Barua ya wazi kwa Wizara ya TAMISEMI

Natafuta kiki

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
911
1,284
Ndugu waziri ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa; pole na majukumu ya kitaifa.

Yah: KUZUILIWA UHAMISHO WA KUBADILISHANA.

Sisi watumishi wa serikali hususan kada ya Ualimu tunayo masikitiko makubwa sana pale tunapotaka kuhama kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine kwa njia ya kubadilishana lakini tunakutana na vikwazo kadhaa kama ifuatavyo.

1. Maafisa elimu kukataa kusaini barua za uhamisho

2. Wakurugenzi kukataa kusaini pia barua kwa kisingizio kwamba uhamisho umefungwa

3. Baadhi ya watumishi waliopo hapo ofisini TAMISEMI Dodoma kuwa na kauli mbaya dhidi ya watumishi wanaotaka kuhama hata kama ikiwa watumishi wanabadilishana vituo.

Tunafahamu kwamba uhamisho uliozuiliwa na serikali ni ule wa watumishi wanaotaka kuhama bila replacement yeyote hali iliyopelekea sehemu moja kuwa na upungufu na ndio maana mkazuia uhamisho huo.

Lakini pia kumekuwa na tabia ya upendeleo kwa baadhi ya walimu/watumishi kuhama ili hali wengine wanazuiliwa hali inayoonyesha viashiria vya rushwa.

Ombi letu:

1. Tunakuomba mheshimiwa Waziri ingilia hili suala kwani uhamisho wa kubadilishana hauna athari zozote yaani kila kituo kinakuwa na balance ya watumishi.

2. Utoe tamko rasmi kwa watumishi wa halmashauri ikiwemo wakurugenzi na maafisa elimu kwamba uhamisho wa kubadilishana usizuiiwe kwa namna yoyote ile.

3. Kukemea viashiria vyote vya rushwa hapo ofisini kwako TAMISEMI kwani kuna watumishi wachache wanaomba rushwa kwa watumishi ili wawasaidie kuhama.

Wako katika ujenzi wa taifa......

Walimu wanaobadilishana vituo vya kazi.
 

Ndugu waziri ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa; pole na majukumu ya kitaifa.

Yah: KUZUILIWA UHAMISHO WA KUBADILISHANA.

Sisi watumishi wa serikali hususan kada ya......
 
Acha ubinafsi wewe paza sauti Serikali ifungulie uhamisho achana na hivyo kubadilishana cjui nini. Mana kwa ujumla kufunga uhamisho ni uonevu
 
Mkuu mbona hujataja utofauti wa malipo ya uhamisho?

Na mtu aneenda katika mazingira magumu kupewa malipo madogo kuliko anaeenda mazingira mazuri.



Azimio to iwambi and ileje to ipande!
 
Ila kuwa Mtumishi zama hizi inabidi ujikaze kweli..vinginevyo utakufa kwa stress..!
 
Acha ubinafsi wewe paza sauti Serikali ifungulie uhamisho achana na hivyo kubadilishana cjui nini. Mana kwa ujumla kufunga uhamisho ni uonevu
Mkuu hapo hakuna ubinafsi kwa leo nmemueleza kwa kubadilishana
Nipo naandaa waraka kwa raisi kuhusiana na hali inavyoendelea kuwa na subira
 
Mkuu mbona hujataja utofauti wa malipo ya uhamisho?

Na mtu aneenda katika mazingira magumu kupewa malipo madogo kuliko anaeenda mazingira mazuri.



Azimio to iwambi and ileje to ipande!
Mkuu nmemueleza kuhusu uhamisho wa kubadilishana tu ambao mtu anajigharamia mwenyewe
Haingii akilini eti hadi huo wanazuia
 
RUSWA IPO KWELI
Mimi nilibadilisha na mtu yeye akahamia huku niliko tangu 2018, mimi jina langu halikutoka, nimepeleka nakala kwa KATIBU TAWALA mara 2, Kwa KATIBU MKUU TAMISEMI mara 2, ila hakuna kinachoendelea,, lakini wenye connection wanahama kila siku, tena bila hata kubadilishana na mtu hata mwezi hauishi.
Daaah! MUNGU TUNAKUOMBA HII CORONA isiishe hadi nchi ibaki na watu safi wenye kujali haki, utu, na wenye hofu ya MUNGU pekee!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom