Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,545
Mpendwa mwanafunzi,
Natumaini kuwa u buheri wa afya, na ni imani yangu kuwa unaendelea vizuri na masomo yako. Kama unaokumbana na changamoto kitaaluma na kijamii pole sana, naomba Mungu akupiganie.
Leo sina mengi sana, ila naomba nikukumbushe tu ile hela unayopewa na serikali yako ya kujikimu (malazi na chakula) itumie vizuri. Jibane kadri uwezavyo ili badae usijekutulaumu.
Najua unajua hali iliyopo sasa nchini, kama hauna konekisheni, ajira utaisikia tu kwenye redio na kuiona kwenye runinga.
Wenzako waliotunza huo mkopo, sasa angalau wamejiajiri, wapo wanachoma mahindi, wapo wanashona nguo, wapo wanauza nguo za mtumba, n.k.
Hata mimi najua, unasoma kozi za sayansi, ila nachokuambia ni ukweli mtupu. Kama huamini, nenda, Uhuru sekondari skuli, yenye wanafunzi 1000 na kidogo ila ina mwalimu mmoja wa baiolojia. Au nenda kituo cha afya cha Tanzania Mpya, chenye majengo mapya manne lakini kina wauguzi wawili tu na daktari mmoja mwenye dispensary yake.
Sawa, we kama utajitolea JKT ni juu yako, ila kumbuka kuna watu walijitolea, leo tupo nao mtaani tunaangaika nao kulisukuma tairi la maisha.
Usidhani, Clara na Johnson walibahatisha, naomba ukumbuke kuwa mjomba wao ni Kanali wa Jeshi. Na yule Sophia alipewa kazi kwa sababu like shirika la dhehebu lake la Wasabato.
Najua una GPA ya 4.2 ila si unamkumbuka Jakob mtoto wa mzee Isaka? Achana na Jakobo kada wa chama, yule mwenye gari na nyumba nzuri. Namzungumzia Jakob kichwa, yule dogo aliyekuwa kichwa toka primary, dgo ana 4.5 ya UDSM ila siku hizi anahudumia kwenye mgahawa wa shangazi yake.
At least wewe ni Mhaya, kidogo unaweza pata nafasi pale St. Shomile Schools, ila usipategemee sana maana hali haitabiriki.
Mi mwenyewe, vyeti vyangu ni A',s na nina uwezo mzuri wa ufanisi, ila ndio hivyo, niliokuwa nawafundisha chuoni, wameajiriwa, yule Ruth, girlfriend wangu na yy ameajiriwa na yule jamaa niliyemfumaga nae amasema ni kaka yake.
Najua hujui kuhusu Hussein yule mwenye shahada ya sheria ya UDSM, yupo anarusha miziki. Yule John engineer wa St. Joseph yupo stationary ya Venny anatoa copy.
Ila nashukru Mungu nimepata nafasi ya kujitolea hpa nalipwa 60,000 kwa mwezi. Na chai ya asubuhi napewa.
Halafu naomba kama una kabalance kidogo unitumie mdgo wangu, nifate cheti changu chuoni, niombe scholarship ulaya.
Wako,
ALUMNI
Sent using Jamii Forums mobile app
Natumaini kuwa u buheri wa afya, na ni imani yangu kuwa unaendelea vizuri na masomo yako. Kama unaokumbana na changamoto kitaaluma na kijamii pole sana, naomba Mungu akupiganie.
Leo sina mengi sana, ila naomba nikukumbushe tu ile hela unayopewa na serikali yako ya kujikimu (malazi na chakula) itumie vizuri. Jibane kadri uwezavyo ili badae usijekutulaumu.
Najua unajua hali iliyopo sasa nchini, kama hauna konekisheni, ajira utaisikia tu kwenye redio na kuiona kwenye runinga.
Wenzako waliotunza huo mkopo, sasa angalau wamejiajiri, wapo wanachoma mahindi, wapo wanashona nguo, wapo wanauza nguo za mtumba, n.k.
Hata mimi najua, unasoma kozi za sayansi, ila nachokuambia ni ukweli mtupu. Kama huamini, nenda, Uhuru sekondari skuli, yenye wanafunzi 1000 na kidogo ila ina mwalimu mmoja wa baiolojia. Au nenda kituo cha afya cha Tanzania Mpya, chenye majengo mapya manne lakini kina wauguzi wawili tu na daktari mmoja mwenye dispensary yake.
Sawa, we kama utajitolea JKT ni juu yako, ila kumbuka kuna watu walijitolea, leo tupo nao mtaani tunaangaika nao kulisukuma tairi la maisha.
Usidhani, Clara na Johnson walibahatisha, naomba ukumbuke kuwa mjomba wao ni Kanali wa Jeshi. Na yule Sophia alipewa kazi kwa sababu like shirika la dhehebu lake la Wasabato.
Najua una GPA ya 4.2 ila si unamkumbuka Jakob mtoto wa mzee Isaka? Achana na Jakobo kada wa chama, yule mwenye gari na nyumba nzuri. Namzungumzia Jakob kichwa, yule dogo aliyekuwa kichwa toka primary, dgo ana 4.5 ya UDSM ila siku hizi anahudumia kwenye mgahawa wa shangazi yake.
At least wewe ni Mhaya, kidogo unaweza pata nafasi pale St. Shomile Schools, ila usipategemee sana maana hali haitabiriki.
Mi mwenyewe, vyeti vyangu ni A',s na nina uwezo mzuri wa ufanisi, ila ndio hivyo, niliokuwa nawafundisha chuoni, wameajiriwa, yule Ruth, girlfriend wangu na yy ameajiriwa na yule jamaa niliyemfumaga nae amasema ni kaka yake.
Najua hujui kuhusu Hussein yule mwenye shahada ya sheria ya UDSM, yupo anarusha miziki. Yule John engineer wa St. Joseph yupo stationary ya Venny anatoa copy.
Ila nashukru Mungu nimepata nafasi ya kujitolea hpa nalipwa 60,000 kwa mwezi. Na chai ya asubuhi napewa.
Halafu naomba kama una kabalance kidogo unitumie mdgo wangu, nifate cheti changu chuoni, niombe scholarship ulaya.
Wako,
ALUMNI
Sent using Jamii Forums mobile app