Bavicha: Taarifa kwa umma mwisho wa kurudisha fomu ni trh 26 April.

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
TAREHE YA UCHAGUZI: Uchaguzi utafanyika siku ya Jumamosi tarehe 28 Mei 2011.

NAFASI ZINAZOGOMBEWA: Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji, Mweka Hazina, Wawakilishi wa BAVICHA kwenye Mkutano Mkuu wa chama na wawakilishi wa BAVICHA kwenye Baraza Kuu la chama.

UMRI UNAORUHUSIWA KUGOMBEA: Kwa mujibu wa Katiba umri wa ujana ni kati ya Miaka 18 na 35. Mgombea anatakiwa kugombea kwenye umri unaomruhusu kumaliza kipindi chake cha uongozi akiwa bado na umri wa Ujana; hivyo wagombea wenye umri wa zaidi ya miaka 30 hawataruhusiwa kugombea ili kufanya viongozi wa vijana wasiwe zaidi ya miaka 35 katika kipindi chao chote cha utumishi katika BAVICHA.

TAREHE ZA KUCHUKUA NA KURUDISHA FOMU: Wagombea watachukua na Kurudisha Fomu kuanzia tarehe 4 Aprili hadi tarehe 26 Aprili. Fomu zitatolewa kuanzia ngazi ya Mkoa, Makao Makuu ya chama na zinaweza kupatikana kwa kubofya hapa.

GHARAMA ZA FOMU: Kwa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji na Mwekahazina watalipia Shilingi Elfu Thelathini Tu (30,000) kwa Fomu.Kwa nafasi za Ujumbe watalipia Shilingi Elfu Kumi tu (10,000).

Taarifa kwa Umma

Kauli mbiu ya BAVICHA-Vijana; Nguvu ya Mabadiliko


John Mnyika (Mb)
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Vijana
 
TAREHE YA UCHAGUZI: Uchaguzi utafanyika siku ya Jumamosi tarehe 28 Mei 2011.

NAFASI ZINAZOGOMBEWA: Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji, Mweka Hazina, Wawakilishi wa BAVICHA kwenye Mkutano Mkuu wa chama na wawakilishi wa BAVICHA kwenye Baraza Kuu la chama.

UMRI UNAORUHUSIWA KUGOMBEA: Kwa mujibu wa Katiba umri wa ujana ni kati ya Miaka 18 na 35. Mgombea anatakiwa kugombea kwenye umri unaomruhusu kumaliza kipindi chake cha uongozi akiwa bado na umri wa Ujana; hivyo wagombea wenye umri wa zaidi ya miaka 30 hawataruhusiwa kugombea ili kufanya viongozi wa vijana wasiwe zaidi ya miaka 35 katika kipindi chao chote cha utumishi katika BAVICHA.

TAREHE ZA KUCHUKUA NA KURUDISHA FOMU: Wagombea watachukua na Kurudisha Fomu kuanzia tarehe 4 Aprili hadi tarehe 26 Aprili. Fomu zitatolewa kuanzia ngazi ya Mkoa, Makao Makuu ya chama na zinaweza kupatikana kwa kubofya hapa.

GHARAMA ZA FOMU: Kwa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji na Mwekahazina watalipia Shilingi Elfu Thelathini Tu (30,000) kwa Fomu.Kwa nafasi za Ujumbe watalipia Shilingi Elfu Kumi tu (10,000).

Taarifa kwa Umma

Kauli mbiu ya BAVICHA-Vijana; Nguvu ya Mabadiliko


John Mnyika (Mb)
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Vijana

Mradi wa rushwa unaanza sasa, ngoja tujipange !
 
Back
Top Bottom