Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,426
- 18,228
Baraza la sanaa limemfutia msanii Godfrey Tumaini "Dudubaya" leseni, kwahiyo hatakiwi kujihusisha tena na muziki. Mwanzoni msanii huyo alitoa kashfa tofauti kwa kutumia clips za video kwenye Instagram, sababu za kufungiwa ni pamoja na kutoa matusi, na Baraza la Sanaa lilipomwita alisema hataenda kuwasikiliza.
********
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfutia usajili Msanii wa Muziki, Godfrey Tumaini maarufu Dudu Baya kutojishughulisha na shughuli zozote za sanaa kuanzia leo Januari 07, 2020.
Baraza hilo limeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Msanii huyo kukiuka wito wa kutakiwa kufika BASATA baada ya kutoa lugha zisizo na maadili kuhusu Wasanii katika Mitandao ya Kijamii.
Inaelezwa kuwa Dudu Baya alisema ameuona wito huo na hatakwenda huku akilitaka Baraza hilo kutatua migororo iliyopo kati ya baadhi ya vyombo vya habari na Wasanii ili muziki usonge mbele.
Itakumbukwa kuwa Februari 27, 2019, Dudu Baya alikamatwa na kuhojiwa na Polisi ikiwa ni agizo la Waziri wa Sanaa, Harrison Mwakyembe baada ya kusambaa kwa video zake akionekana kumdhihaki Ruge Mutahaba.
********
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfutia usajili Msanii wa Muziki, Godfrey Tumaini maarufu Dudu Baya kutojishughulisha na shughuli zozote za sanaa kuanzia leo Januari 07, 2020.
Baraza hilo limeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Msanii huyo kukiuka wito wa kutakiwa kufika BASATA baada ya kutoa lugha zisizo na maadili kuhusu Wasanii katika Mitandao ya Kijamii.
Inaelezwa kuwa Dudu Baya alisema ameuona wito huo na hatakwenda huku akilitaka Baraza hilo kutatua migororo iliyopo kati ya baadhi ya vyombo vya habari na Wasanii ili muziki usonge mbele.
Itakumbukwa kuwa Februari 27, 2019, Dudu Baya alikamatwa na kuhojiwa na Polisi ikiwa ni agizo la Waziri wa Sanaa, Harrison Mwakyembe baada ya kusambaa kwa video zake akionekana kumdhihaki Ruge Mutahaba.