pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 221
- 431
Tarehe 24/05/2019 nilipanda basi tajwa nikielekea mombasa nchini kenya kwa shughuli maalum basi liiliondoka ubungo saa sita mchana, kufika Tanga ilisimama kidogo kisha kuendelea na safari baada ya kutoka nje kidogo ya jiji la Tanga alitokea muhudumu mmoja shombeshombe na kutuomba tiketi zetu bila kujua lengo lake, basi lilisimama na tukapewa maelekezo kuwa tunahamishiwa kwenye coaster ambalo kiuhalisia lilikuwa limejaza sana mizigo na abiria pia, abiria wengine walipanda tukabaki wanne ambao hatukuwa tayari kupanda kwani gari lilikuwa limejaa mno tulisisitiza turudishwe Tanga mjini na tupewe tiketi zetu yule muhudumubwa basi alikataa katakata ndipo nilipoomba msaada wa RTO Tanga maarufu kama afande Solomon (alijizolea umaarufu kwa kupambana na majambazi ubungo na kuokoa hela za benki miaka ya nyuma) nilipiga picha ya gari husika, yule muhudumu baada ya kuona hali hiyo alinifuata kwa vitisho "hata sisi pia tunajua watu usitafute shari hutaiweza" huyu kaka huwa anakata tiketi kwenye ofisi ya tahmeed Tanga kisha kuyasindikiza magari na kuongea na simu muda mrefu akiwapa maelekezo wahudumu wa basi ntaitafuta picha yake pia, alikuwa anajiandaa kuondoka na kutuacha pale usiku ule, nilimkamata na kumbeba tayari kumrusha kwenye mtaro alipiga mayowe kiuhalisia nilikuwa tayari kwa lolote, ndipo alipompigia simu bosi wake kumueleza hali halisi ambapo iliamuriwa gari iondoke na kuendelea na safari....hili gari lina namba za usajili za kenya kama inavyoonekana ila wanatakiwa kuhesimu utu wetu (social media for social justice)