Bashungwa: Bilioni 55.57 kujenga nyumba za walimu kwenye maeneo yasiyo fikika kirahisi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968


Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa ameelezea mafaniko ya Serikali ya awamu ya sita katika kwenye kada ya elumu ambapo amesema mwaka 2021/22 walimu wapya 24749 wameajiriwa huku malimbikizo ya mishahara pamoja na ulipaji wa pesa za pensheni kwa wastafu vikifanyika kwa wakati.

Pamoja na uwepo wa mafanikio haya, kumekuwepo na changamoto tano kubwa zinazo wakabili walimu ambazo ni
  • Kutokulipwa stahiki za uhamisho, likizo na mazishi
  • Kutokupewa vibali vya kwenda masomoni pamoja na malipo ya mafunzo hayo
  • Uwepo wa mawasiliano hafifu kati ya walimu na viongozi wao
  • Kutokupandishwa madaraja
  • Upungufu wa nyumba za kuishi
Serikali imedhamiria kutatua kero tajwa kwa kuwataka wakurugenzi na maafisa wa tume ya utumishi wa elimu kusikiliza na kutatua changamoto hizi kwa haraka kadri zinavyokuwa zinaripotiwa. Aidha, posho na stahiki zao zote zikiwemo zile za mafunzo ni lazima zilipwe pasipo kucheleweshwa.

Kuhusu uwepo wa mawasiliano mabovu miongoni mwa walimu na viongozi wa ngazi ya halmashauri, kata na shule, Waziri amewaagiza viongozi hao kushirikiana vizuri na walimu, pia ameelekeza viongozi wanaohudumia walimu waache tabia ya kukaa maofisini, badala yake waende kwenye shule kufuatilia ufundishaji pamoja na kusikiliza kero zao wakiwa huko.

Katika kutatua changamoto ya upandishwaji vyeo na madaraja, Waziri Bashungwa ameagiza Tume ya Utumishi wa walimu kuziwesha kamati za tume za utumishi za wilaya kuwapandisha walimu madaraja pamoja na kuwapandisha vyeo kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Aidha, amewataka Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanawasimamia watendaji wanaotoa huduma kwa walimu kwa kuhakikisha kuwa wanawafuata waalimu mashuleni huku akipiga marufuku kuwaacha walimu wakipita kila ofisi ya halmashauri wakitafuta huduma kwani wanapaswa kupelekewa huduma shuleni badala ya watoa huduma kukaa maofisini.

Pia, mwalimu akiandika barua kwenye mamlaka ya Serikali za mitaa akitafuta huduma anapaswa kujibiwa kwa maandishi ndani ya siku saba.

Kuhusu upungufu wa nyumba za walimu, Serikali imeanza kushughulikia jambo hili kwa kutenga bilioni 55.57 kwa kuanzia ili kujenga nyumba kwenye maeneo yasiyofikika kirahisi na itaendelea kuboresha kila mwaka.
 
Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa ameelezea mafaniko ya Serikali ya awamu ya sita katika kwenye kada ya elumu ambapo amesema mwaka 2021/22 walimu wapya 24749 wameajiriwa huku malimbikizo ya mishahara pamoja na ulipaji wa pesa za pensheni kwa wastafu vikifanyika kwa wakati.
Asante kwa taarifa.
P
 
Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa ameelezea mafaniko ya Serikali ya awamu ya sita katika kwenye kada ya elumu ambapo amesema mwaka 2021/22 walimu wapya 24749 wameajiriwa huku malimbikizo ya mishahara pamoja na ulipaji wa pesa za pensheni kwa wastafu vikifanyika kwa wakati.
Waeleze na changamoto sio mafanikio tu
 
Blah Blah Blah kutoka kwa waziri, what?kuboresha huduma kwa waalimu!

loooooo my minister hii it sounds very familiar!,my minister may be you still very young, nenda pale wizarani na omba Ile ripoti ya Mh.J.Makwetta(rip), naelewa imepitwa na wakati ila isome kwanza kabla hujaanza kutoa kauli kama hizi,mazuzu watakuamini ila mimi sio zuzu, nakuona ur lying 🤥 big time!
 
Mmeogopa Nini!!?

Walimu mbona ni wapole na wajinga kama mnavofanya miaka YOTE!!?

Waajiriwa wa mwaka 2014 wamekaa bila kupanda cheo kwa miaka saba na nyie mmewapandisha cheo kimoja tu badala ya viwili kwa mujibu wa SHERIA!je mmeona wamegoma kufanya KAZI!!?

Si wamezoea matatizo yao!!?

Japo sisi ndio waasisi wa Taifa hili na tunadharaulika SANA!!

Hatutaki blah blah

Tunataka katiba mpya kama SHERIA Mama ya kusimamia maslahi ya wafakazi na sio blah blah!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"
 
Huyu waziri mimi sijamwelewa ko hizo barua zitajileta zenyewe mpaka halmashauri ili ziingizwe kwenye file la mwalimu anayetaka huduma ?Au hao maafisa wa halmashauri wataota kwamba kuna mwalimu yupo shule fulani ameandika barua ya kutaka huduma fulani tufuate kwani tukidhani watachukua wanapotembelea watatembelea shule ngapi!
 
Back
Top Bottom