Naona mambo ni moto kweli kweli, inasemekana Ndugai aliwekwa kizuizini na barua yake ya kujiuzulu Uspika hakuiandika yeye ni kwa mujibu wa hii tweet.
Sisi yetu mambo, maana malipo ni hapa hapa. Hakika muosha huoshwa.
Sisi yetu mambo, maana malipo ni hapa hapa. Hakika muosha huoshwa.
- Tunachokijua
- JamiiForums imefatilia taarifa hii na kubaini kuwa mnamo Desemba 4, 2018 Dkt. Bashiru alihojiwa kuhusu uzushi uliovuma katika mtandao wa Twitter dhidi yake ambapo alikana kutumia mtandao wowote wa kijamii.
Dkt. Bashiru alisema:
“Watu wanaonijua wanafahamu jinsi ninavyotumia simu, sipo huko na sina Instagram, Twitter, WhatsApp, Facebook wala mfumo wa barua pepe kwenye simu yangu, ni wazushi hao puuzeni hizo habari”
Kwa mantiki hiyo, Uvumi huo ulioenea kwenye mtandao wa Twitter ni uzushi kwa sababu akaunti inayoeneza ujumbe huo imesajiliwa mwaka 2014.
Bashiru Ally Kakurwa alizaliwa Wilaya ya Bukoba Vijijini Januari 1, 1968, alichaguliwa kuwa katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Mei 31, 2018.
Kabla ya kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Bashiru alikuwa mhadhiri katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Februari 26, 2021 aliteuliwa na Rais wa awamu ya 5, Hayati John Magufuli kuwa katibu mkuu kiongozi kisha baadae Machi 31, 2021 aliteuliwa na Rais wa awamu ya 6, Samia Suluhu Hassan kuwa Mbunge kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.