EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Wajumbe wa BAVICHA chini ya kamanda John Mnyika leo wako Kibaha Mjini katika warsha inayofanyika kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yahusuyo mustakabali wa vijana nchini. Warsha hiyo ya siku tatu ambayo inajumuisha sekretarieti na viongozi wengine wakuu wa BAVICHA, imeandaliwa maalumu kwa ajili ya kujadili na kuweka mpango kazi wa baraza hilo, kwa mwaka 2012-2013 na maandalizi ya mkakati wa miaka mitano (2012-2016).
Katika siku hizo tatu za warsha, baraza litajadili Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana, Sera ya CHADEMA ya Vijana, Kanuni/Mwongozo wa Baraza, utendaji kazi wa vijana wa CHADEMA 2006-2010, katiba ya CHADEMA, utendaji kazi na rasilimali za chama pia Mpango Mkakati wa CHADEMA kwa mwaka 2011-2016.
Hongera BAVICHA Hongera Chadema.
Katika siku hizo tatu za warsha, baraza litajadili Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana, Sera ya CHADEMA ya Vijana, Kanuni/Mwongozo wa Baraza, utendaji kazi wa vijana wa CHADEMA 2006-2010, katiba ya CHADEMA, utendaji kazi na rasilimali za chama pia Mpango Mkakati wa CHADEMA kwa mwaka 2011-2016.
Hongera BAVICHA Hongera Chadema.