg
 
Yaani BAVICHA wanaamini kauli ya makamu wa Rais ni Kama kauli ya Mbowe, kifupi Mashimba Ndaki katafutwa kajaa mkononi mwa wateuaji
tokea lini mteuaji aanze kumtafuta aliyemteua, sijui umekula maharage ya wapi. kwa mfumo wetu raisi aweza kukurupuka tu saa yoyote akasema amemtema waziri flani, aanzaje kumtafuta sasa
 
Nimeona hii taarifa mahali,ila nimeshindwa kuielewa, mwenye taarifa alichokisema VP atusaidie kuhusu hao Maji na samaki
 
Ni rahisi tu kujua , ukiona mdogo anakupinga na unanywea ujue ulikurupuka
Siasa za upinzani ngumu sana kwa Sababu zimekaa kiharakati mno Sasa kwa busara na hekima za VP Dr.Mpango unategemea kabisa atatumia muda wake kujibishana na waziri? Dkt.Mpango kwa nafasi yake sio busara kujibishana na waziri Kama watoto.

Lakini wenye akili tumeshajua anayetafutwa ni waziri wa uvuvi na tunaomjua Mpango sio mtu wa kukurupuka
 
Siasa za upinzani ngumu sana kwa Sababu zimekaa kiharakati mno Sasa kwa busara na hekima za VP Dr.Mpango unategemea kabisa atatumia muda wake kujibishana na waziri? Dkt.Mpango kwa nafasi yake sio busara kujibishana na waziri Kama watoto.

Lakini wenye akili tumeshajua anayetafutwa ni waziri wa uvuvi na tunaomjua Mpango sio mtu wa kukurupuka
Kama Mpango ni mkweli si athibitishe tu
 
Mwenyekiti wa Bavicha , ambayo ni Taasisi bora kabisa ya vijana barani Africa , John Pambalu , akizungumza na vijana wenzake huko Geita kwenye vikao vya ndani , bila kumung'unya maneno wala kuona aibu , amemtaka Makamu wa Rais wa Tanzania Mh Philipo Mpango , kujitokeza hadharani na KUOMBA RADHI KUTOKANA NA KUTELEZA KWA ULIMI WAKE NA KUONGEA UONGO KUHUSU MAJI YA MAITI KUTUMIKA KUHIFADHIA SAMAKI wanaovuliwa Ziwa Victoria .

Pambalu amedai kwamba ni muhimu sana kwa Makamu wa Rais kuwapigia magoti wananchi , kwa vile kauli yake ile iliyopingwa na bunge la Tanzania imepunguza ama kuua kabisa soko la Sangara , Sato na dagaa wa Mwanza , huku njia pekee na fupi sana ya kurudisha Soko la samaki hao duniani ni kwa Makamu wa Rais kusimama hadharani na kukiri kwamba alikurupuka .
Huyo pambalu hana akili
 
Kwahiyo Makamu wa Raisi Hana Mashushushu Waliomwambia Hayo???? Au Yeye ndio alienda Pima Hizo Samaki

Sidhani kama Makamu aliropoka maneno asiyoyajua..
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom