OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 428
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Hussein Bashe amesema kuwa taifa linahitaji kuombewa na viongozi wa dini kwa madai kuwa kuna pepo mbaya anayelisumbua.
Bashe alitoa kauli hiyo juzi jioni katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye uzinduzi wa DVD inayojulikana kwa jina la ‘Muziki wa Injili' iliyoimbwa na Kwaya ya Mbiu ya Kanisa la Wasabato, Tandale.
Aliwaomba viongozi hao kufunga na kuiombea Tanzania ili kuliondoa pepo linalosababisha kuwepo kwa hali ya kutoelewana kati ya viongozi wa juu wa nchi kwa lengo la kuondoa matendo ya kifisadi na udini yanayochochewa na wanasiasa walioshindwa kutimiza wajibu wao.
Bashe alisema kuwa kilichoifanya nchi ifike hapa ilipo ni viongozi walioshindwa kuwajibika kwa wananchi waliowachagua na badala yake wameamua kutengeneza fitina ikiwemo kutumia kivuli cha udini.
"…Taifa limekosa mwelekeo kutokana na pepo mbaya ambaye ameanzia juu hali inayoashiria kuwa wanasiasa wameshindwa hivyo inahitajika nguvu ya viongozi wa dini kutushika mkono wanasiasa na kutuonyesha njia sahihi," alisema na kuwaongoza waamini kuchangia sh milioni 22 zitakazotumika kuwafungulia chuo cha ufundi stadi vijana wa Tandale.
Bashe alitoa kauli hiyo juzi jioni katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye uzinduzi wa DVD inayojulikana kwa jina la ‘Muziki wa Injili' iliyoimbwa na Kwaya ya Mbiu ya Kanisa la Wasabato, Tandale.
Aliwaomba viongozi hao kufunga na kuiombea Tanzania ili kuliondoa pepo linalosababisha kuwepo kwa hali ya kutoelewana kati ya viongozi wa juu wa nchi kwa lengo la kuondoa matendo ya kifisadi na udini yanayochochewa na wanasiasa walioshindwa kutimiza wajibu wao.
Bashe alisema kuwa kilichoifanya nchi ifike hapa ilipo ni viongozi walioshindwa kuwajibika kwa wananchi waliowachagua na badala yake wameamua kutengeneza fitina ikiwemo kutumia kivuli cha udini.
"…Taifa limekosa mwelekeo kutokana na pepo mbaya ambaye ameanzia juu hali inayoashiria kuwa wanasiasa wameshindwa hivyo inahitajika nguvu ya viongozi wa dini kutushika mkono wanasiasa na kutuonyesha njia sahihi," alisema na kuwaongoza waamini kuchangia sh milioni 22 zitakazotumika kuwafungulia chuo cha ufundi stadi vijana wa Tandale.