valid statement
JF-Expert Member
- Sep 18, 2011
- 2,851
- 868
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA), limewaagiza viongozi wa mashirikisho ya sanaa hapa nchini kufuatilia kwa karibu matukio ya ukiukwaji wa maadili yanayoendelea katika sekta hiyo hivi sasa na kuchukua hatua kwa wanaobainika kufanya hivyo. Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego, mbali na kuwakemea vikali wasanii wanaotumia majukwaa kwa kuidhalilisha sanaa, wao wenyewe na watazamaji, pia limeyataka mshirikisho kushirikiana na vyama vyao, kuwaita wale wote watakaohusika na uvunjwaji wa maadili ili kuwakanya katika hatua ya kwanza na kama wasipoacha tabia hizo, Baraza litawafungia kujishughulisha na kazi ya sanaa hapa nchini. Shirikisho la Muziki tumeliagiza kuangalia tungo za wanamuziki zenye maneno yenye lugha isiyofaa, Shirikisho la Sanaa za Ufundi limeagizwa kuwachukulia hatua wasanii wachoraji na wachongaji wanaotengeneza sanaa zinazokiuka maadili. Aidha Shirikisho la Sanaa za Maonyesho waliagizwa kufuatilia wasanii wote wanaocheza bila staha majukwaani. Na mwisho Shirikisho la Filamu tumeliagiza kuwaita, kuwaonya na kuwachukulia hatua wasanii wote katika fani hiyo wanaovaa nusu utupu bila kuzingatia uhusika katika kazi za sanaa, alisema Ghonche. Aidha, alisema Baraza limewaagiza wamiliki wa kumbi zote za burudani, kuzingatia maadili pale ambapo sanaa zitakuwepo jukwaani na kwamba, hawatasita kuufungia ukumbi wowote utakaokiuka agizo hilo. Pia tunaviomba vyombo vya usalama, kuhakiki muda wa vibali vya maonyesho na bila kuchelewa kuwachukulia hatua stahiki wasiozingatia muda wa maonyesho. Na tunawakumbusha wamiliki wa vyombo vya habari na wahariri, kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wasimamizi wa sanaa kwa kutokurusha wala kutangaza maonyesho ambayo kwa njia yoyote yanachangia mmomonyoko wa maadili ya taifa letu. Kwa suala hili, Baraza linaziomba mamlaka zinazohusika na usimamizi wa uendeshaji wa vyombo vya habari nchini, kuingilia kati na kuvichukulia hatua vyombo vya habari ambavyo kila siku vimekuwa mstari wa mbele kueneza wimbi la mmomonyoko wa maadili hapa nchini na kushusha hadhi ya tasnia/sekta ya sanaa nchini, alisema Ghonche. Hivi karibuni, kumekuwepo na malalamiko kuhusiana na tamasha moja linaloendelea hivi sasa hapa nchini, ambako wasanii wa filamu maarufu kama Bongo Movie wamekuwa wakipanda jukwaani wakinengua huku sehemu kubwa za miili yao ikiwa utupu, huku BASATA ikiwa kimya. SOURCE: GAZETI TANZANIA DAIMA Hivi ukishakuwa supastaa wa kike hapa Tanzania ni lazima uwe unavaa nusu uchi kila wakati? Wakicheza izo filamu zao wanavaa vimini hata kama wanaigiza maisha ya kijijini, wakiwa kwenye intavyuu kwenye luninga, wanagonga vimini, wakiwa jukwaani kwenye disko/tamasha ndo kabisaa wanakufuru na vimini vyao. Hebu BASATA na waanze na wacheza shoo katika mabendi hawa wanaovaa boxa na kucheza jukwaani! Leo ni ijumaa tunajua kabisa watapanda nusu uchi kama kawaida yao, BASATA wawajibishe hizo kumbi za starehe tuone kuwa wako makini.