Justinr
JF-Expert Member
- May 22, 2020
- 3,709
- 6,832
Apo mkuu usitake kulazimisha mambo yasio landana unawezaje kulinganisha nchi za Afrika na marekan kwenye swala la chanjo? Wakati kule zipo za kutosha km wahawajachanja ni sababu ya kutotaka uwezi linganisha na Afrika kamwe....alafu tusilazimishane kuchanja mnao ona inamana nendeni mkachanje .Kwahiyo Kenya, Rwanda na Uganda ambako wamehamasishwa na kuhamasika kuchanja Nako pia sababu ya kuwa na "low covarege rate" ni kwamba hawataki?(wenyewe wanakusikiliza).
Huu upuuzi wa kupinga chanjo alianzisha Magufuli na sanasana ni hapa Tanzania, nchi zote zinazotuzunguka watu hawana tatizo na chanjo.
Katika Mambo yaliyoshusha heshima ya Magufuli duniani ni pamoja na hili la kupinga chanjo bila kufanya utafiti wa kisayansi, tusijaribu kuambuliza mapungufu yetu kwa watu wengine.
Wakat unabishana apa nijibu kwanini visiwa vya shelisheli ambapo kwa Afrika ndio tunaweza sema wamechanjwa kwa asilimia kubwa, wamekufa sana kwa korona?