BAVICHA kuanika kila kitu leo

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Baraza la vijana CHADEMA leo linatarajiwa kuweka kila kitu hadharani katika mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika makao makuu ya CHADEMA leo.

BAVICHA ambalo kwa sasa ndiyo baraza bora kabisa la vijana nchini litaweka msimamo wake kuhusiana na ombi la Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe kuwataka kusitisha msimamo wao wa kwenda Dodoma kuzuia mkutano mkuu wa CCM.

BAVICHA ambayo inaungwa mkono na maelfu ya vijana kote nchini tayari ilikwishaandikisha vijana zaidi ya 5000 kutoka sehemu mbalimbali nchini kwenda Dodoma kwa kazi hiyo.

Mkutano huo na waandishi wa habari utafanyika leo makao makuu kuanzia saa 6 nchini na utahutubiwa na viongozi wake wakuu Mwenyekiti Patrobass Katambi,Makamu Mkiti Patrick Sosopi,Katibu Mkuu Julius Mwita na Mratibu wa Baraza hilo kitaifa Edward Simbeye.

Waandishi wote mnakaribishwa!
 
BAVICHA ambayo inaungwa mkono na maelfu ya vijana kote nchini tayari ilikwishaandikisha vijana zaidi ya 5000 kutoka sehemu mbalimbali nchini kwenda Dodoma kwa kazi hiyo.

Mkwala fix huo.Eti tuliandikisha elfu 5!!!!!!!!.Nyooooooo!! Mlianza na elfu 2 baadaye mkapandisha ikawa elfu 4 Sasa elfu 5 ha ha ha!! Acheni mkwala mbuzi huo .Mnaropoka tu bila ushahidi.Mkikutana na waandishi pandisheni kuwa mliandikisha Elfu 10 NA BADO WENGINE WANAENDELEA kujiandikisha!!!!! fix fix fix
 
Mkwala fix huo.Eti tuliandikisha elfu 5!!!!!!!!.Nyooooooo!! Mlianza na elfu 2 baadaye mkapandisha ikawa elfu 4 Sasa elfu 5 ha ha ha!! Acheni mkwala mbuzi huo .Mnaropoka tu bila ushahidi.Mkikutana na waandishi pandisheni kuwa mliandikisha Elfu 10 NA BADO WENGINE WANAENDELEA kujiandikisha!!!!! fix fix fix
I previously thought you were sober!
 
Vipi mpambano wa Lizaboni na Mhishimiwa DC Umefikia wapi. Bado wanagombea uongozi kama Mafisi.


Malizeni kwanza mpambano kati ya BAVICHA na Mbowe.Mbowe akitoa agizo kama mwenyekiti wa Chama Taifa kwa BAVICHA badala ya kulitii moja kwa moja kuwa mheshimiwa mwenyekiti kasema ,wao BAVICHA wanamwambia hilo tukikaa vikao vyetu kwanza tutaliangalia ndio tutoe jibu!!!

Kwa hiyo wanamponda kuwa alitakiwa alipeleke kwenye vikao sio atamke tu kama mwenyekiti!!!

Vitoto vya BAVICHA vimeota sharubu.Mbowe poleeeeeee Una watoto watukutu.Agizo la baba ndani ya nyumba halisikilizwi hadi watoto wakae waongee ndio waseme kwenye kikao chetu tumeamua hivi kwa lile baba yetu ulisema!!

LOOO! BAVICHA wangekuwa wanangu ningewapiga nondo kama kufungwa nifungwe.Nini maana ya kuwa baba kwenye nyumba?
 
Malizeni kwanza mpambano kati ya BAVICHA na Mbowe.Mbowe akitoa agizo kama mwenyekiti wa Chama Taifa kwa BAVICHA badala ya kulitii moja kwa moja kuwa mheshimiwa mwenyekiti kasema ,wao BAVICHA wanamwambia hilo tukikaa vikao vyetu kwanza tutaliangalia ndio tutoe jibu!!! Kwa hiyo wanamponda kuwa alitakiwa alipeleke kwenye vikao sio atamke tu kama mwenyekiti!!! Vitoto vya BAVICHA vimeota sharubu.Mbowe poleeeeeee Una watoto watukutu.Agizo la baba ndani ya nyumba halisikilizwi hadi watoto wakae waongee ndio waseme kwenye kikao chetu tumeamua hivi kwa lile baba yetu ulisema!! LOOO! BAVICHA wangekuwa wanangu ningewapiga nondo kama kufungwa nifungwe.Nini maana ya kuwa baba kwenye nyumba?
Hujui unachokiandika nakuonea huruma sana.Unadhani Bavicha ni sawa na UVCCM ambao hawana ushawishi wowote kwa jamii.Unastahili kuhurumiwa tu
 
Wanajidanganya kuwa nyoyo za Watanzania Magu amezibadilisha na zimeenda tena ccm. Watanzania kwanza waliwavumulia sana CCM, wakashindwa kubadilika.

Wakawakea kimoyo moyo hawakubadilika, Wakawalaani. CCM iliko sasa kwa Watanzania wengi hasa vijana wameilaani CCM.

Uliyemlaani siku zote aonekanapo mzuri wewe uendelea kumuona aliye laanika. Yale afanyayo kukufurahisha hukufikia ukiwa umefura kimoyo moyo na kukasirika zaidi kujiuliza kuwa alikuwa akitambua kuwa alikuwa anakukosea?

Utamsemehe lakini hutasahau. Wakati unaanza kumchukia hadi kufika kumulaani, wewe huanza kujenga urafiki kwingine, wakati anapotafuta bulldozer kufukia mashimo hukuta mashimo maengine yameishakuwa makorongo na hilo bulldozer likijitia hata hayo makorongo kuyafukia litajikuta linatumbukia huko huko. Na wakati huo urafiki wa kwingine unakuwa unakua.

Unakua kwa kiwango kikubwa ili kitambua kuwa unafukia mashimo waliyo yasababisha. Makorongo waliyo yasababisha. Na wanakazana kufukia bila vision. Watanzania wako kimya lakini mwanya ukitokea shangwe itapasuka na ndipo dunia itajua mahali roho zao zilipohamia.
 
Wanajidanganya kuwa nyoyo za Watanzania Magu amezibadilisha na zimeenda tena ccm. Watanzania kwanza waliwavumulia sana ccm, wakashindwa kubadilika. Wakawakemea kimoyo moyo hawakubadilika, Wakawalaani. CCM iliko sasa kwa Watanzania wengi hasa vijana wameilaani ccm.

Uliyemlaani siku zote aonekanapo mzuri wewe uendelea kumuona aliye laanika.

Yale afanyayo kukufurahisha hukufikia ukiwa umefura kimoyo moyo na kukukasirisha zaidi huku ukijiuliza kuwa alikuwa akitambua kuwa alikuwa anakukosea?

Utamsemehe lakini hutasahau. Wakati unaanza kumchukia hadi kufika kumulaani, wewe huanza kujenga urafiki kwingine, wakati anapotafuta bulldozer kufukia mashimo hukuta mashimo maengine yameishakuwa makorongo na hilo bulldozer likijitia hata hayo makorongo kuyafukia litajikuta linatumbukia huko huko.

Na wakati huo urafiki wa kwingine unakuwa unakua. Unakua kwa kiwango kikubwa ili kutambua kuwa unafukia mashimo waliyo yasababisha. Na wanakazana kufukia bila vision. Watanzania wako kimya lakini mwanya ukitokea shangwe itapasuka na ndipo dunia itajua mahali roho zao zilipohamia.
 
BAVICHA songa mbele tunawakubali sana.Mwanza tulijiandaa vizuri kuja dodoma kuzuia mkutano wa Intarahamwe.Tupeni ratiba kamili leo
 
Magufuli saizi yake Bavicha, mkwara wa watoto majeshi yote amehamishia Dodoma! Wangekuja wazazi wao?
Wazazi waliishageuka kitambo. Wanajinadi kuwa sasa cdm kime-graduate toka chama cha uanaharakati na kuwa chama cha siasa. Maba-vichaa yanajitia kichwa ngumu, hayajasoma alama za nyakati.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom