Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.
Treni la uchaguzi linapozidi kuchanja mbuga si haba kukumbushana tunapojikwaa hapa na pale ili miradi tuweze kufika salama. Katika harakati kama hizi ni vizuri kuirejea historia ili kuweza kusonga tukiwa kifua mbele zaidi. Ndiyo maendeleo hayo ati!
Miaka ya nyuma, Mzee ruksa akiwa mgombea mpendekezwa wa CCM aliwahi kusema, "mimi mgombea wa chama ni kama mwali anayetaka kuolewa. Si sahihi sana kwangu, kujipigia mno debe." Maneno ya hekima kabisa.
Akiendelea mzee ruksa alisema, "mwali anayetaka kuolewa akiulizwa, eti unataka kuolewa? Yeye hucheka cheka tu na hiyo ndiyo dalili kuwa amekubali huyo!" Akamalizia, "akishabikia kwenye kuolewa huko - mchimvi huyo, mchimvi huyo!" Maneno kuntu kabisa.
CCM, mbona huyu mwali wetu wa sasa anatuacha hoi na midomo ikiwa wazi? Ama kwa hakika kuna mengi anasema ambayo kwa kweli ni bora angeshauriwa angalau akakaa kimya tu. Kujikweza mno hadi kudhani na kutaka kutuaminisha ati tusipomchagua yeye kama taifa tutakuwa tumepata hasara isiyo mfano ni kuvuka mipaka kusiko kwa lazima hata kidogo.
Tumshaurini kama anasikia. Inahitaji busara ndogo sana kuona walakini mkubwa kwenye kujipigia debe huku. Hawakukosea waswahili kunena kuwa: "chema chajiuza na kile kingine chajitembeza."
Upande mwingine ni katika ITV dak. 45 majuzi. Katika kipindi hicho, amenukuliwa Dk. Bashiru akitamka kuwa hawa wasanii wakubwa wakubwa katika mikutano ya mgombea wetu huyu wapo kuwa kwa kujitolea zaidi.
Kuwa wasanii hawa hawalipwi chochote na wanafanya show zote kwa kumpenda mno mgombea wetu na chama chetu. Kuwa wasanii hawa ni wanachama wetu kama tulivyo wengine wakiwamo kina nchukuma na kina vibajaji.
Bashiru alionyesha kuwa hata kwa nyomi la vyombo vya habari (vya umma na binafsi) vinavyomfuatilia vilivyo mgombea wetu na chama chetu ni mapenzi tu ya moyo kutokana na kukubalika kwake. Hayo hayo kama ya kina kiba, diamond na kina konde boy.
Yote kheri. Hivi bashiri anawafanya watanzania wajinga kiasi hicho? Kuwa hayapo maslahi binafsi ya wazi au ya hisani sasa au baadaye kwa taasisi na watu wa namna hii wakiwamo wasanii wetu hawa?
Vipi misukosuko zikiwamo kesi za kubambikiziwa na hata zile pendwa za kutakatisha pesa kwa wale wanaojaribu kujitokeza pande zile zingine?
Kwamba, watanzania hawanazo kumbukumbu hai za kufungiwa zikiwamo biashara, bambikizi bambikizi zikwamo kodi na mashinikizo lukuki yenye mrengo wa kushinikiza kutengwa kwa vyama vya upinzani ili kujiwekea ukiritimba wa fursa zote? Hii mbona itakuwa kujidanganya wenyewe?
Ndani ya CCM hatuna budi kutofautisha kauli za wanaojinasibu kuwa ni kina darasa la saba. Hasa wale ndugu zetu wapendwa akina vibajaji na kina nchukuma.
Bashiru, pole pole, Kabudi na hata Kafulila hamna maneno mazuri kweli ya kumjenga mgombea wetu huyu ili asiendelee kuwa kituko zaidi machoni mwa watu na hata kwa watoto wadogo?
Nchukuma na vibajaji kutokuona umuhimu wa midahalo ni sawa. Lakini hata nyinyi wakuu?
Jitendeeni haki basi ili angalau usomi wenu ukaweze kuwa na mchango wa maana japo kidogo kwenye nchii hii?
Jamani tu wamoja:
Kwa pamoja tuwasaidie watia nia wetu kukubalika kwa wananchi
Uchaguzi huu na usitufanye kujitoa hadi ufahamu wa kawaida tu.
Niombe kuwasilisha.
Treni la uchaguzi linapozidi kuchanja mbuga si haba kukumbushana tunapojikwaa hapa na pale ili miradi tuweze kufika salama. Katika harakati kama hizi ni vizuri kuirejea historia ili kuweza kusonga tukiwa kifua mbele zaidi. Ndiyo maendeleo hayo ati!
Miaka ya nyuma, Mzee ruksa akiwa mgombea mpendekezwa wa CCM aliwahi kusema, "mimi mgombea wa chama ni kama mwali anayetaka kuolewa. Si sahihi sana kwangu, kujipigia mno debe." Maneno ya hekima kabisa.
Akiendelea mzee ruksa alisema, "mwali anayetaka kuolewa akiulizwa, eti unataka kuolewa? Yeye hucheka cheka tu na hiyo ndiyo dalili kuwa amekubali huyo!" Akamalizia, "akishabikia kwenye kuolewa huko - mchimvi huyo, mchimvi huyo!" Maneno kuntu kabisa.
CCM, mbona huyu mwali wetu wa sasa anatuacha hoi na midomo ikiwa wazi? Ama kwa hakika kuna mengi anasema ambayo kwa kweli ni bora angeshauriwa angalau akakaa kimya tu. Kujikweza mno hadi kudhani na kutaka kutuaminisha ati tusipomchagua yeye kama taifa tutakuwa tumepata hasara isiyo mfano ni kuvuka mipaka kusiko kwa lazima hata kidogo.
Tumshaurini kama anasikia. Inahitaji busara ndogo sana kuona walakini mkubwa kwenye kujipigia debe huku. Hawakukosea waswahili kunena kuwa: "chema chajiuza na kile kingine chajitembeza."
Upande mwingine ni katika ITV dak. 45 majuzi. Katika kipindi hicho, amenukuliwa Dk. Bashiru akitamka kuwa hawa wasanii wakubwa wakubwa katika mikutano ya mgombea wetu huyu wapo kuwa kwa kujitolea zaidi.
Kuwa wasanii hawa hawalipwi chochote na wanafanya show zote kwa kumpenda mno mgombea wetu na chama chetu. Kuwa wasanii hawa ni wanachama wetu kama tulivyo wengine wakiwamo kina nchukuma na kina vibajaji.
Bashiru alionyesha kuwa hata kwa nyomi la vyombo vya habari (vya umma na binafsi) vinavyomfuatilia vilivyo mgombea wetu na chama chetu ni mapenzi tu ya moyo kutokana na kukubalika kwake. Hayo hayo kama ya kina kiba, diamond na kina konde boy.
Yote kheri. Hivi bashiri anawafanya watanzania wajinga kiasi hicho? Kuwa hayapo maslahi binafsi ya wazi au ya hisani sasa au baadaye kwa taasisi na watu wa namna hii wakiwamo wasanii wetu hawa?
Vipi misukosuko zikiwamo kesi za kubambikiziwa na hata zile pendwa za kutakatisha pesa kwa wale wanaojaribu kujitokeza pande zile zingine?
Kwamba, watanzania hawanazo kumbukumbu hai za kufungiwa zikiwamo biashara, bambikizi bambikizi zikwamo kodi na mashinikizo lukuki yenye mrengo wa kushinikiza kutengwa kwa vyama vya upinzani ili kujiwekea ukiritimba wa fursa zote? Hii mbona itakuwa kujidanganya wenyewe?
Ndani ya CCM hatuna budi kutofautisha kauli za wanaojinasibu kuwa ni kina darasa la saba. Hasa wale ndugu zetu wapendwa akina vibajaji na kina nchukuma.
Bashiru, pole pole, Kabudi na hata Kafulila hamna maneno mazuri kweli ya kumjenga mgombea wetu huyu ili asiendelee kuwa kituko zaidi machoni mwa watu na hata kwa watoto wadogo?
Nchukuma na vibajaji kutokuona umuhimu wa midahalo ni sawa. Lakini hata nyinyi wakuu?
Jitendeeni haki basi ili angalau usomi wenu ukaweze kuwa na mchango wa maana japo kidogo kwenye nchii hii?
Jamani tu wamoja:
Kwa pamoja tuwasaidie watia nia wetu kukubalika kwa wananchi
Uchaguzi huu na usitufanye kujitoa hadi ufahamu wa kawaida tu.
Niombe kuwasilisha.