CHAMA CHADEMOKRASIA NA MAENDELEO – CHADEMA.
MKOA WASINGIDA.
TAARIFA KWAVYOMBO VYA HABARI:
MKOA WASINGIDA.
TAARIFA KWAVYOMBO VYA HABARI:
Kwa kuelewa hilo, sisi vijana wa CHADEMA, Mkoa wa Singida tunamwonya Katibu wa Itikadina Uenzi wa CCM Taifa, Bw. Nape Nauye kwa kuwatumia vibaya vijana wa kitanzania wasio na ajira, na ambao ‘wamefika bei' kulingana na matarajio ya mafisadi.Vijana wanaonunulika na mafisadi, hawawezi kamwe kuwa viongozi kwanihawatashindwa ‘kufika bei' siku nyingine na kuuza nchi. Hivyo hawafai kuwaviongozi wa nchi.
Tumepokea kwa masikitiko makubwa kuwa Nape na baadhi ya viongozi Mafisadi wanatumia pesa zao kuwatumia vijana wa kitanzania wasio naajira, na kupandikiza migogoro ndani ya CHADEMA, chama pekee cha kutumainiwa nawatanzania ili kuleta maisha bora. Tunamwonya Nape aachane na siasa za majitakazisizo na tija kwa shida za watanzania.
Badala yake, Nape kama anataka kuwa Mwanasiasa Mzuri, awaeleze watanzania jinsi alivyoshindwa kusimamia mkakati wa kujivua gamba,ulioasisiwa na Chama chake. Alizunguka nchi nzima kuelezea dhana ya kujivuagamba lakini siku hizi anafanya kazi na wale aliowatukana usiku na mchana kuwani magamba.
Nape awaeleze watanzania, jinsi Meli za Katibu Mkuu waChama chake, Abdulrahman Kinana, anavyosafirisha meno ya tembo nje ya nchi wakati serikali inalalamika kila siku kuna ujangili katika mbuga zetu, na itakuwa vema zaidi Nape akijitokeza kuwaambia watanzania kwanini hadi sasa tangu kuibuka kwa taarifa kuwa meli zilikuwa ni za Abdulrahmani Kinana Serikaliya CCM haijazitaifisha meli hizo. Sheria za nchi yetu zipo wazi kuhusu chombo chochote kitakacho kamatwa na maliasili zetu ni lazima kitaifishwe. Je, hivi vyombo vya usafiri vya Katibu Mkuu wa CCM vinangoja nini kutotaifishwa hayo ndo mambo ambayo Nape anaweza kuwaambiawatanzania, na yana manufaa kwao.
Bavicha Mkoa wa Singida, tunawapongeza vijana wenzetu wa Mkoa wa Mwanza kwa kutoa tamko zuri, na sisi vijana wa CHADEMA Mkoa wa Singida hatupo tayari kutumiwa na CCM wala kutumikia mafisadi. Tutakilinda Chama chetu na viongozi wake na hatutakubali propaganda ambazo hazina tija kwawatanzania.
Tunakiomba Chama chetu kiwachukulie hatua vijana wote waliosimamishwa uongozi sehemu mbalimbali nchini lakini wameendelea kujipachika vyeo bandia ili kuhalalisha utoaji wa matamko yasiyo rasmi. Nami kama msemaji wa BAVICHA Mkoa wa Singida, Nasisitiza kuwa hatuna mpango wowote wa kuandamana kusaidia propaganda za CCM. Dhumuni la dirisha kwenye nyumba nikupitisha hewa,cha kushangaza ukilifungua wataingia inzi, mbu na vingine ambavyo havikusudiwa.
Tunachotaka kusema sisi BAVICHA Singida ni kuwa mbu, nzi na kunguni wameshaingia kwenye chama, kilichobaki kunatakiwa kufanyike usafi kwa umakini wasijewakachafua zaidi.
Lakini vijana waliosimamishwa uongozi ndani ya CHADEMAni vema wakajiunga na CCM wazi ili wakasaidie mafisadi waliosababisha maisha magumu kwa watanzania. Watanzania wanajua hali yao ya maisha, na ndio waamuzi sahihi wa Tanzania wanayoitaka, tusiwalishe maneno ya uongo kurutubisha Ufisadi nchini.
Josephat Isango,
MWENYEKITI WA BAVICHA-MKOASINGIDA.