Bashe: Taifa linahitaji maombezi 'limekosa mwelekeo kutokana na mapepo'

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
May 24, 2008
10,942
428
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Hussein Bashe amesema kuwa taifa linahitaji kuombewa na viongozi wa dini kwa madai kuwa kuna pepo mbaya anayelisumbua.

Bashe alitoa kauli hiyo juzi jioni katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye uzinduzi wa DVD inayojulikana kwa jina la ‘Muziki wa Injili' iliyoimbwa na Kwaya ya Mbiu ya Kanisa la Wasabato, Tandale.

Aliwaomba viongozi hao kufunga na kuiombea Tanzania ili kuliondoa pepo linalosababisha kuwepo kwa hali ya kutoelewana kati ya viongozi wa juu wa nchi kwa lengo la kuondoa matendo ya kifisadi na udini yanayochochewa na wanasiasa walioshindwa kutimiza wajibu wao.

Bashe alisema kuwa kilichoifanya nchi ifike hapa ilipo ni viongozi walioshindwa kuwajibika kwa wananchi waliowachagua na badala yake wameamua kutengeneza fitina ikiwemo kutumia kivuli cha udini.

"…Taifa limekosa mwelekeo kutokana na pepo mbaya ambaye ameanzia juu hali inayoashiria kuwa wanasiasa wameshindwa hivyo inahitajika nguvu ya viongozi wa dini kutushika mkono wanasiasa na kutuonyesha njia sahihi," alisema na kuwaongoza waamini kuchangia sh milioni 22 zitakazotumika kuwafungulia chuo cha ufundi stadi vijana wa Tandale.
 
pepo la ufisadi lililoko CCM ni kiburi sana hata likemewe vipi halitoki dawa ni kuwaomba viongozi wa dini waitambue NGUVU YA UMMA na kuisupport ili tuiondoe CCM!
 
tatizo hawa wa ccm sometimes wanaongea haya bcs walikosa uongozi au walifanyiwa tuu! SIWAAAMINI KABISAA HAWA CCM WOOTE WACHAFUU!
 
pepo la ufisadi lililoko CCM ni kiburi sana hata likemewe vipi halitoki dawa ni kuwaomba viongozi wa dini waitambue NGUVU YA UMMA na kuisupport ili tuiondoe CCM!

Hapo umenifurahisha tunakemea pepo kwa jinsi ya rohoni baada ya hapo tunarudi mwilini kwa matendo..GOOOOD!!!
 
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Hussein Bashe amesema kuwa taifa linahitaji kuombewa na viongozi wa dini kwa madai kuwa kuna pepo mbaya anayelisumbua.



Bashe alitoa kauli hiyo juzi jioni katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye uzinduzi wa DVD inayojulikana kwa jina la ‘Muziki wa Injili' iliyoimbwa na Kwaya ya Mbiu ya Kanisa la Wasabato, Tandale.



Aliwaomba viongozi hao kufunga na kuiombea Tanzania ili kuliondoa pepo linalosababisha kuwepo kwa hali ya kutoelewana kati ya viongozi wa juu wa nchi kwa lengo la kuondoa matendo ya kifisadi na udini yanayochochewa na wanasiasa walioshindwa kutimiza wajibu wao.



Bashe alisema kuwa kilichoifanya nchi ifike hapa ilipo ni viongozi walioshindwa kuwajibika kwa wananchi waliowachagua na badala yake wameamua kutengeneza fitina ikiwemo kutumia kivuli cha udini.



"…Taifa limekosa mwelekeo kutokana na pepo mbaya ambaye ameanzia juu hali inayoashiria kuwa wanasiasa wameshindwa hivyo inahitajika nguvu ya viongozi wa dini kutushika mkono wanasiasa na kutuonyesha njia sahihi," alisema na kuwaongoza waamini kuchangia sh milioni 22 zitakazotumika kuwafungulia chuo cha ufundi stadi vijana wa Tandale.
Hayo maneno yenye red, kweli kayasema kwa dhati au ndo maandalizi ya 2015!!!!:A S 13:
 
Bashe...tumeshaomba sana, tunachosubiri ni majibu ya maombi yetu...ambayo ni chama na serikali mbadala ya kuiongoza nchi yetu ya Tanzania na si CCM
 
dogo hajui somalia ilipoteza uelekeo toka zamani? au anaongelea bongo?
 
dogo ni mfanyakazi wa habari corparation ambayo ni ya rostam haziz sasa pimeni maneno yake na vitendo
 
Hayo maneno yenye red, kweli kayasema kwa dhati au ndo maandalizi ya 2015!!!!:A S 13:

Ndugu yangu nakwambia mpaka ifike hiyo 2015 tutaona mengi kwani tayari wameshaanza mbio kabla ya filimbi, huyo Bashe ndiye aliyeshiriki kwa nguvu kubwa ya kipesa aliyopewa na Rostam pamoja na EL kumg'oa Seleli wa Nzega ili aupate Ubunge na kweli alishinda lakini kumbe hakujua kuwa kundi jingine ndani ya CCM lilikuwa linaona bora ubunge aupate yule Mrundi kwani yeye Bashe si kutoka kundi la Makamba na JK, sasa naona wameanza kujipanga kwa nguvu zote kwani ni juzijuzi tu EL naye alikuwa na waimbaji sijui wa wapi vile na alitoa kauli kama hii ya Bashe na eti EL ataishawishi serikali kuongeza mishahara...mmmhhhhh ama kweli shetani kavaa joho/Kanzu madhahabuni
 
Taratibu mh. Bashe hayo mapepo unayoomba yakemewe yasije yakawalipukia nyie wenyewe na chama chenu!!!
 
Sasa hivi tutakuwa tunamwamini mtu kwa kuangalia kwanza historia yake. Pamoja na mazuri ambayo bashe ameongea sina uhakika kama ana 'moral authority' ya kuongea hivyo hadharani. Mtanisaidia wenzangu.
 
Makanisa huwa yanajaa kama watu either wana shida na matatizo kama ilivyo kwa watanzania wengi,ama kama wamebarikiwa,makanisa huwa yananufaika either or,hata hivyo makanisa ya Afrika yanajaa kutokana na wakazi wake kuwa masikini na wenye magonjwa mengi wasiokuwa na matumaini ya maisha kabisa,wenye njaa na wasiokuwa na elimu,ndo ukweli huo.

Na huyo bashe anayedai nchi ina mapepo and so iombewe,je anajua nani kalitupia Taifa mapepo na kwasababu gani?Badala ya kuendelea kuomba mchawi asituloge ama kututupia mapepo,kwanini tusimkamate huyo mchawi,tummalizie mbali yeye na mapepo yake?Kiutaratibu,mtu huyaachia mapepo yaingie ama huyakaribisha yeye mwenyewe,sasa nani kakaribisha mapepo kiasi kwamba yamewatawala viongozi na hivyo kufanya maamuzi ya kimapepo?Sidhani kama kila mwananchi wa Tanzania ameyakaribisha mapepo,lazima kuna walioyakaribisha,sidhani kama ni wote.
 
unajua saa nyingine hata haya mapepo tunayaonea tu, hivi ni kweli Watanzania hatujuhi matatizo yetu kweli kiasi cha kumsingizia pepo?
Unataka kuniamboa issue ya Dowans, EPA, IPTL na zingine kama hizo ni mapepo, hayo ni mapepo ya aina gani?

yeye (Bashe) alipotolewa na kina Kingwangwalah anataka kutuambia lilikuwa ni pepo? au hajuhi sababu gani zilizomnyima kuongoza jimbo la Nzega?
 
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Hussein Bashe amesema kuwa taifa linahitaji kuombewa na viongozi wa dini kwa madai kuwa kuna pepo mbaya anayelisumbua.



Bashe alitoa kauli hiyo juzi jioni katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye uzinduzi wa DVD inayojulikana kwa jina la ‘Muziki wa Injili' iliyoimbwa na Kwaya ya Mbiu ya Kanisa la Wasabato, Tandale.



Aliwaomba viongozi hao kufunga na kuiombea Tanzania ili kuliondoa pepo linalosababisha kuwepo kwa hali ya kutoelewana kati ya viongozi wa juu wa nchi kwa lengo la kuondoa matendo ya kifisadi na udini yanayochochewa na wanasiasa walioshindwa kutimiza wajibu wao.



Bashe alisema kuwa kilichoifanya nchi ifike hapa ilipo ni viongozi walioshindwa kuwajibika kwa wananchi waliowachagua na badala yake wameamua kutengeneza fitina ikiwemo kutumia kivuli cha udini.



"…Taifa limekosa mwelekeo kutokana na pepo mbaya ambaye ameanzia juu hali inayoashiria kuwa wanasiasa wameshindwa hivyo inahitajika nguvu ya viongozi wa dini kutushika mkono wanasiasa na kutuonyesha njia sahihi," alisema na kuwaongoza waamini kuchangia sh milioni 22 zitakazotumika kuwafungulia chuo cha ufundi stadi vijana wa Tandale.

matatizo yetu watz kwa sasa ni ya kiuchumi zaid and so need uvumbuzi wenye mantiki kiuchumi. huyu dogo Hussein akafungue kanisa....aah no i mean msikiti(hussein) akatangaze injili njema kwa watu wote. mtu kama huyu eti ndo mafisadi walitaka kumwingiza kwenye ubunge then wampe uwaziri....halafu eti tunatarajia watanzania tusiendeleee kuliwa na funza???!!! how ikiwa watu wenyewe ndo kama hawa??
 
Bashe,wakati ule mwenyekti wa ccm alipotengewa majini yamlinde kutoka kwa she yahya mbona hakusema tukemee?? Au kuna majini mazuri na mabaya?anyway!
 
Makanisa huwa yanajaa kama watu either wana shida na matatizo kama ilivyo kwa watanzania wengi,ama kama wamebarikiwa,makanisa huwa yananufaika either or,hata hivyo makanisa ya Afrika yanajaa kutokana na wakazi wake kuwa masikini na wenye magonjwa mengi wasiokuwa na matumaini ya maisha kabisa,wenye njaa na wasiokuwa na elimu,ndo ukweli huo.

Na huyo bashe anayedai nchi ina mapepo and so iombewe,je anajua nani kalitupia Taifa mapepo na kwasababu gani?Badala ya kuendelea kuomba mchawi asituloge ama kututupia mapepo,kwanini tusimkamate huyo mchawi,tummalizie mbali yeye na mapepo yake?Kiutaratibu,mtu huyaachia mapepo yaingie ama huyakaribisha yeye mwenyewe,sasa nani kakaribisha mapepo kiasi kwamba yamewatawala viongozi na hivyo kufanya maamuzi ya kimapepo?Sidhani kama kila mwananchi wa Tanzania ameyakaribisha mapepo,lazima kuna walioyakaribisha,sidhani kama ni wote.

Aliyekaribisha mapepo humjui? Ulikuwepo kwenye mkutano wake pale jangwani alipozirai? anga lilikuwa limejaa uchafu mtupu! nchi hii inahitaji maombi ya kweli, ama sivyo blah blah zitakuwa nyingi lakini shida zinabaki pale pale...
 
Hizi mbio za 2015,ametumwa na kikosi kazi, wameshaanza kupiga jaramba. Tutamtambua Bashe kwa matendo. Anatamka maneno hayo huku bado analala na kuamkia kwenye lindi la ufisadi ulitopea! Tuanze kumuombea yeye na task force ya RA.
 
Hizi mbio za 2015,ametumwa na kikosi kazi, wameshaanza kupiga jaramba. Tutamtambua Bashe kwa matendo. Anatamka maneno hayo huku bado analala na kuamkia kwenye lindi la ufisadi ulitopea! Tuanze kumuombea yeye na task force ya RA.

Binafsi simfahamu bali najaribu kufikiri juu ya ulichokisema,nani ambae hapa JF atakuja na kusema yeye ni Msafi hana uhusiano na Mafisadi PAPA au Nyangumi.
Ninaanza wanao lala na kuamka kwa mafisadi PAPA ama Nyangumi

wafanyakazi wa vodacom RA ni shareholder
wafanyakazi wa CRDB Mengi ni shareholder
Wafanyakazi GGM Mafisadi wanaopora rasilimali zetu wapo huko
Wafanyakazi wa TIGO Mafisadi wanaotuibia sekunde unalipa kwa garama dk
Wafanyakazi Airtel mafisadi wanaotuibia kwa matangazo mazuri tofauti
na garama halisi
Wafanyakazi wa Bank M
Wafanyakazi wa Quality Group
wafanyakazi wa Twiga Cement
Wafanyakazi wa IPP
kwa njia moja ama nyingine wengine humo ni mawakala wa vocha za mafisadi ama tunawasaidia kuhamisha rasilimali za nchi tunafanya kazi kwenye Mabenki tuna shiriki kuhamisha peasa zao kwenda ulaya.
now tujiulize tunahaki hiyo ya kumnyoshea BASHE mkono? kuhusiana na hoja kwamba anafanyakazi kwa RA?

wana JF tujadili issue na sio personalities.
 
Back
Top Bottom