MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe aliyeteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo amemshukuru Rais John Magufuli kwa kumteua kushika nafasi hiyo na kueleza kuwa atahakikisha anakuwa msaidizi mwema wa Waziri Japhet Hasunga ili kuhakikisha sekta hiyo inasonga mbele.
Bashe amesema hayo leo jijini Dar es Salaam, “Mimi niseme tu kwanza nimshukuru Rais kwa imani yake kwangu ambayo amenipa, kwa jukumu langu nimepewa kwenda kumsaidia Waziri Japhet Hasunga, kwenda kuhakikisha tunafikia malengo na matamanio ya Watanzania”.
Bashe amesema, “Hii ndiyo sekta iliyoajiri Watanzania wengi, inaendesha uchumi wa nchini inachangia asilimia 28 ya GDP na asilimia 70 ya ajira lakini ina changamoto nyingi, nina amini katika ushirikiano tutafanikiwa”