Baba Clara
Member
- May 10, 2011
- 94
- 27
KUTOKA GAZETI LA MAJIRA LA LEO JUMAPILI UK4.
Umoja wa vijana wa Chadema(BAVICHA) wamesema rufaa iliyompa ushindi mbunge wa arusha mjini Godbless Lema ni fundisho kwa vyama vya siasa hususani chama cha mapinduzi(CCM) kazi ambayo ameifanya akiwa nje ya bunge ya kuimarisha chama chake ni kubwa tofauti na wenye mawazo kwamba mbunge akiwa nje ya bunge kumdhoofisha.
"Hii ni fundisho kwa vyama vya siasa kazi aliyofanya Lema ya kuimarisha chama kipindi ambacho alikuwa nje ya bunge ni mwiba kwa CCM"
Kauli hiyo ilitolewa Dar es salaam jana na katibu mkuu wa Bavicha mkoa wa Mwanza Salvatory Magafu, wakati akizungumza na gazeti hili kuhusiana najinsi walivyopokea uamuzi wa mahakama ya rufaa Tanzania kwa kumrejeshea ubunge wake Lema.
Alisema jambo hilo lilikuwa wazi labda kwa mgeni wa fani ya sheria. Alifafanua kuwa sheria inaweza kuwa katika kesi ya udhalilishaji anayelalamika na mhusika, lakini jambo hilo halikufanyika kwenye kesi hiyo.
Aliongeza kwamba kwa maoni yake mahakama kuu kanda ya Arusha ilihukumu shauri hilo kisiasa. "Uwamuzi uliotolewa ni maamuzi mazuri" alisema. Kuhusu kazi ya Lema ambayo aliifanya akiwa nje ya bunge Magafu alisema: "inauma Lema kurudi bungeni, kwani kazi aliyoifanya akiwa nje ni kubwa amesaidia kukuza chama....tunaweza kusema ni pigo kwa chama".
Alisema Chadema itaathirika kwa kiasi fulani kwa kipindi ambacho atakuwa bungeni kwani atakuwa hana nafasi ya kukiimarisha chama hicho, ikilinganishwa na kipindi ambacho amekuwa nje.
Kwa upande wake katibu wa Bavicha mkoa wa Tanga Deogratius Kisandu, alisema uamuzi wa mahakama kumurejeshea Lema ubunge fundisho kwa serikali kuwa watu wengine wakivuliwa ubunge wanamwaga sumu nchi nzima.
Alisema baada ya kurejeshewa ubunge nguvu sasa atazielekeza bungeni na jimboni kwake. Alisema hukumu iliyompa ushindi Lema inaleta picha kuwa mahakama haiwezi kupingana na nguvu za ukweli.
Alifafanua kuwa tangu awali mbunge huyo alikuwa akipigana kutafuta ukweli ambao sasa amerejeshewa na mahakama.
Umoja wa vijana wa Chadema(BAVICHA) wamesema rufaa iliyompa ushindi mbunge wa arusha mjini Godbless Lema ni fundisho kwa vyama vya siasa hususani chama cha mapinduzi(CCM) kazi ambayo ameifanya akiwa nje ya bunge ya kuimarisha chama chake ni kubwa tofauti na wenye mawazo kwamba mbunge akiwa nje ya bunge kumdhoofisha.
"Hii ni fundisho kwa vyama vya siasa kazi aliyofanya Lema ya kuimarisha chama kipindi ambacho alikuwa nje ya bunge ni mwiba kwa CCM"
Kauli hiyo ilitolewa Dar es salaam jana na katibu mkuu wa Bavicha mkoa wa Mwanza Salvatory Magafu, wakati akizungumza na gazeti hili kuhusiana najinsi walivyopokea uamuzi wa mahakama ya rufaa Tanzania kwa kumrejeshea ubunge wake Lema.
Alisema jambo hilo lilikuwa wazi labda kwa mgeni wa fani ya sheria. Alifafanua kuwa sheria inaweza kuwa katika kesi ya udhalilishaji anayelalamika na mhusika, lakini jambo hilo halikufanyika kwenye kesi hiyo.
Aliongeza kwamba kwa maoni yake mahakama kuu kanda ya Arusha ilihukumu shauri hilo kisiasa. "Uwamuzi uliotolewa ni maamuzi mazuri" alisema. Kuhusu kazi ya Lema ambayo aliifanya akiwa nje ya bunge Magafu alisema: "inauma Lema kurudi bungeni, kwani kazi aliyoifanya akiwa nje ni kubwa amesaidia kukuza chama....tunaweza kusema ni pigo kwa chama".
Alisema Chadema itaathirika kwa kiasi fulani kwa kipindi ambacho atakuwa bungeni kwani atakuwa hana nafasi ya kukiimarisha chama hicho, ikilinganishwa na kipindi ambacho amekuwa nje.
Kwa upande wake katibu wa Bavicha mkoa wa Tanga Deogratius Kisandu, alisema uamuzi wa mahakama kumurejeshea Lema ubunge fundisho kwa serikali kuwa watu wengine wakivuliwa ubunge wanamwaga sumu nchi nzima.
Alisema baada ya kurejeshewa ubunge nguvu sasa atazielekeza bungeni na jimboni kwake. Alisema hukumu iliyompa ushindi Lema inaleta picha kuwa mahakama haiwezi kupingana na nguvu za ukweli.
Alifafanua kuwa tangu awali mbunge huyo alikuwa akipigana kutafuta ukweli ambao sasa amerejeshewa na mahakama.