Barua ya wazi kwa Waziri Mwigulu Nchemba

Bufa

JF-Expert Member
Mar 31, 2012
10,593
20,964
Kwako Mh Mwigulu Nchemba najua upo humu na huwa unapita pale upatapo nafasi.

Kama ulivyosikia mwingine kauwawa tena leo huko Kibiti kabla hata maumivu ya mauaji ya juzi hayajapoa. Toka haya mauaji yaanze naamini watu zaidi ya 40 wameuwawa (Sina idadi kamili), hawa ni wazazi, walezi, wame/wake na ndugu zetu.

Mtu hahitaji kuwa forensic expert kuelewa pattern ya mauji yaendeleayo huko Kibiti: wanauwawa viongozi, wanaume, watu wazima huku wakina Mama wakiachwa wajane na watoto yatima. Aidha mauji karibu yote Kama inavyoripotiwa yanatokea Usiku. Swali ni je kwanini polisi chini ya wizara yako hawaongezi ulinzi hasa mida ya Usiku?

Njia ya kuongea na wazee wa Kibiti kila baada ya tukio ni dhahiri imefeli. Kama hamuwezi kuwapa ulinzi basi msifanye nao mikutano kuwaonyesha sura zao ili wabaya wao wawaue ifikapo usiku.

Lakini pia kila siku tunasikia polisi wameuwa majambazi wanaodhaniwa kuwa ndo wahusika wa Kibiti, Police watapata wapi inside info kama wanaua wahusika? Haya mauji ya polisi yanatia doa uwezo na mafunzo yao achilia mbali intelegensia ya vyombo vya usalama ambao inaonekana hawana clue hadi leo

Ni wakati sasa viongozi muwajibike kwa kushindwa kutimiza wajibu wenu. Sasa kila nikisikia jina Lyanga mkuu wa polisi Kibiti japo simfahamu sura najua tayari kuna ndugu yetu huko ameshakatishwa uhai. Kuachia ngazi ni uzalendo wa Hali ya juu unapoona mwenyewe unapwaya. Mjitathimini

Kibiti salama au muwajibike.
 
Akale wapi mkuu hao ndio chama cha makinikia hawana time na wananchi wao nia ya ni madaraka tuu [HASHTAG]#2020[/HASHTAG] mwaga pombe tuanze kusuka upya

kimeo
 
Mambo yapo kimchakato zaidi kuwa mpole!
Roho za watu zinapotea wao wamekalia michakato tu. Mipango gani isiyotekelezeka? Hadi lini? Hadi wapotee wangapi ili tuseme sasa yatosha?

Sirro nae aliingia kwa mbwembwe kumbe hamna kitu
 
Kuna mtu alishauri labda Chadema watangaze kufanya mkutano huko hapo armed forces zote zitakuwa deployed huko. Ni mzaha ila una ukweli ndani yake hii serikali inaact tena haraka ikisikia Chadema tu
 
Naona mkuu umezungumzia mpaka INTELIJENSIA hapo, Geshi lile linauwezo mkubwa wa kuvuruga AMANI, kuleta MACHUKIZO na KERO kwenye utulivu, KUNYONG'ONYESHA wanaTZ, kuongoza MAGARI, kukusanya FAINI, kupitia BAR zote kuchukua chochote kitu, kuombea AJALI, kupiga RISASI hewani mbele ya raia asiye hata na manati, kutangaza HABARI(yaliyodhaniwa majambazi yamekutwa na silaha hizi, kumbe zao wametoa stoo), kujaza kwenye misafara, n.k Walikosa hata intelijensia ya wenzao kuuawa, kituo kuvamiwa.

Ngoja tuone
 
Mda mwingine unaweza kuchoka kuishi tanzania maana vitu siliazi wanaviletea maigizo. Wamekalia kudanganya wa tanzania nakukamata kamata wapinzani.

Sent from my HUAWEI Y625-U32 using JamiiForums mobile app
 
Polisi wanawaua moja kwa moja..inabidi wawatie nguvuni kwanza kuwahoji kuhusu huo mtandao wao na si kuwaua kwa hasira
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom