BASATA: Shughuli za wasanii hazijaruhusiwa kwa sababu ya janga la ugonjwa wa Corona

Cannabis

JF-Expert Member
Jan 20, 2014
8,933
25,268
Katibu Mtendaji anawakumbusha Wasanii na wadau wote wa Sanaa kuwa shughuli za Sanaa bado hazijaruhusiwa rasmi kuendelea kufanyika kutokana na janga la ugonjwa wa CORONA.

Amesema hayo huku wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam wakijiandaa na sherehe za kuiaga Corona nchini Tanzania zitakazoambatana na upigaji wa mziki.
 
Aiseee hii jumapili ya kesho tayari nimeanza kuichagiza na jibapa langu mdogomdogo
 
Mbona wanatchanganya sasa? Bashite kasema tunywe tupige kelele twende bar,tufanye sherehe kwamba tumeishinda corona19 sasa sherehe utafanyaje bila kupiga mziki au kuwa na wasanii kupiga muziki live? Haujaona KTN wameshatangaza kwamba tanzania tarehe 24 ni Covid Party?
 
Hahaha Dr.Ndugulile alianza hivi hivi tukasikia kapigwa chini, huyo wa basata asome nyakati, covid-19 haipo Tanzania ndio wimbo unaoimbwa na vipenzi wa muheshimiwa rais.
 
Back
Top Bottom