Bashungwa awaonya Wakandarasi Wazawa wanaosaini tenda kisha wanaingia mitini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
3,819
13,582
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amezinyoshea kidole baadhi ya Kampuni za Makandarasi Wazawa zinazoshindwa kutekeleza miradi na tenda za ujenzi wanazopewa kwa weledi na mujibu wa mikataba na kuanza kuwazungusha waliowapa kazi ambapo kitendo hicho kinaharibu taswira ya Makampuni ya Makandarasi wengine nchini.

Bashungwa ametoa onyo hilo, leo Septemba 04, 2024 jijini Dar es salaam wakati akifungua Mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kujadili masuala ya mazingira katika utekelezaji wa miundombinu nchini.

“Kuna Makandarasi mnaochukua zabuni za Ujenzi wa Majengo lakini baada ya kusaini mkataba, uswahili unaanza mpaka aliyekupa kazi anajiuliza hawa ndio Wazawa ambao Serikali inawatengenzea mazingira ya kuwapatia fursa mara dufu, sasa niwaombe kabla hatujachukua hatua mjirekebishe” amesisitiza Bashungwa.
WhatsApp Image 2024-09-04 at 19.27.57_9fb07030.jpg

WhatsApp Image 2024-09-04 at 19.27.56_b925af14.jpg
Bashungwa ameziagiza Bodi ya Usajili ya Wakandarasi (CRB), Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili ya Wakadiriaji Majenzi na Wabunifu wa Majengo (AQRB) kuanza kuchukua hatua baadhi ya Kampuni ya Makandarasi ya ujenzi yanayoshindwa kutekeleza kazi kwa weledi (Makanjanja).

Kadhalika, Bashungwa ameeleza kuwa dhamira ya Mheshimiwa Rais ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuwawezesha Makandarasi Wazawa ambapo tayari Wizara ya Ujenzi imesharekebisha masharti na kutoa fursa za ushiriki wa utekelezaji wa miradi kwa Wakandarasi nchini.
WhatsApp Image 2024-09-04 at 19.27.57_66ea1b59.jpg
Bashungwa amewataka Makandarasi wanaofanya kazi za ujenzi wa majengo ya Serikali na Binafsi kutoyafumbia macho baadhi ya Makampuni yanayoharibu taswira ya taaluma yao na kuhakikisha wanalinda weledi na taaluma hiyo kwa kushirikiana.

Bashungwa ameeleza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi itaendelea kuhakikisha usimamizi wa ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara, madaraja pamoja na majengo yanaenda sambamba na utunzaji wa mazingira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Chemba ya Sekta ya Ujenzi na Miundombnu Tanzania, Bw. Steven Mkomwa ameeleza kuwa mkutano huo umewakutanisha wadau mbalimbali kuziangazia Sera, Sheria na Teknolojia zitakavyoweza kusaidia Sekta ya Ujenzi na kuweza kutoa mchango chanya katika masuala ya mazingira pamoja na uwepo wa miundombinu ya kijani.
 
Baadhi ya wakandarasi wazawa ni kichefuchefu. Walikuwa wanalilia kupewa tenda lakini kazi wanazofanya ni vioja. Wapo kwa ajili ya kuiba pesa za umma.

Wakandarasi wazawa wanaheshimu labda pesa za World Bank mana wanapigwa Mkwara kwamba watakuja watu wa World Bank kukagua. Lakini pesa zinazotolewa na serikali ya Tanzania wakandarasi wazawa wanazipiga tu.

Miradi mibovu lakini waidhinishiwa malipo kama siyo kushirikiana ni nini!

NB. Siyo wote.
 
Tatizo kubwa ni wakandarasi baadhi kuweka bei ndogo sana kwa sasa ambazo haziendani na uhalisia ,wakipata kazi wanakuta mambo tofauti.
Pili mtu anaomba kazi hana rasilimali zakufanyia kazi matokeo yake anakimbia .


Suluhisho ni kuchagua zabuni zinazoendana na uhalisia ,pili wakandarasi wanatakiwa kuangalia uwezo wakufanya kazi husika kabla ya kubet kuomba
 
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amezinyoshea kidole baadhi ya Kampuni za Makandarasi Wazawa zinazoshindwa kutekeleza miradi na tenda za ujenzi wanazopewa kwa weledi na mujibu wa mikataba na kuanza kuwazungusha waliowapa kazi ambapo kitendo hicho kinaharibu taswira ya Makampuni ya Makandarasi wengine nchini.

Bashungwa ametoa onyo hilo, leo Septemba 04, 2024 jijini Dar es salaam wakati akifungua Mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kujadili masuala ya mazingira katika utekelezaji wa miundombinu nchini.

“Kuna Makandarasi mnaochukua zabuni za Ujenzi wa Majengo lakini baada ya kusaini mkataba, uswahili unaanza mpaka aliyekupa kazi anajiuliza hawa ndio Wazawa ambao Serikali inawatengenzea mazingira ya kuwapatia fursa mara dufu, sasa niwaombe kabla hatujachukua hatua mjirekebishe” amesisitiza Bashungwa.
Bashungwa ameziagiza Bodi ya Usajili ya Wakandarasi (CRB), Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili ya Wakadiriaji Majenzi na Wabunifu wa Majengo (AQRB) kuanza kuchukua hatua baadhi ya Kampuni ya Makandarasi ya ujenzi yanayoshindwa kutekeleza kazi kwa weledi (Makanjanja).

Kadhalika, Bashungwa ameeleza kuwa dhamira ya Mheshimiwa Rais ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuwawezesha Makandarasi Wazawa ambapo tayari Wizara ya Ujenzi imesharekebisha masharti na kutoa fursa za ushiriki wa utekelezaji wa miradi kwa Wakandarasi nchini.
Bashungwa amewataka Makandarasi wanaofanya kazi za ujenzi wa majengo ya Serikali na Binafsi kutoyafumbia macho baadhi ya Makampuni yanayoharibu taswira ya taaluma yao na kuhakikisha wanalinda weledi na taaluma hiyo kwa kushirikiana.

Bashungwa ameeleza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi itaendelea kuhakikisha usimamizi wa ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara, madaraja pamoja na majengo yanaenda sambamba na utunzaji wa mazingira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Chemba ya Sekta ya Ujenzi na Miundombnu Tanzania, Bw. Steven Mkomwa ameeleza kuwa mkutano huo umewakutanisha wadau mbalimbali kuziangazia Sera, Sheria na Teknolojia zitakavyoweza kusaidia Sekta ya Ujenzi na kuweza kutoa mchango chanya katika masuala ya mazingira pamoja na uwepo wa miundombinu ya kijani.
Huyu dogo namkubali sana yuko vizuri.
 
Back
Top Bottom