maulaga
JF-Expert Member
- Feb 22, 2009
- 472
- 120
Maelezo marefu ya Bashe juu ya mbunge wake yananipa shida sana.
Majambazi yakizidiana huishia kuuana.
- Kwanini Bashe aliamua kuisaliti nafsi yake na imani yake juu ya UKWELI na sasa kuja kunung'unika hivi?
- Kwanini hukusimamia ukweli tangu mwanzo?
- Bashe alijua fika kwamba mbunge alikwenda mahakamani kwenda kutoa kiapo cha uongo kwanini alijiingiza kumfanyia kampeni mtu muongo na aliye "ruin future" ya mtu mwingine?
- Bashe alijua hata utata wa elimu ya mbunge wake, alijua mikakati mibovu ya kujinufaisha ya mbunge wake, bado Bashe alifunga macho nakuendelea kumkampenia mtu huyo, sasa Bashe anaitoa wapi 'moral authority' ya kumsuta Hamis Kigwangalah?
Majambazi yakizidiana huishia kuuana.