akajaseh mbambah
Member
- Jun 11, 2021
- 6
- 1
Kwako Mheshimiwa Rais Samia Suluhu
Salam!
Mimi ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 40 ambaye nimesoma nchini Tanzania kuanzia shule ya Msingi, Sekondari na pia Chuo Kikuu. Elimu yangu kubwa nimeipata kwa watanzania ndani na nje ya Darasa.
Nashukuru katika kuitumikia nchi nimehusika kwa njia moja au nyingine katika kusambaza na kutoa Elimu kwa Watanzania kwa njia mbalimbali. Lakini pia katika hilo nimeweza kupata Elimu toka kwa watanzania mbali mbali pasipo kuhusisha vyeti vyao vya Elimu. Katika Elimu kikubwa ambacho nilijifunza ni kuendelea kujifunza siku zote pasipo kukoma.
Mheshimiwa Rais. Si kawaida katika siasa au jamii yetu mtu kuomba uteuzi kwa namna hii ambayo naitumia kwako. Nimekuwa nikiangalia na kutafakari mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanywa na viongozi vijana wenzangu katika nafasi ambazo wamepewa. Na siku zote nimekuwa nikiumia kuwa pengine kuna tatizo fulani katika uelewa wetu vijana na mambo ya uongozi na wajibu wetu.
Mimi nakuja mbele yako nikiwa pembeni ya watanzania wengi ambao wanaangalia kila kinachotokea na kukitafakari kwa kina. Mh. Rais, naamini kwa yale ambayo nimejifunza katika maisha nikiwa nimeajiriwa na kujiajiri kuna mengi ambayo ningeweza pia yatumia katika kutumikia nchi yangu. Inawezekana kabisa kuna sehemu kama binadamu sikutenda au kunena ilivyopaswa lakini napokaa na kutafakari peke yangu naweza kugundua wapi nilikosea na wapi napaswa kurekebisha au pia kuweka mkazo ikiwa kunaleta matokeo chanya.
Mimi Chama Changu ni Utanzania kwanza. Imani yangu ni Utanzania kwanza na katika hili naamini ninaweza tumika vyema kabisa kwa ajili ya Watanzania kupitia Chama chako cha Mapinduzi. Nikiwa na Kadi ya Chama ya zaidi ya miaka 10. Nimekuwa nikiangalia maslahi ya Watanzania na Utu katika mitizamo yangu, hili naomba niliweke wazi mbele yako. Nikiamini katika Utu Bora, Haki na Wajibu katika kila jambo. Nimekuwa nikiamini matendo mema yanalipa na hali kadhalika matendo maovu yanalipa pasipo kujali Dini, Kabila, Itikadi, Rangi, Umri na Jinsia.
Mh. Rais, Kipekee kabisa naomba nikuombe unipe nafasi ya kuwatumikia Watanzania. Hizi nafasi nafahamu huwa haziombwi, zinahitaji mtu ambaye amekuwa kwenye Chama kwa muda mrefu, mwenye kufahamika ndani ya Chama, mwenye watu wa kumsaidia n.k Lakini hayo yote nimeona niyaweke pembeni nijikite katika Imani yangu kwa Mungu, Kwako na kwa Watanzania kuwa nahitaji kuitumikia nchi.
Mh. Rais naamini nikipata nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa nafasi ya Ukuu wa Wilaya naweza leta mchango na sifa njema kwa Nchi yangu, Serikali na Watanzania kwa Ujumla. Zaidi naweza fanikisha adhma njema uliyo nayo katika kuwatumikia Watanzania.
Kama ambavyo nimesema awali. Si kawaida kwa mtu kuomba nafasi hizi za kuteuliwa lakini naomba kwa mara ya kwanza MIMI MTANZANIA MWENYEWE NISIYE NA MTU WA KUNIPIGIA CHAPUO, KUNIOMBEA AU KUNITAMBULISHA KWAKO. NIKUOMBE UNIPATIE NAFASI YA KUWATUMIKIA WATANZANIA. Uwezo mzuri ninao, Nia njema ninayo, Ari ya Utendaji mwema ninayo.
Nina uzoefu wa kutembelea mikoa mingi Tanzania na kukaa sehemu zenye changamoto nyingi. Huko kote nilifanikiwa kujifunza mengi. Sitochagua Wilaya au Mkoa. Nipo Tayari kuanza kutumika wakati wowote mahali popote. Nipo tayari pia kuonana nawe wakati wowote.
Natumaini Ombi langu litakufikia nawe utalifikiria.
Wako Katika Ujenzi wa Taifa.
Napatikana kwa anuani ya barua pepe hii - a.mbamba@yahoo.com
Salam!
Mimi ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 40 ambaye nimesoma nchini Tanzania kuanzia shule ya Msingi, Sekondari na pia Chuo Kikuu. Elimu yangu kubwa nimeipata kwa watanzania ndani na nje ya Darasa.
Nashukuru katika kuitumikia nchi nimehusika kwa njia moja au nyingine katika kusambaza na kutoa Elimu kwa Watanzania kwa njia mbalimbali. Lakini pia katika hilo nimeweza kupata Elimu toka kwa watanzania mbali mbali pasipo kuhusisha vyeti vyao vya Elimu. Katika Elimu kikubwa ambacho nilijifunza ni kuendelea kujifunza siku zote pasipo kukoma.
Mheshimiwa Rais. Si kawaida katika siasa au jamii yetu mtu kuomba uteuzi kwa namna hii ambayo naitumia kwako. Nimekuwa nikiangalia na kutafakari mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanywa na viongozi vijana wenzangu katika nafasi ambazo wamepewa. Na siku zote nimekuwa nikiumia kuwa pengine kuna tatizo fulani katika uelewa wetu vijana na mambo ya uongozi na wajibu wetu.
Mimi nakuja mbele yako nikiwa pembeni ya watanzania wengi ambao wanaangalia kila kinachotokea na kukitafakari kwa kina. Mh. Rais, naamini kwa yale ambayo nimejifunza katika maisha nikiwa nimeajiriwa na kujiajiri kuna mengi ambayo ningeweza pia yatumia katika kutumikia nchi yangu. Inawezekana kabisa kuna sehemu kama binadamu sikutenda au kunena ilivyopaswa lakini napokaa na kutafakari peke yangu naweza kugundua wapi nilikosea na wapi napaswa kurekebisha au pia kuweka mkazo ikiwa kunaleta matokeo chanya.
Mimi Chama Changu ni Utanzania kwanza. Imani yangu ni Utanzania kwanza na katika hili naamini ninaweza tumika vyema kabisa kwa ajili ya Watanzania kupitia Chama chako cha Mapinduzi. Nikiwa na Kadi ya Chama ya zaidi ya miaka 10. Nimekuwa nikiangalia maslahi ya Watanzania na Utu katika mitizamo yangu, hili naomba niliweke wazi mbele yako. Nikiamini katika Utu Bora, Haki na Wajibu katika kila jambo. Nimekuwa nikiamini matendo mema yanalipa na hali kadhalika matendo maovu yanalipa pasipo kujali Dini, Kabila, Itikadi, Rangi, Umri na Jinsia.
Mh. Rais, Kipekee kabisa naomba nikuombe unipe nafasi ya kuwatumikia Watanzania. Hizi nafasi nafahamu huwa haziombwi, zinahitaji mtu ambaye amekuwa kwenye Chama kwa muda mrefu, mwenye kufahamika ndani ya Chama, mwenye watu wa kumsaidia n.k Lakini hayo yote nimeona niyaweke pembeni nijikite katika Imani yangu kwa Mungu, Kwako na kwa Watanzania kuwa nahitaji kuitumikia nchi.
Mh. Rais naamini nikipata nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa nafasi ya Ukuu wa Wilaya naweza leta mchango na sifa njema kwa Nchi yangu, Serikali na Watanzania kwa Ujumla. Zaidi naweza fanikisha adhma njema uliyo nayo katika kuwatumikia Watanzania.
Kama ambavyo nimesema awali. Si kawaida kwa mtu kuomba nafasi hizi za kuteuliwa lakini naomba kwa mara ya kwanza MIMI MTANZANIA MWENYEWE NISIYE NA MTU WA KUNIPIGIA CHAPUO, KUNIOMBEA AU KUNITAMBULISHA KWAKO. NIKUOMBE UNIPATIE NAFASI YA KUWATUMIKIA WATANZANIA. Uwezo mzuri ninao, Nia njema ninayo, Ari ya Utendaji mwema ninayo.
Nina uzoefu wa kutembelea mikoa mingi Tanzania na kukaa sehemu zenye changamoto nyingi. Huko kote nilifanikiwa kujifunza mengi. Sitochagua Wilaya au Mkoa. Nipo Tayari kuanza kutumika wakati wowote mahali popote. Nipo tayari pia kuonana nawe wakati wowote.
Natumaini Ombi langu litakufikia nawe utalifikiria.
Wako Katika Ujenzi wa Taifa.
Napatikana kwa anuani ya barua pepe hii - a.mbamba@yahoo.com