BARUA YA WAZI YA RAIS WATU MPENDWA Jakaya M. Kikwete

Kachanchabuseta

JF-Expert Member
Mar 8, 2010
7,269
675
WanaJf sijui kama hii barua ilishakuja hapa maana katika pitapita zangu nimekumbana na hii barua labda ilishamfikia Rais wetu mpendwa, Kama ilishakuja hapa Mod atanisadia Source:Google



(1) Kundi la maskini Walipa kodi wa Tanzania (95% ya Watanzania). Hawa wenye kipato kilicho chini ya dola moja kwa siku, wakimemo wakulima na wafanyakazi wengi serikalini (>80%) wanaolipwa chini ya Tsh 450000/- kwa mwezi wakiwamo Walimu wa shule za msingi na sekondari. Kwa bahati mbaya zaidi, hawa ndio waliokupigia kura. Katika kundi hili wamo walala hoi waliochini ya msatali wa umasikini (poverty line) pia wapo walio kwenye umaskini wa kutupwa (abject line). Wapo ambao wanafia majumbani kwa kukosa fedha ya usafiri wa Tsh 500/- za kwenda hospitalini, wapo wanaofia mlangoni (reception corridor) kwa kukosa ada ya kumwonaBARUA YA WAZI KWA RAIS JAKAYA KIKWETE
Ndugu jakaya kikwete napenda kukueleza kuwa unaipeleka nchi kubaya. Umeigawa nchi katika makundi haya:


Daktari hospitalini , wapo wanaofia hospitalini –wodini kwa kukosa kumhonga nesi ama daktari ili atoe dawa. Na mbaya zaidi wewe unaishi angani kama mwewe. Hapa rais unaandaa taratibu na kwa uhakika uvujaji wa amani wa taifa hili, kwani wananchi wameshaanza kuonyesha kupotea kwa uvumilivu kwa kuona RASILIMALI ZA TAIFA HILI ZINATUMIWA NA WATU WACHACHE (5%) HUKU WAKIFAHAMU KUWA WANASTAHILI KUFAIDIKA NA RASILIMALI HIZO KAMA WATANZANIA. Rais wangu, hakuna Mtanzania bora zaidi.Kundi hili watoto wao wanasoma katika shule za YEBO YEBO ZINAZOENDESHWA NA WAALIMU YEBO YEBO..Kundi hili kuna wazazi ama walezi ambao watoto wao wameshindwa kulipa ada za sekondari ama uchangiaji wa masomo ya chuo kikuu, huku kundi lako (la watu 5%) watoto wao wakisoma katika shule za kimataifa ama nje ya nchi. Chuki hii unayoichonga ni mbaya kuliko kipindupindu. Iko siku italipuka. Nakuomba uondoe ubaguzi huu jinnai


(2) Kundi la UDINI. Inasikitisha rais wangu kujikita katika propaganda za kuanzisha matabaka ya kidini.Mara nyingi umekuwa mpiga debe wa udini kwa kasi kubwa. Kwa mfano umelivalia njuga kwa kasi kubwa zaidi na kwa mwendo mkali . Umekuwa ukiwaahidi Waislamu unapokutana kuwa utafanikisha MAHAKAMA YA KADHI katika taifa linaloongozwa na katiakisiyo ya udini ama kikundi Fulani tu chenye itikadi isiyoyo lingana na katiba ya nchi.
Rais wangu kama unajua , Mila (culture ) imeundwa na vitu kama elimu (education), sanaa (arts) ufundi (crats), desturi (customs), utamaduni (traditions), dini (religion),, itikadi (ideology) na lugha (language). Hivi vyote kwa taifa letu viko chini ya katiba ya nchi vikipewa usawa linganifu. Hakuna kiungo (component of culture ) kilichobora zaidi, vote vinatumika kujenga umoja wa kitaifa. Taifa letu kikatiba si la kidini (rejea ilani ukurasa wa 8).. Kumbuka kuwa dini ni kiungo kimoja kati ya component 7 za mila (culture), iweje kakiungo kamoja kwenye dini (uislamu) kajione bora kuliko viungo vingine vya dini (ukristo, uhindu, ubudha, dini asili)????????!!!!!!?.
Hoja zinazijengwa na baadhi ya waislam wanadai kua
(a) Vatican ian ubalozi hapa nchini na hali ya papa wa Roman Catholic. Vatican City ni taifa Huru kabisa . Papa ni rais wan chi ya Vatican City . Hivyo anakuwa halali kufanya MAHUSIANO YA KIDIPLOMACIA NA TAIFA LOLOTE DUNIANI.. Ndiyo maana ana ubalozi katika nchi zaidi ya 190 duniani, zikiwemo zenye itikadi ya Kiislam, Kihinfu, Kibudha, Kikomunisti zisizotambua kuwa kuna Mungu.. Kinachochanganya watu ni kwamba serikali ya vatican ni complex, kwani papa ni rais na kwa kofia nyingine ni kioncozi wa Kanisa katol;iki duniani. Anapotembelea nchi Fulani huwa anatangaza sera za kisias na mahusiano ya kimataifa , ikiwemo kutangaza na kutetea haki za binadamu kama ilivyobainishwa katika Azimio la Haki za Binadamu. Ndiya maana hivi karibuni papa alitembelea nchi za Kikomunist na Kiislam, hapo alikuwa hatangazi Ukatoliki bali alikuwa kwenye kofia yake ya uraisi akinadi mahusiano ya kimataifa ikiwa pamoja na kukemea ufisadi na rushwa iliyokithiri ulimwenguni (rejea Tanzania). Kwa hiyo kusema Vatican ina ubalozi Tanzania huwa ni ufinyu wa hoja elimu ya Mahusiano ya kimataifa kwa mtoa hoja. Narudia kuwa Vatican ni taifa huru. Na kama vile yalivyo mataifa yanayoongozwa na serikali ya dini ya kidini(Kiislam) kama vile Saudia, Oman, Iran , yanapokuwa na ubalozi Uinngereza, Ujeruman, Uswizi n.k. huwa ni juu ya mahusiano ya kimataifa sio kusaidia kueneza uislamu.
(b) Hoja ya uislamu kutetea mirathi na ndoa kwa taratibu ya kiisalam ni jambo ambalo linatrakiwa walifanye kidini (as a sub- component of culture ), sio kwamba waiweke kwenye katiba ya nchi isiyofuata misingi ya kidini kama Tanzania.. Hii rais wangu italeta uvunjani wa katiba ya nchi na mahisiano ya kitaifa. Nasema hivyo kwa sababu kila dini na kila dhehebu lina itikadi zake. Kwa hiyo kuruhu taratibu za dhehebu Fulani la dini liingizwe kwenye katiba na ghalama za nchi ni kukosa busara na hekima. Ina maana kwamba kila dini ama dhehebu lina taratibu zake , kwa mfano:
(i) Wakristo wengi wanasistizia ndoa kwa misingi kuwa mtu akioa mke wa pili ama wa tatu ama wa nne anakuwa amewekwa kwenye kundi la uzinzi, na anatakiwa ashughulikiwe kidini. Je hili nalo wakristo wadai MAHAKAMA YA WWH(WATEULE WENYE HAKI). TUTAFIKA?
(ii) Wakristo wanadai mirathi igawiwe sawa kwa watoto wote, wa kike na wa kiume kwa kufuata maagizo ya Mungu wao Muumba wa mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo. Je hili nalo waliundie mahakama ya WWH?
(iv) Wakristo wa dhehebu la Wadventisata Wasabato wanadai suala ibada ni Jumamosi (siku ya saba ya wiki), Pia wanasema kambale, nguruwe, sungura, mbweha , fisi, wameharamihwa , Je ili kufanikisha hoja hizo, nao wanahitaji wadai kuwa na mahakama ya WWH?

(v) Wakatoliki wa Roma kwa suara la ndoa ni kwamba kijana wa kiume akitaka kuwa padri hatakiwi kuoa, vile vile binti akitaka kuwa SISTA (SISTER) hatakiwi kuolewa. Lakini kuna baadhi ya vijana wa kike na kiume huwa wanashindwa kutimiza masharti hayo, je hili nalo liundiwe mahakama ya WWH?
(vi) Wakristo wote wana kanuni ya ndoa kuwa watu wakioana hawatakiwi kupeana taraka mpaka watenganishwe na mauti. Lakini wengine wanandoa wengine hukosana na kufikia kudaiana talaka. Je hili nalo liundiwe mahakama ya WWH?
(Vvii)Wanadai kuwa Uganda in mahakama ya Kadhi!!, hivi hawajui kuwa nchi hiyo ni ya kidikteta. Hayati nduli alikuwa diktete, Mseveni ni Dikteta la kutupwa. Hivyo mambo hayo hayakufuata haki za binadamu. Taifa hili sio la kidikteta ingawaje taratibu sasa limeokota 45% ya kuwa tiara la kidiktera. Ukisoma kisaikolojia jinsi unavyotetea MAFISADI NA UFISADI utajua kuwa unalipeleka kubaya taifa, maana unakuwa component ufisadi. Rejea ulivyo liingiza taifa kwenye ufisadi na utapeli wa IPTL.!!!!!.
Kwa hiyo mahakama ya kadhi si lolote wala si chochote bali ni ubaguzi wa kidioni, hali ya kakundi Fulani ka dini kujiona kana ubora zaidi kuliko vikundi vingine .Kakundi hako kanafikia kudai kuingizwa kwenye matumizi za kodi za raia wote. Ni ajabu ya Abunuasi kama siyo ya Karumekenge.

3. Kundi la matajiri-mafisadi wanaoishi kama wako peponi chini ya ulinzi na utetezi wako.Watoto wao wanasoma shule za kimataifa nje ya nchi, wako kwenye sekta muhimu (nyeti hata kama hawana uwezo wa kufanya kazi , watoto wao,wakibaki kusomea nchinihupewa 100% ya mkopo utolewao na bodi ya mkopo. Mafisadi hawa wameshika sehemu kubwa kubwa serikalini ama kuwa na biashara haramishi. Wengine wamejificha bungeni, kwenye viti vya ukatibu kwenye mawizara, kwenye uwaziri. Cha kusikitisha zaidi , watu wanafahamu kuwa unawalinda kwa nguvu zote zikiwamo za dola. Rais wangu , kumbuka kuwa BWANA WA MAJESHI , MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA NI MUNGU WA MBINGUNI. Ammekupatia kiti utende haki. Utetee maskini, wanyonge na wahitaji wa taifa hili. Kinyume cha hayo UNAFANYA VITA NA BWANA WA MAJESHI. SIJUI MSHINDI ATAKUWA NI NANI. Umekuwa kibaraka wa Mafisadi . MUFILISI HAO NI HAWA:

(a) A..F. Magoma Mhasibu feki SUA (kalipotezea taifa zadi ya Tsh millioni 21,532,000,000/-kati ya mwaka 1995 na 2009
(b) PROFESA PETER MSOLLA(WST)- Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh 30,569,176,000 tangu akiwa SUA hadi leo
(c) JUMA NGASONGWA-Alilipotezea taifa hili zaidi ya Tsh billioni 45 kwa kuuza wanyama pori
(d) Ndugu KAPUYA-Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh 35 billioni miradi ya madini(nzega na Arusha) na bendi yake aliyoidanganya ya jeshi
(e) Mwangunga –kalipotezea taifa zaidi ya Tsh 125 billion (Mali asili na Utalii)
(f) ROSTAM AZIZI--Kalipotezea taifa hili zaidi ya Tsh 546.7 billion kupitia EPA ya BOT, UBIA FISADISHI NA JAPAN, pia kupitia makampuni fisadishi manane
(g) MEGHDI-Alilifirisi taifa zaidi ya Tsh billion 20 kwa vitalu vya uwindaji haramu vya wanyama pori na Tsh za EPA/BOT zaidi ya Billion Tsh 133
(h) KINGUNGE NGOMBALEMWILO-Huyu amelipotezea taifa hili zaidi ya Tsh 980 billion kupitia kampuni yake ya ulinzi jijini na stand ya Ubungo terminal kwa kukwepa kulipa ushuru halisi
(i) ABDALLAH KIGODA-Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh 6.1 trillion kwa sakata la MIKATABA MIBOVU YA MADINI, UUZAJI FISADISHI WA MASHIRIKA YA UMMA, NA SAKATA LA GLOBOLISATION AMBAO ALIUFANYA KAMA KIFUNGUA KICNYWA..
(ib) Yona , kalipotezea taifa ya Tsh Trillion 5.9 kwa kipindi chake akiwa na na Mkapa kupitia sakata la rada,EPA,, KIWIRA, mikataba mibovu ya madini. Cha ajbu ni kwamba hizi kesi zilizofunguliwa dhidi ya mafisadi tumeshagundua ni na usani tu ili uwadanganye nchi waone kuwa uko serious na ufisadi at the moment wakupatie fedha za kuishi angani ama kuwaenzishia mafisadi wanaoitafuna nchi yetu


(j) Edward Hosea (TAKUKURU- Taasis ya kukuza na kurutubisha rushwa)
Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh billion 298.2 kupitia kulinda RICHMOND, EPA (BOT), kuharalisha vitalu haramu vya uvunaji wanyama pori,kupitisha mikataba feki kama ya TICS, TRL, MIKATABA MIBOVU YA MADINI PAMOJA NA MADUDU MENGINE MENGI.
(k) ANDREW CHENGE-Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh trillion 133.7 kupitia yafuatayo> EPA, RADA FEKI, NDEGE FEKI YA RAIS, MIKATABA MIBOVU YA MADINI, UUZWAJI TUPATUPA WA MASHIRIKA YA UMMA, UFICHAJI FEDHA NJE YA NCHI, KULA RUSHWA NZITO NZITO KWA MATAPELI WA KIHINDI N.K.
(l) Karamagi-amelipotezea taifa zaidi ya Tsh 9,824,000,000 Kwa ufisadi wa RICHMOND, DOWANS na TICS akiwa. TICS ni wazi KATUMEKENGE amejifichamo
(m) E. Lowassa-Amelipotezea taifa zaidi ya Tsh 1,824,000,000 Kwa mwaka wake wa RICHMOND
(n) Msabaha-Amelipotezea taifa zaidi ya Tsh 1,824,000,000 Kwa mwaka wake wa RICHMOND
(o) MASHA,-wizara ya wizi wa ndani-Amelipotezea taifa zaidi ya Tsh billion 458.7 kwa kampuni yake inayodaiwa ni kampuni ya jeshi la wana na sakata la vitambulisho fisdadishi vya taifa
(p) Pro/ MAGHEMBE-Amelipotezea taifa zaidi ya Tsh 130,000,000/- kwa kulea wauzaji wa mitihani ya NECTA na uuzaji wa vyeti bandia. Pia ameamua kujenga taifa la mazezeta kwa kuachia mitihani iliyovuja kutahini wanafunzi. He could the most dangerous figure in our national.).
(q) WILLIAM NGEREJA:-Ameeendela kulipotezea taifa Tsh 35,561,602,550/-Kwa mwaka kupitia kukumbatia ufisadi wa mikataba mibovu ya madini, utapeli wa vigogo wa TANESCO, DOWANS, IPTL, APR, KIWIRA POWER RESOURCE, SONGAS n.k.
(r) BENJAMINI MKAPA-Kalipotezea taifa zaidi ya Tsh Trillion 98.5 kwa miaka yake akiwa ikulu kwa miaka 10 (1995-2005) kwa kupitia uanzishaji wa EPA,, Kampuni zake (ANGEN, fosnik, TANPOWER,) Ndege feki ya rais, RADA, utupaji wa mashirika ya umma, kushiriki mikataba mibovu ya madini kwa masrahi yake binafsi,kuweka rais pandikizi-karumekenge, kuendelea kuienzi kampuni angamizi ya ITPL
(s) WASIRA-Waziri wa kilimo na chakula. -Alikiua kilimo tangu miaka ya sitini kwa kujali maslahi yake binafsi. Ikiwemo kula fedha ya mbolea ya ruzuku waka 2008. Sasa amekiua kilimo kwa kusambaza mbolea angamizi ya MINJINGU ambayo amesababisha loss ya Tsh billion 378 kwa kuua mazao ya Mahindi,maharage na viazi mviringo mwaka 2008
(t) MWANYIKA , MWANASHERIA MKUU TANZANIA,-Amekomba zaidi ya billioni 987 kwa kupokea rushwa nene na kutoa taarifa feki kwenye uchunguzi wa RICHMOND , sakata la Buzwagi, mikataba mibovu ya madini, sakata na hujuma za wahindi kupanga kwenye nyumba nzuri za National Housing kuliko wazawa, Sakata la DOWANS na hujuma nyingine nyingi. Ni fisadi anayetakiwa ajiuzuru mara moja.. Pia lilikuwa kwenye kamati ya kuchunguza wizi wa fedha za BOT (kupitia EPA), Je fisi anaweza kumchunguza fisi mwezie au kujihukumu mwenyewe? NEVER!!!!. Hiyo ni danganya toto
(u) SHUKRURU KAWAMBWA- Waziri Wizara zisizoelewka. Ametumikia wizara nne kwa muda wa miaka miwili na nusu na kila alipopita ameboronga 100%. Mfano , akiwa Wizara ya mifugo alisababisha upotevu wa zaidi ya Tsh million 1235 kwa kuzembea kuzuia makongamano,washa na semina mufilisi zilizokuwa zinafanyika kwenye gorofa ya 10 ama 12 Dar kumjadili mfugaji na mifugo yake huko Ihefu, Mara, Shinyanga, Mwanza, Tabora, Dodoma, Singida, Babati kijijini nk . Pia alishindwa kudhibiti safari za vigogo Wizarani (makatibu na kurugenzi)zisizo na tija za kwenda Ulaya na baadhi ya nchi zilizoendeleza mifugo Afrika kama vile Botswan, Africa kusini. Kwenye wizara zingine nako Kawambwa kawambwa kweli, maana ameshindwa kabisa, huku akilindwa na mjomba wake (Karumekenge-JK).Rais hatuiendeshi nchi kwa ujomba.
(v) VIGOGO WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI- Wizara hii imeoza mpaka kwenye visigino tukisema imeoza hadi kichwani tutakosea. Hebu fikiria , Botswana ina ng'ombe millioni tatu na nusu , lakini inaingiza pato la taifa kiasi cha 80% GDP. Tanzania ina ng'ombe 18.5 million, lakini inaingiza pato la taifa kwa asilimia 4.9% tu. Hivi pinda huoni kuwa hapo panahitaji kusambaratishwa na kuundwa upya. Kumtoa Diallo peke yake haikutosha, mimi nachukulia kuwa ilikuwa chuki ya kibinafsi kati ya diallo na bosi wako. Maana aliacha mapapa yanayotafunafedha za walipa kodi kwa kudai wanatuma mamia ya millioni kila mwaka kudai zinakwenda kuboresha sherehe kama vile (a)maonyesho ya nane nane (b)wiki za maziwa (c)maonyesho ya sabasaba (d) Safari za nje ya nchi za makatibu wakuu. Kurugenzi, na marafiki wa vigogo hao waliopo wizarani. Zote Nasema kuwa safarSafari hizo zote matunda yake ni ziro kama sio kwenda kupata mitaji haramu na material fisadishi. Kwani mifugo na mfugaji mwenyewe wamebaki vile vile kama miaka ya 1820 AD. Sehemu zingine ambazo zinatafuna fedha ni makongamano, washa na seminar zailizoanza tangu miaka ya 60 lakini hadi leo mifugo imebaki hafifu isiyokidhi soko la nje. Wafugaji wamekuwa wakimbizi ndani ya nchi yao , wakifukuzwa kila wanapokwenda bila kutengewa eneo maalumu.?. Ihefu?, Kilombero?, Kilosa?) na kuhamishiwa kwenyhe kanda za ndolobo kama vile Lindi ili mifugo yetu isiweze kuwa na thamani ya soko la nje. Ndugu pinda anayajua haya na bosi wake Karumekenge. Lakini kutokana na ufinyu wa akili zao, wameshindwa kuivunja wizara hiyo ama kuiweka chini ya WIZARA YA ULINZI, yaani iwe "WIZARA YA ULINZI NA MAENDELEO YA MIFUGO", na kuwang'oa VINGUNGE WALIOPO HAPO KWA NAFASI ZA UKATIBU MKUU AMA KURUGENZI FISADISHI. Hapo ndipo Mifugo ingezalisha pato linaloeleweka.. Lakini Pinda akipelekewa matatizo hayo ANASHANGAA SHANGAA TU HUKU Bosi wake akiyasikia hayo anacheeeeekaaaa kama kichaa kaokota tambala chafu jalalani. INATISHA!!!!!!? MASKINI TANZANIA UMEVAMIWA NA VIONGOZI MATAPELI, POLE SANA MTANZANIA!!!!!. Wizara hii ameipiga HATI CHAFU MKAGUZI WA MAHESABU YA TAIFA (CAG), YAANI AMEIPIGA ZIRO. WEWE PINDA HULIONI HILO????. Kwa bahati mbaya zaidi , MAGUFULI AMEFUNGA KUFULI KWENYE MIFUGO, AMEJILKITA KWENYE SAMAKI PEKE YAKE. NILISHANGAA SIKU MOJA KUSIKIA KUWA AMEKAMATA KOKOLO ZA UVUVI HARAMU KWENYE MADIMBWI YA SAMAKI HUKO ARUSHA. JE TUTAFIKA???.


(w) PINDA MIZENGO –WAZIRI MKUU TZ.
Ndugu Pinda, amekuwa akilea mali za mafisadi kama akina Rostam, Vijicenti(ambaye aliwahi kuizidi serikali ya Tanzania Tsh billion 15 mwaka 2008), Jeetu , Karamagi, n.k huku umenyang'anya (i)watanzania masikini fedha yao kwenye DECI kwa kusingizia kuwa taasisi hiyo ilikuwa ya kitapeli. Kina mama ntilie, wasukuma mikokoteni na watumishi kimo cha chini unaowalipa Tsh 80,000/- take home kila mwezi waliwekeza DECI , na serikali yako ikatoa majengo yakiwamo ya CCM, ulinzi wa polisi mpaka leo, Benki kuu ikapokea kodi ya mapato, wakuu wa mikoa 11 (uliowahamishia mikoa mingine hivi karibuni) walihamasisha ufunguzi wa matawi ya DECI, Mkulo alifungua tawi la DECI Gairo (Kilosa baadaye akajidai kukanusha kwani vyombo vya habari ni vyenu) , Pinda akafungua tawi la DECI Mpanda. Baadaye akawageuka maskini hawa kwa kuichukua fedha yao akidai yeye na Mkulo wananusuru fedha ya wananchi maskini kama hao. Leo Pinda na Mkulo wanasema hawahusiki. AU MNAANDAA EPA YA 2010 KWA JASHO LA MASKINI HAWA?. Maskini hawa walijikuta hawana njia ya kujinasua na umaskini iliowajengea serikali kwa takribani miaka 50 tangu tupate uhuru KWA KUNEEMESHA WAGENI MATAPELI WA KIHINDI NA KIARABU, kwani hata fehda yako ya kibabaishaji (Kikwete –Karumekenge) haijulikani iko wapi na inamnufaisha nani. Kama si wake wa vigogo mafisadi wewe unaelewa, maana inawezekana mmechonga EPA YA UCHAGUZI WA MWAKA 2010 kwa Slogan ya mabilioni Tsh 21 ya kibabaishaji . Kikwete na Pinda, nawashauri mwogope na kumheshimu Mungu . Aliwaweka mfanye kazi ya kutetea haki ya watu wote WALA SIO MAFISADI, AMA UDINI (KADHI), AMA WAPENZI WENU, AMA UKABILA AMA UTAIFA(WAHINDI, WAJOMBA.


Rais wangu , ukiweza kutatua angalau .1/8 (0.125) yq matatizo haya kwa kipindi kilichobaki, Utarudisha Imani ya Watanzania inayozidi kupotea kila kukicha







 
hujataja machapisho ya pesa mpya,ambazo hazitumiki kwa sasa na tayari tumepoteza mabilioni ya pesa ktk kuzichapisha
 
Kwa kweli kuhusu machapisho ya pesa ni swala zito. kama kuna mtu yoyote anayefahamu nchi yoyote inayotumia noti za aina mbili tofauti zenye thamani sawa kwa kipindi kimoja atuambie hapa, sijawai kuona hili popote maana mpaka leo hii ATM zetu zinatema zile noti za zamani, hii ina maanisha bado zinaingia kwenye mzunguko. Mbaya zaidi izi noti mpya zimechakaa kuliko noti za zamani.
 
Ahsante, ila siku nyingine unapoandika habari ndefu hivi weka font kubwa kidogo
 
Nzuri, mpangilio rekebisha hata kama umeikopi mahali
 
umeeleza vizuri sana na umegusa sana hisia zangu. Pia natarajia umegusa sana hisia za watu wengi. Pia umeonyesha ni jinsi gani taifa hili linavyorudishwa nyuma na watu wachache,, aidha kwa makusudi ama kwa uelewa mdogo ukilinganisha na mamlaka waliopewa.
Lakini nimepata mashaka kidogo kwa jinsi ulivyolizungumzia suala la dini, kwani pamoja na juhudi zako kubwa za kuweka mambo haya wazi ili wananchi wachukue hatua slahili, ila hapa inawezekana ukakosa uungwaji mkono kwa kuwa kwenye suala la dini kwako uislamu ndio tatizo, na tatizo hilo kwako limekuja kwakuwa rais aliyopo madarakani ni wa dini hiyo. Lakini umesahau yafuatayo.
1. Katika watu uliowataja kwa majina, karibu zaidi ya asilimia 85 ni wakrito, na ni watu tunaowaona wakialikwa ama kushirikishwa kuchangia maendeleo mbali mbali ya dini yao, je wizi wao wa mali ya umma kuna uhusiano wowote na dini yao? Umetaja hapa EL, Chenge, wasira, yona, mkapa, ngereja, pinda, mwanyika, hosea, nk. Mi nadhani utendaji mbaya wa mtu hauhusiani kabisa na dini, rangi, kabila ama mahali anapotoka.
2. Umetoa shutuma kubwa na nzito kwa jk, ila makosa mengi uliyaeleza ni yale ambayo yamefanywa kabla ya kipindi chake. Wakati B.W.M anaongoza hamkuyaeleza haya kwa kuwa labda alikuwa ni wa dini yako, nimesema kwa dini yako ni kutokana na ulivyowasilisha hoja ya udini na ku base upande mmoja. Leo mambo yameharibika ndio mnainua midomo kwasababu aliepo ni mwislamu, hata hivyo historia lazma ituhukumu, wote, waislamu na wakristo wamelifikisha taifa hapa lilipo kwa ubaguzi wetu wa kidini. Na leo hii hakuna kundi lililofaidika na ubaguzi huo.
Kwamfano, unaonekana wewe ni mtu unaejua mambo mengi sana ya nchi hii, lakini unajua zaidi maovu zaidi ya mazuri, kwanini wizi wa pr. Msolwa wa 1995 unatuambia leo baada ya miaka 16? Why? Nyinyi ndio watu hatari sana wa nchi hii, na ndio maadui wetu no 1, kwani inaonyesha ulikuwa unanufaika na mfumo huo na sasa umewekwa pembeni na ndio umeamua kusema haya!,
fafanua haya nitarudi tena ukirudi umeme, kwani umekata na simu haina chaji
 
Back
Top Bottom