BAVICHA hakukaliki! Viongozi wa juu waandaliwa maandamano nchi nzima...

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,571



*Viongozi wa juu waandaliwa maandamano nchi nzima
*Yadaiwa wameshindwa kutatua kero zinazowakabili

HALI imeendelea kuwa si shwari ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baada ya Makatibu wa Baraza la Vijana Taifa (BAVICHA), kuandaa maandamano makubwa ya nchi nzima yenye nia ya kuwang’oa viongozi wa juu wa umoja huo.

Habari za kuaminika zilizopatikana mjini Dar es Salaam jana, zinasema sababu kubwa ya kuwang’oa viongozi, inatokana na kukosa mwelekeo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Katibu wa BAVICHA Mkoa wa Tanga, Deogratius Kisandu, ilisema hivi sasa makatibu wa umoja huo nchi nzima, wanaandaa mkakati mzito wa kuandamana.

“Tumejipanga na tupo kwenye mkakati mkali wa kuitisha maandamano ya nchi nzima, ili kwanza tuhakikishe Katibu wa BAVICHA Deogratius Mushi na wenzake wanang’oka kwenye nafasi ya ukatibu.

“Hii ni kutokana na wao kushindwa kututetea katika matatizo yanayotukabili, tumejikuta makatibu tunafanya kazi kwa kuletewa taarifa na wenyeviti, tumechoka sasa.

“Tulitarajia angetusaidia kushiriki vikao vya BAVICHA kwa mjibu wa mwongozo wa mabaraza, kwani ibara ya 6.8.6 wajumbe wa Kamati Tendaji, ambapo Katibu huyu na safu yake wamekuwa wakikiuka Katiba ya chama na kuwaita wenyeviti wa mikoa kwenye vikao vya Kamati Tendaji kama kilichofanyika Morogoro mwaka huu.

“Kikao hiki, kilitakiwa kushirikisha makatibu wa BAVICHA wa mikoa kwa mujibu wa katiba na mwongozo wa mabaraza, lakini waliitwa wenyeviti wa mikoa kama fadhila ya uchaguzi uliofanyika mwaka 2011. Katika uchaguzi huo mimi nilikuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa BAVICHA.

“Namshangaa sana bosi wangu huyu na inabidi nihoji hata uwezo wake wa kuliongoza baraza, maana anaposema hakuna migogoro wakati kwenye mitandao ya kijamii kama Jamiiforum, tunasoma vijana wakilumbana na hata Makamu Mwenyekiti wetu, Juliana Shoza kuonekana hafanyi kazi na safu yake, kisa ikionekana hakuna maelewano baina ya viongozi wa juu wa baraza hilo.’

“Kwanza katibu huyu, hatuoni alichokifanya tangu amekamata wadhifa huo, ametembelea mkoa gani nchini akaomba kukutana na viongozi wote wa majimbo na wilaya na kufanya nao vikao kwa maendeleo ya BAVICHA? Sioni kama tuna baraza ila tuna jina la baraza.

“Kashindwa hata kuwatetea viongozi wa mikoa wa umoja wetu, kushiriki Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), badala yake kila anayetoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), leo anaingia kwenye ziara za M4C na wakongwe kuwekwa pembeni au kutokufikiriwa katika baraza.

“Hapa kuna vijana waliogombea ubunge, wana uwezo mzuri kabisa wa kuwa kwenye ziara za M4C, lakini hawafikiriwi, badala ya kuwatetea leo anasema eti kuna virusi.

Alipoulizwa kuhusiana na hali hiyo, Katibu wa BAVICHA Taifa, Deogratius Mushi, alisema hawezi kuzungumzia chochote kuhusiana na taarifa hiyo.

“Jamani siwezi kusema lolote kuhusu madai ya huyo Katibu, andikeni alichosema tu,” alisema Mushi.

KUTOKA CHADEMA TO NCCR
 

Attachments

  • DSC00586.JPG
    DSC00586.JPG
    39.6 KB · Views: 47
  • KAY(1).jpg
    KAY(1).jpg
    64.3 KB · Views: 34
Chadema kuweni makini.hivi mnavyokwenda sio.mtasababisha ccm wakose upinzani mzuri na hivyo wengi wao kujisahau tena kama walivyokuwa wamejisahau huko nyuma.
 
Hivi hizi ngonjera zitaisha lini.Kila kitu maaandamano, kwanini msimalize mambo yenu kwenye vikao vyenu vya chama. Kila siku vyombo vya habari haipendezi bwana. Tumewachoka sana. Huyu wa Tanga sindie alisema nayeye anataka kugombea Uraisi.Acheni hizo bwana
 
wanataka Deo munishi apige kelele mitandani ndo wajue anafanya kazi? me nadhani the guy anadeserve pongezi coz kutokana na malumbano yasiyo na tija yanayoendelea mtu ambaye siyo smart angekuwa ameropoka na yeye...ila yupo kimya na ukimya ndo dawa.
i think kisandu yuko after somethng sio bure...maandamano ya kichama?!! kuupinga uongoz wa bavicha?!! zen anamuattack munishi?!! cdhani kama vijana wa chadema ni mambulura kama kuna tatizo la kiutendaji zen lazima kuna procedure za kufuata.halaaaa!!!!
 
Msidhani kuandamana ni sifa.Hakuna atakaewasapoti na ujinga wenu.Hamuwezi kung'oana kwa mujibu wa katiba za chama?Msifanye kila kijana aonekane mpumbafu!
 
Huyu Kisandu ndiye alisema atagombea Urais 2015.Pia ndiye aliunga mkono wazee wa kabla ya uhuru wawapishe vijana Chadema.Kwa hiyo huyu yuko kundi lilelile la wahuni wa Masalia.
 
Hivi hizi ngonjera zitaisha lini.Kila kitu maaandamano, kwanini msimalize mambo yenu kwenye vikao vyenu vya chama. Kila siku vyombo vya habari haipendezi bwana. Tumewachoka sana. Huyu wa Tanga sindie alisema nayeye anataka kugombea Uraisi.Acheni hizo bwana
Ndugu ni walewale kasoro majina,aite hayo maandamano tuone.cku zote giza na mwanga hujitenga.
 
Hivi hizi ngonjera zitaisha lini.Kila kitu maaandamano, kwanini msimalize mambo yenu kwenye vikao vyenu vya chama. Kila siku vyombo vya habari haipendezi bwana. Tumewachoka sana. Huyu wa Tanga sindie alisema nayeye anataka kugombea Uraisi.Acheni hizo bwana
Huyo mtu sasa naanza kuona kuwa ni kibaraka, au kapokea kitu fulani.
kumbukeni kuna watu wanafanya kila mbinu kuua CDM. so kuna watu watavuruga kama hakutakuwa na mwelekeo mzuri na watu kuchambua mambo (maandamano sijui nini yote si hoja, ila mapandikizi tu!)
 
Huyu Kisandu ndiye alisema atagombea Urais 2015.Pia ndiye aliunga mkono wazee wa kabla ya uhuru wawapishe vijana Chadema.Kwa hiyo huyu yuko kundi lilelile la wahuni wa Masalia.

with no doughts mkuu.ila ni bora wamejionesha wenyew mapema hii!! wanakera sana.
 
Hili suala la bavicha sasa linatuchosha. Badala ya kipindi hiki kufanya tathmini kuona impact ya vijana kwa mwaka mzima ilikuaje ili kujipanga kwa ajili ya mwaka ujao nyie kazi ni migogoro isiyo ya tija kwa harakati za kuleta mabadiliko nchini. Mambo hayo tulizoea kuyasikia kwa magamba, sasa mnataka kuyahamishia huku? Tunaomba kamati kuu ya cdm iliangalie hili kwa jicho la karibu kwani kuna mamluki wanaotumiwa kutuvuruga, tuwatoe mapema ili tusonge mbele.
 
Yale ya bavicha mwanza yameyeyukia wapi?huyu wa tanga hajajifunza tu?ataandamana yeye na kuku na bata wake! Sio vijana wa chadema,hii post ya urais mmeidharau kabisa!!kwamba hata tahira aweza kuwa rais? Au unalala unataka kuamka rais?mnaanza kugawana vipuri vya gari hilohilo mnalosafiria,safari itaendelea kweli? Hii ni vita ya kijing.a kabisa na haitakuwa na mshindi,na jf ndiyo imegeuzwa kuwa jukwaa la kampeni za urais hewa.
 
This now is too much,someone has to stand and stop this nosense
 
Huyo kijana ni mjinga sana.
Yeye na Masalia wenzake wanahangaika usiku na mchana kujaribu kuleta mtafaruku ndani ya Chadema, baada ya mipango yao ya kuhujumu chama chao kugundulika.

Kwanini wasiandamane basi kila siku wanalalamika na kutishia tu?
 
Hivi hizi ngonjera zitaisha lini.Kila kitu maaandamano, kwanini msimalize mambo yenu kwenye vikao vyenu vya chama. Kila siku vyombo vya habari haipendezi bwana. Tumewachoka sana. Huyu wa Tanga sindie alisema nayeye anataka kugombea Uraisi.Acheni hizo bwana

Nahisi hii mikakati ya CCM kuhakikisha chama kinapoteza umoja kabla ya 2015, nyuma ya pazia lazima kuna viroja vinafanyika. Hawa viongozi wa BAVICHA inawezekana kabisa wameshakuwa corrupted!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom