BASATA yamfutia Usajili Msanii Dudubaya kwa kukataa wito wake

Mm namsubiria NAY WA MITEGO na ROMA watoe wimbo mpya unaohusu tukio hili la dudu na basata yake.
Nakaa benchi nawasubiria makamanda wangu wajilipue studio watupe tunachopenda kusikia watu wao:D:p
 
Screenshot_20200107-131057.png

Nigga with balls of steel
 
Dudu Baya hana cha kupoteza kwasababu Muziki wenyewe alishamaliza zamani sana.
 
Dudu hadi anafungiwa hakuwa tena mwanamziki... alikua mtukanaji mwenye matusi hadi kero
 
Baraza la sanaa limemfutia msanii Godfrey Tumaini "Dudubaya" leseni, kwahiyo hatakiwi kujihusisha tena na muziki. Mwanzoni msanii huyo alitoa kashfa tofauti kwa kutumia clips za video kwenye Instagram, sababu za kufungiwa ni pamoja na kutoa matusi, na Baraza la Sanaa lilipomwita alisema hataenda kuwasikiliza.

********

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfutia usajili Msanii wa Muziki, Godfrey Tumaini maarufu Dudu Baya kutojishughulisha na shughuli zozote za sanaa kuanzia leo Januari 07, 2020.

Baraza hilo limeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Msanii huyo kukiuka wito wa kutakiwa kufika BASATA baada ya kutoa lugha zisizo na maadili kuhusu Wasanii katika Mitandao ya Kijamii.

Inaelezwa kuwa Dudu Baya alisema ameuona wito huo na hatakwenda huku akilitaka Baraza hilo kutatua migororo iliyopo kati ya baadhi ya vyombo vya habari na Wasanii ili muziki usonge mbele.

Itakumbukwa kuwa Februari 27, 2019, Dudu Baya alikamatwa na kuhojiwa na Polisi ikiwa ni agizo la Waziri wa Sanaa, Harrison Mwakyembe baada ya kusambaa kwa video zake akionekana kumdhihaki Ruge Mutahaba.

Mtu mwenyewe anaitwa dudu baya .
La nini sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ulitaka apewe haki ipi wkt ameitwa na Basata akagoma kwenda?
Viongozi wetu hawana dispute resolution skills, wamekalia mabavu tu na kujimwambafy. Obviously kama umeona unaonewa na kwakua vyombo vyetu havitoagi haki bali vinaangali ni namna gani vitapata mkate wao wa kila siku kwa jusifu na kuabudu ndio maana hakuona umuhimu wa kwenda.

Sent using Jamii Forums mobile app

dodge
 
Back
Top Bottom