Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,558
- 217,846
Wakati Viongozi wote wa kitaifa pamoja na wale wa ccm wakijazana Chato kumuenzi Nyerere lakini kwa kupamba kaburi la Magufuli , kiasi cha Kusababisha Mshangao duniani , Ile Taasisi bora ya vijana barani Africa , BAVICHA , yenyewe imefika Butiama na kupokelewa kwa kishindo na kisha kupelekwa hadi kwenye kaburi la Baba wa Taifa na kuweka mashada ya maua .
Vijana wa Bavicha wakiwa wamevalia fulana zao nzuri zinazochagiza umuhimu wa Katiba Mpya , wamemuenzi Mwl Nyerere Kihalali kwa kufika kwenye malalo yake , badala ya kufanya kama wale wengine walioenda kupiga porojo upande mwingine huku wakishindwa kueleweka Marehemu wanaye muenzi au kumkumbuka ni yupi .
Baada ya shughuli ya kumuombea dua Baba wa Taifa , vijana hao wakaamua kucheza bao kama ishara ya kuuenzi mchezo uliopendwa sana na Hayati Nyerere .
Vijana wa Bavicha wakiwa wamevalia fulana zao nzuri zinazochagiza umuhimu wa Katiba Mpya , wamemuenzi Mwl Nyerere Kihalali kwa kufika kwenye malalo yake , badala ya kufanya kama wale wengine walioenda kupiga porojo upande mwingine huku wakishindwa kueleweka Marehemu wanaye muenzi au kumkumbuka ni yupi .
Baada ya shughuli ya kumuombea dua Baba wa Taifa , vijana hao wakaamua kucheza bao kama ishara ya kuuenzi mchezo uliopendwa sana na Hayati Nyerere .