Elections 2010 Barua ya wazi kwa wana JF na Watanzania wote.

Zawadi Ngoda

JF-Expert Member
Aug 13, 2009
3,768
1,817
Ndugu wana JF, Ndugu Watanzania wenzangu, mabibi na mabwana, vijana na wazee, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchaguzi huu mkuu. Shukurani za pekee ziwaendee viongozi wa JF, Wanachama wa JF, Vyama vyote vya siasa, wagombea wote toka udiwani mpaka urais.

Uchaguzi umekwisha, na jana tu tulikuwa tumegawanyika katika makundi, kama wana NCCR-Mageuzi, TLP, CHADEMA, CUF, CCM na kadhalika, Lakini leo sisi wote ni Watanzania. Watanzania kwa maana kusahau tofauti zetu za kivyama, kusahau majeraha ya kipindi cha kampeni na tudumishe ummoja ambao siku zote tumekuwa nao. Tukutane tena hapa JF bila ya kukumbushana mambo ya kampeni, tukutane Magomeni, mwanza, Zanzibar n.k na tupeane mikono kama zamani. Hii ndio Demokrasia na ni muhimu kuelewa kuwa mara kampeni zinapoisha basi hatuendelei nazo tena mpaka 2015 katika kipindi kile cha miezi 3. Vinginevyo tutasahau suala la ujenzi wa Taifa, na tukaendelea kupiga kampeni kwa kipindi cha miaka 5.

Kabla ya kuedelea nafikiri ni vyema nieleze nini ninachoamini mimi. Ninaamini katika Demokrasia, Ninaamini kuwa Demokrasia yetu itakuja si kwa 'Revolution bali kwa Evolution', Ninaamini kuwa Demokrasia ni Process inayochukua muda mrefu sambamba na elimu ya wananchi, uchumi na ueleo. Ninaamini kuwa CCM itapoteza viti vya ubunge Chaguzi baada ya chaguzi na kamwe haitavidharau vyama vya siasa na Rais toka upinzani atapatikana pale wabunge wa upinzan watafikia 40% ya wabunge wote wa Tanzania.

Demokrasia ni uchaguzi wa watanzania, na hatutarudi nyuma kamwe. Kuna usemi usemao pindi ukishaionja Demokrasia basi hata kwa bunduki hakuna kiongozi anayeweza kuwarudisha wananchi nyuma. Lakini siamini eti Demokrasia yetu ijengwe na watu au mataifa toka nje, hili halitowezekana na kama likitokea basi Demokrasia hiyo itakuwa sio halisia. Kwa hiyo kwa wale wanaotegemea nchi za Magharibi au Marekani ndio wajuzi wa kujenga Demikrasia yetu, wanajidanganya kwani hilo halitatokea ispokuwa vurugu. Kwa hiyo napenda kutoa ujumbe kwa wale wanaopenda kukimbilia nje ya nchi na kulalama dosari zilizojitokeza katika uchaguzi eti ndio huko kuna majibu, wanafanya kosa kubwa sana. Tuna nafasi ya kukutana wenyewe na tuelezane dosari kama vile walivyofanya Zanzibar kati ya CCM na CUF. Na tumehakikisha kuwa inawezekana! Ni vigumu kumaliza dosari katika nchi masikini kama yetu ambayo Teknolojia, ueleo, elimu na miundo mbinu bado ipo katika zama za ujima.

Watanzania ni watu wanaopenda umoja na amani. Kwa maana hiyo Chama chochote kitachotaka kuingia madarakani kwa kutengua moja kati ya hayo, chama hicho machoni mwa watanzania ni kama nguvu ya soda. Kitavuma kwa muda mfupi na kitatokomea pole pole na pengine hata kufa. Ikiwa chama kina mlengo wa Kikabila, dini, au rangi basi nacho kitakufa ama kitashinda ubunge tu katika maeneo yale ambayo walengwa wako wengi. Lakini kamwe hakitashinda urais! Kinyume chake, vyama hivyo vitaipa nguvu CCM iendelee kushinda na kuwa maarufu kwa miaka dahli. Tusaidiane kuvionya vyama au watu waliopo ndani ya vyama hivyo.

Pamoja na kulingana na nchi nyingi za Afrika na Afrika mashariki, lakini ukuaji wa Demokrasia ya Tanzania hautalingana na nchi yeyote ya Afrika. Kuna wanaopenda kulinganisha na Kenya kwa yale yaliyowasibu katika uchaguzi uliopita, lakini napenda kuwaeleza watanzania kuwa huko sisi hatutafika kwa vile tupo katika mazingira tofauti. Demokrasia ya Tanzania itakuzwa na kuimarishwa kupitia Bunge na sio mpaka chama cha upinzani kipate urais.

Mwisho napenda kuwashukuru tena Viongozi wa JF, na nina wosia mkubwa kwa wana JF na waandishi wote wa habari. Sekta yenu ni muhimu sana katika kuigeuza jamii kwa mazuri au mabaya, hivyo ni muhimu sana kwenu kufuata maadili ya uandishi. Hii ikiwa na pamoja na kutoandika kiushabiki au upendeleo wa chama fulani maadam unakipenda.

Mungu ibariki Tanzania, kibariki chama tawala kiweze kutuongoza vyema mpaka 2015.
 
Ni kweli kabisa kuwa ukiiba kura watu wanyamaze na kupiga makofi kukupongeza kwa wizi wako kwani hiyo ndiyo demokrasia? Nasema katu kamwe na sitakubali kuwa mfuasi wa falsafa ya wizi na ukiukwaji wa matakwa ya watu. Na kwa ukweli hilo ni kosa la uhaini ambalo ni kosa kubwa kushinda yote kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu. Hivyo matumaini yako kuwa tutanyamaze na kufumbata mikono yetu kwa wizi huu wa demokrasia ni ya kijinga na ninaomba mwambie Kikwete, Makamba, Kinana na vibaraka wao Makame na Kiravu kuwa Watanzania wenye dhamira hai na uwezo mkubwa wa kufikiria ambao ni wengi sana watapinga kwa nguvu zote utawala wake na wataanika hadharani wizi wao. Na kama wanataka kuingia mbinguni (kama kweli ni waumini) wanatakiwa kwanza watubu kwa Watanzania na kueleza kwa kina jinsi walivyoshiriki kuiba kura na kutangaza matokeo ya uongo. Bila hivyo ni Jehanamu ndiyo yatakuwa makao yao makuu.
 
anayewaza kukimbilia nje ya nchi labda ni JK anatafuta kwa kujificha maana anajua wananchi akituletea zengwe safari hii tutamuadabisha. mkuu post nyingi sana tumeandika na kupendekeza kuwa sisi hatusahau yaliyopita maana yote ni dhuluma.mnayewaza kuganga yajayo nyinyi ndo wezi maana mnawaza namna ya kutuibia tena.kwetu sisi yaliyopita ni dhahabu, sisi hatufuti makovu kwa maana tulijeruhiwa tutayaacha hivihivi mbaka tutakapowaonyesha wajukuu zetu.kufutika kwake labda ndo kuisha kwa ufisadi, kufutwa kwa matabaka na kuhakikisha kuwa nchi ianatawaliwa na kuongozwa na wazalendo kwa manufaa ya wazalendo. na sio kama hivi sasa nchi inatawaliwa na wahindi na waarabu kwa manufaa yao huku mkwere akibaki kama sanamu.
NDUGU ZANGUNI,
TUUNGANE PAMOJA,TUPAMBANE PAMOJA ILI TUSHINDE PAMOJA.
Hili ndilo suluhisho pekee la maisha yetu
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU IBARIKI AFRIKA
AMEN!
 
zawadi ngoda!!!...hivi nikikuangalia kwenye macho nitakiona unachoongea?...au umepaste frm s/where!
 
Mkuu Zawadi,

Je wewe upo upande gani CCM au ni mmoja wa internal observers? maana hupendi international observers ati!

Maneno yako yamejaa mbwembwe za kupindisha au kuyumbisha au kucheza na mawazo ya wana mageuzi wengi na ambao wataendelea kuwepo mika nenda rudi.

Demokrasia Tanzania imekomaa kwa sasa isipokuwa kuna walakini katika kuitekeleza ambapo maoni ya wengi bado hayakubaliki.

Unazungumzia kwamba demokrasia inatoka au inapenyezwa na watu kutoka mataifa ya nje ni yapi hayo? je una ushahidi na mawazo hayo? na unasahau kwamba sasa hivi ulimwengu umekuwa kijiji na watu wanasoma magazeti,majarida wanaangalia televisheni yenye kurusha habari kutoka kona nyingi za dunia na kuona jinsi dunia inavyobadilika.

Unazungumzia kuhusu amani na utulivu wa nchi yetu na una wasiwasi wa kuona chama mbadala kitashinda uchaguzi na kuongoza nchi na huenda kikavuruga amani na utulivu huo ni mawazo gani hayo ndugu yangu?. Amani na utulivu vipo siku zote Tanzania na wala haitavurugwa isipokuwa endapo watu wanakuwa tayari kucheza rafu kwenye uchaguzi.

Halafu umehitimisha kwa kusema kwamba JF ni ya waandishi wa habari je unaweza kufafanua juu ya hili maana hapa jukwaani panajumuisha watu wa aina zote.
 
Ndugu wana JF, Ndugu Watanzania wenzangu, mabibi na mabwana, vijana na wazee, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchaguzi huu mkuu. Shukurani za pekee ziwaendee viongozi wa JF, Wanachama wa JF, Vyama vyote vya siasa, wagombea wote toka udiwani mpaka urais.

Uchaguzi umekwisha, na jana tu tulikuwa tumegawanyika katika makundi, kama wana NCCR-Mageuzi, TLP, CHADEMA, CUF, CCM na kadhalika, Lakini leo sisi wote ni Watanzania. Watanzania kwa maana kusahau tofauti zetu za kivyama, kusahau majeraha ya kipindi cha kampeni na tudumishe ummoja ambao siku zote tumekuwa nao. Tukutane tena hapa JF bila ya kukumbushana mambo ya kampeni, tukutane Magomeni, mwanza, Zanzibar n.k na tupeane mikono kama zamani. Hii ndio Demokrasia na ni muhimu kuelewa kuwa mara kampeni zinapoisha basi hatuendelei nazo tena mpaka 2015 katika kipindi kile cha miezi 3. Vinginevyo tutasahau suala la ujenzi wa Taifa, na tukaendelea kupiga kampeni kwa kipindi cha miaka 5.

Kabla ya kuedelea nafikiri ni vyema nieleze nini ninachoamini mimi. Ninaamini katika Demokrasia, Ninaamini kuwa Demokrasia yetu itakuja si kwa 'Revolution bali kwa Evolution', Ninaamini kuwa Demokrasia ni Process inayochukua muda mrefu sambamba na elimu ya wananchi, uchumi na ueleo. Ninaamini kuwa CCM itapoteza viti vya ubunge Chaguzi baada ya chaguzi na kamwe haitavidharau vyama vya siasa na Rais toka upinzani atapatikana pale wabunge wa upinzan watafikia 40% ya wabunge wote wa Tanzania.

Demokrasia ni uchaguzi wa watanzania, na hatutarudi nyuma kamwe. Kuna usemi usemao pindi ukishaionja Demokrasia basi hata kwa bunduki hakuna kiongozi anayeweza kuwarudisha wananchi nyuma. Lakini siamini eti Demokrasia yetu ijengwe na watu au mataifa toka nje, hili halitowezekana na kama likitokea basi Demokrasia hiyo itakuwa sio halisia. Kwa hiyo kwa wale wanaotegemea nchi za Magharibi au Marekani ndio wajuzi wa kujenga Demikrasia yetu, wanajidanganya kwani hilo halitatokea ispokuwa vurugu. Kwa hiyo napenda kutoa ujumbe kwa wale wanaopenda kukimbilia nje ya nchi na kulalama dosari zilizojitokeza katika uchaguzi eti ndio huko kuna majibu, wanafanya kosa kubwa sana. Tuna nafasi ya kukutana wenyewe na tuelezane dosari kama vile walivyofanya Zanzibar kati ya CCM na CUF. Na tumehakikisha kuwa inawezekana! Ni vigumu kumaliza dosari katika nchi masikini kama yetu ambayo Teknolojia, ueleo, elimu na miundo mbinu bado ipo katika zama za ujima.

Watanzania ni watu wanaopenda umoja na amani. Kwa maana hiyo Chama chochote kitachotaka kuingia madarakani kwa kutengua moja kati ya hayo, chama hicho machoni mwa watanzania ni kama nguvu ya soda. Kitavuma kwa muda mfupi na kitatokomea pole pole na pengine hata kufa. Ikiwa chama kina mlengo wa Kikabila, dini, au rangi basi nacho kitakufa ama kitashinda ubunge tu katika maeneo yale ambayo walengwa wako wengi. Lakini kamwe hakitashinda urais! Kinyume chake, vyama hivyo vitaipa nguvu CCM iendelee kushinda na kuwa maarufu kwa miaka dahli. Tusaidiane kuvionya vyama au watu waliopo ndani ya vyama hivyo.

Pamoja na kulingana na nchi nyingi za Afrika na Afrika mashariki, lakini ukuaji wa Demokrasia ya Tanzania hautalingana na nchi yeyote ya Afrika. Kuna wanaopenda kulinganisha na Kenya kwa yale yaliyowasibu katika uchaguzi uliopita, lakini napenda kuwaeleza watanzania kuwa huko sisi hatutafika kwa vile tupo katika mazingira tofauti. Demokrasia ya Tanzania itakuzwa na kuimarishwa kupitia Bunge na sio mpaka chama cha upinzani kipate urais.

Mwisho napenda kuwashukuru tena Viongozi wa JF, na nina wosia mkubwa kwa wana JF na waandishi wote wa habari. Sekta yenu ni muhimu sana katika kuigeuza jamii kwa mazuri au mabaya, hivyo ni muhimu sana kwenu kufuata maadili ya uandishi. Hii ikiwa na pamoja na kutoandika kiushabiki au upendeleo wa chama fulani maadam unakipenda.

Mungu ibariki Tanzania, kibariki chama tawala kiweze kutuongoza vyema mpaka 2015.

Hizi pumba peleka kwengine sio hapa. Wewe unasema eti uchaguzi umepita yaani watu wamedhulumiwa wewe unasema umepita nikuulize wewe ukidhulumiwa na mtu utayasema haya? Unasema Sasa sote ni watanzania wakati muda mfupi uliopita ulikuwa ukiwaita wapinzani wadini, watu wenye wivu, wasio weza kufikiri nikuulize wewe mtu ukimtukana atakuheshimu huo umoja unaozungumzia unatokea wapi? Demokrasia inajengwa si kwa kupitia Bunge (This is totally wrong) Demokrasia hujengwa kwa misingi ya uhuru wa kila mtu kutoa mawazo yake na kusikilizwa na pamoja na kutenda haki. Sasa wewe na CCM mnafanya hivyo.

Wewe subiria Tanzania ije kuwa kama Zimbabwe mbakie kusema watanzania wavivu hawataki kufanya kazi but ukweli wa mambo ni kuwa mtu akidhulumiwa lake hata nidhamu, morali na hamu ya kufanya kazi hupotea. Kila la Kheri siasa zako za kinafiki !!!!!
 
kwako zawadi ni leo ndio umekuja kufahamu kwamba sote ni watanzania??? 4 the past two weeks statements zako zilikuwa zinaonyesha hii nchi ina wenyewe na si watanzani sasa unataka kutuambia sisi wajinga unatukumbusha kwamba Tanzania ni ya wadanganyika basi tukae na ujinga wetu. Of coz Tanzania itaendelea kuwepo na wenye Tanzania yao wataendelea kuwepo. Acha kupaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa kwa huruma gani uliyokuwa nayo uje hapa na maneno yako ya kupaka asali wakati juzi ulikuwa unaona kila mpinzani kama si binadamu.
 
anayewaza kukimbilia nje ya nchi labda ni JK anatafuta kwa kujificha maana anajua wananchi akituletea zengwe safari hii tutamuadabisha. mkuu post nyingi sana tumeandika na kupendekeza kuwa sisi hatusahau yaliyopita maana yote ni dhuluma.mnayewaza kuganga yajayo nyinyi ndo wezi maana mnawaza namna ya kutuibia tena.kwetu sisi yaliyopita ni dhahabu, sisi hatufuti makovu kwa maana tulijeruhiwa tutayaacha hivihivi mbaka tutakapowaonyesha wajukuu zetu.kufutika kwake labda ndo kuisha kwa ufisadi, kufutwa kwa matabaka na kuhakikisha kuwa nchi ianatawaliwa na kuongozwa na wazalendo kwa manufaa ya wazalendo. na sio kama hivi sasa nchi inatawaliwa na wahindi na waarabu kwa manufaa yao huku mkwere akibaki kama sanamu.
NDUGU ZANGUNI,
TUUNGANE PAMOJA,TUPAMBANE PAMOJA ILI TUSHINDE PAMOJA.
Hili ndilo suluhisho pekee la maisha yetu
MUNGU IBARIKI TANZANIA,
MUNGU IBARIKI AFRIKA
AMEN!

Hawa ndio wale wachache wenye matarajio ya kufanya vyama vya siasa kama sehemu ya idiolojia za ubaguzi wa Rangi na Ukabila. Mimi binafsi sioni kabisa, na wala sidhani kama nchi hii inaongozwa na Wahindi na Waarabu.

Tupo katika kipindi cha utandawazi na tumekaribisha nchi kwetu watu toka mataifa mbali mbali toka ulaya mpaka uchina, Arabuni mpaka India, Marekani mpaka Afrika Kusini.

Iweje mwenzetu ubague watu na kufikiri eti tutakuwa pamoja! Mbaguzi hana nafasi katika Tanzania ya leo.

Na bado unaimba tuwe pamoja! Sikuelewi.
 
Hawa ndio wale wachache wenye matarajio ya kufanya vyama vya siasa kama sehemu ya idiolojia za ubaguzi wa Rangi na Ukabila. Mimi binafsi sioni kabisa, na wala sidhani kama nchi hii inaongozwa na Wahindi na Waarabu.

Tupo katika kipindi cha utandawazi na tumekaribisha nchi kwetu watu toka mataifa mbali mbali toka ulaya mpaka uchina, Arabuni mpaka India, Marekani mpaka Afrika Kusini.

Iweje mwenzetu ubague watu na kufikiri eti tutakuwa pamoja! Mbaguzi hana nafasi katika Tanzania ya leo.

Na bado unaimba tuwe pamoja! Sikuelewi.
Toa pumba
 
Mimi sikujibu na sababu na nia ya kutokukujibu ninayo. Na kwa nini nikujibu? Ili ukahadithie na kujitapa kwa wazembe wenzako wa kufikiri kuwa nimekujibu? Kafie mbele huko na ccm yako.
 
Mkuu Zawadi,

Je wewe upo upande gani CCM au ni mmoja wa internal observers? maana hupendi international observers ati!

Maneno yako yamejaa mbwembwe za kupindisha au kuyumbisha au kucheza na mawazo ya wana mageuzi wengi na ambao wataendelea kuwepo mika nenda rudi.

Demokrasia Tanzania imekomaa kwa sasa isipokuwa kuna walakini katika kuitekeleza ambapo maoni ya wengi bado hayakubaliki.

Unazungumzia kwamba demokrasia inatoka au inapenyezwa na watu kutoka mataifa ya nje ni yapi hayo? je una ushahidi na mawazo hayo? na unasahau kwamba sasa hivi ulimwengu umekuwa kijiji na watu wanasoma magazeti,majarida wanaangalia televisheni yenye kurusha habari kutoka kona nyingi za dunia na kuona jinsi dunia inavyobadilika.

Unazungumzia kuhusu amani na utulivu wa nchi yetu na una wasiwasi wa kuona chama mbadala kitashinda uchaguzi na kuongoza nchi na huenda kikavuruga amani na utulivu huo ni mawazo gani hayo ndugu yangu?. Amani na utulivu vipo siku zote Tanzania na wala haitavurugwa isipokuwa endapo watu wanakuwa tayari kucheza rafu kwenye uchaguzi.

Halafu umehitimisha kwa kusema kwamba JF ni ya waandishi wa habari je unaweza kufafanua juu ya hili maana hapa jukwaani panajumuisha watu wa aina zote.

Kama hivyo sivyo, ni nini basi nia na madhumuni ya Kuandamana Washington DC, Marekani, wakati hujazuwiwa kuandamana Dar es Salaam?

Sipati jibu kama si kuomba msaada wa mataifa ya nje yaje kuwasaidia kujenga hiyo muiitayo Demokrasia. Pili sikusema kuwa inapenyezwa na watu toka nje, nilichosema ni kwamba, kwa wale watanzania wanaofikiria kuitafuta Demokrasia huko nje (i.g Marekani) kwa kwenda kushitaki dosari za uchaguzi zilizojitokeza kana kwamba wao wanamajibu au ni walimu wa ujenzi wa demokrasia yetu, wanajidangany.

Siogopi chama pinzani kushika uongozi au kushinda uchaguzi, ninachoamini ni kwamba vyama pinzani vinajipa matumaini makubwa kuliko hali halisi kwa sasa hivi. Na maelezo kuwa Chama pinzani kilishinda URAIS mwaka huu ni ndoto za alinacha. Kwa hiyo twende pole pole tutafika tu.

Mwisho niliposema waandishi wa habari JF, niliwalenga viongozi waendesha JF ambao kwa maoni yangu watofautiane na akina Zawadi wasiokuwa na ujuzi wa uandishi. Kama hawana wataalam wenye fani hiyo basi huu ni wakati kwa mtandao mkubwa kama huo kuwa na watu wa aina hiyo kama tuwajuavyo akina Mchuzi, Chemi Chemponda n.k.
 
kwako zawadi ni leo ndio umekuja kufahamu kwamba sote ni watanzania??? 4 the past two weeks statements zako zilikuwa zinaonyesha hii nchi ina wenyewe na si watanzani sasa unataka kutuambia sisi wajinga unatukumbusha kwamba Tanzania ni ya wadanganyika basi tukae na ujinga wetu. Of coz Tanzania itaendelea kuwepo na wenye Tanzania yao wataendelea kuwepo. Acha kupaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa kwa huruma gani uliyokuwa nayo uje hapa na maneno yako ya kupaka asali wakati juzi ulikuwa unaona kila mpinzani kama si binadamu.

Siku zote nilijua kuwa tupo pamoja, nilichokuwqa nakifanya katika KAMPENI ni kuweka UWONGO wa wapiga kampeni pembeni na kusifu yale mazuri.

Kwa bahati mbaya baadhi ya wagombea wa Urais kwa kutaka kuingia Ikulu walikuwa tayari hata kupika baadhi ya Takwimu ili kuwachafulia wenzao. Kibaya zaidi walishindwa hata kutoa source ya Takwimu hizo.

Hili lilikuwa likinichefua sana karibu ya kutapika. N akwa hakika hili si swala la kampeni tu bali sitalivumilia wakati wowote ule.

Ukija na takwimu nieleze umezipata wapi.
 
Ndugu wana JF, Ndugu Watanzania wenzangu, mabibi na mabwana, vijana na wazee, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchaguzi huu mkuu. Shukurani za pekee ziwaendee viongozi wa JF, Wanachama wa JF, Vyama vyote vya siasa, wagombea wote toka udiwani mpaka urais.

Uchaguzi umekwisha, na jana tu tulikuwa tumegawanyika katika makundi, kama wana NCCR-Mageuzi, TLP, CHADEMA, CUF, CCM na kadhalika, Lakini leo sisi wote ni Watanzania. Watanzania kwa maana kusahau tofauti zetu za kivyama, kusahau majeraha ya kipindi cha kampeni na tudumishe ummoja ambao siku zote tumekuwa nao. Tukutane tena hapa JF bila ya kukumbushana mambo ya kampeni, tukutane Magomeni, mwanza, Zanzibar n.k na tupeane mikono kama zamani. Hii ndio Demokrasia na ni muhimu kuelewa kuwa mara kampeni zinapoisha basi hatuendelei nazo tena mpaka 2015 katika kipindi kile cha miezi 3. Vinginevyo tutasahau suala la ujenzi wa Taifa, na tukaendelea kupiga kampeni kwa kipindi cha miaka 5.

Kabla ya kuedelea nafikiri ni vyema nieleze nini ninachoamini mimi. Ninaamini katika Demokrasia, Ninaamini kuwa Demokrasia yetu itakuja si kwa 'Revolution bali kwa Evolution', Ninaamini kuwa Demokrasia ni Process inayochukua muda mrefu sambamba na elimu ya wananchi, uchumi na ueleo. Ninaamini kuwa CCM itapoteza viti vya ubunge Chaguzi baada ya chaguzi na kamwe haitavidharau vyama vya siasa na Rais toka upinzani atapatikana pale wabunge wa upinzan watafikia 40% ya wabunge wote wa Tanzania.

Demokrasia ni uchaguzi wa watanzania, na hatutarudi nyuma kamwe. Kuna usemi usemao pindi ukishaionja Demokrasia basi hata kwa bunduki hakuna kiongozi anayeweza kuwarudisha wananchi nyuma. Lakini siamini eti Demokrasia yetu ijengwe na watu au mataifa toka nje, hili halitowezekana na kama likitokea basi Demokrasia hiyo itakuwa sio halisia. Kwa hiyo kwa wale wanaotegemea nchi za Magharibi au Marekani ndio wajuzi wa kujenga Demikrasia yetu, wanajidanganya kwani hilo halitatokea ispokuwa vurugu. Kwa hiyo napenda kutoa ujumbe kwa wale wanaopenda kukimbilia nje ya nchi na kulalama dosari zilizojitokeza katika uchaguzi eti ndio huko kuna majibu, wanafanya kosa kubwa sana. Tuna nafasi ya kukutana wenyewe na tuelezane dosari kama vile walivyofanya Zanzibar kati ya CCM na CUF. Na tumehakikisha kuwa inawezekana! Ni vigumu kumaliza dosari katika nchi masikini kama yetu ambayo Teknolojia, ueleo, elimu na miundo mbinu bado ipo katika zama za ujima.

Watanzania ni watu wanaopenda umoja na amani. Kwa maana hiyo Chama chochote kitachotaka kuingia madarakani kwa kutengua moja kati ya hayo, chama hicho machoni mwa watanzania ni kama nguvu ya soda. Kitavuma kwa muda mfupi na kitatokomea pole pole na pengine hata kufa. Ikiwa chama kina mlengo wa Kikabila, dini, au rangi basi nacho kitakufa ama kitashinda ubunge tu katika maeneo yale ambayo walengwa wako wengi. Lakini kamwe hakitashinda urais! Kinyume chake, vyama hivyo vitaipa nguvu CCM iendelee kushinda na kuwa maarufu kwa miaka dahli. Tusaidiane kuvionya vyama au watu waliopo ndani ya vyama hivyo.

Pamoja na kulingana na nchi nyingi za Afrika na Afrika mashariki, lakini ukuaji wa Demokrasia ya Tanzania hautalingana na nchi yeyote ya Afrika. Kuna wanaopenda kulinganisha na Kenya kwa yale yaliyowasibu katika uchaguzi uliopita, lakini napenda kuwaeleza watanzania kuwa huko sisi hatutafika kwa vile tupo katika mazingira tofauti. Demokrasia ya Tanzania itakuzwa na kuimarishwa kupitia Bunge na sio mpaka chama cha upinzani kipate urais.

Mwisho napenda kuwashukuru tena Viongozi wa JF, na nina wosia mkubwa kwa wana JF na waandishi wote wa habari. Sekta yenu ni muhimu sana katika kuigeuza jamii kwa mazuri au mabaya, hivyo ni muhimu sana kwenu kufuata maadili ya uandishi. Hii ikiwa na pamoja na kutoandika kiushabiki au upendeleo wa chama fulani maadam unakipenda.

Mungu ibariki Tanzania, kibariki chama tawala kiweze kutuongoza vyema mpaka 2015.


Umeshiba Matapishi ya mafisadi sasa unataka kupumulia hapa.
Wamekushibisha kunde sasa unajibanabana wapi utolee mashuzi.
JF si uwanja wa kutolea hewa ya mlo wako wa kifisadi.
 
Usipime democrasia kwa ncha ya kidole kaka,kama wanavyodai watu waliosoma tanzania nzima 25% ,we kubali kuwa ni rahisi kuwatala wajinga ,kwani wengi wa watanzania bado wapo usingizini ,iko siku utajua kuwa tanzania hakuna hiyo demo.crasia.
 
You must be out of your senses! uniibie then nikushike mkono na kukupigia makofi eti hiyo ndo democracy? (i will kill you aisee)
huu ujinga wako next time kawaandikie ccm kwenye ilani iwe moja ya ilani yao ...
 
Ndugu wana JF, Ndugu Watanzania wenzangu, mabibi na mabwana, vijana na wazee, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchaguzi huu mkuu. Shukurani za pekee ziwaendee viongozi wa JF, Wanachama wa JF, Vyama vyote vya siasa, wagombea wote toka udiwani mpaka urais.

Uchaguzi umekwisha, na jana tu tulikuwa tumegawanyika katika makundi, kama wana NCCR-Mageuzi, TLP, CHADEMA, CUF, CCM na kadhalika, Lakini leo sisi wote ni Watanzania. Watanzania kwa maana kusahau tofauti zetu za kivyama, kusahau majeraha ya kipindi cha kampeni na tudumishe ummoja ambao siku zote tumekuwa nao. Tukutane tena hapa JF bila ya kukumbushana mambo ya kampeni, tukutane Magomeni, mwanza, Zanzibar n.k na tupeane mikono kama zamani. Hii ndio Demokrasia na ni muhimu kuelewa kuwa mara kampeni zinapoisha basi hatuendelei nazo tena mpaka 2015 katika kipindi kile cha miezi 3. Vinginevyo tutasahau suala la ujenzi wa Taifa, na tukaendelea kupiga kampeni kwa kipindi cha miaka 5.

Kabla ya kuedelea nafikiri ni vyema nieleze nini ninachoamini mimi. Ninaamini katika Demokrasia, Ninaamini kuwa Demokrasia yetu itakuja si kwa 'Revolution bali kwa Evolution', Ninaamini kuwa Demokrasia ni Process inayochukua muda mrefu sambamba na elimu ya wananchi, uchumi na ueleo. Ninaamini kuwa CCM itapoteza viti vya ubunge Chaguzi baada ya chaguzi na kamwe haitavidharau vyama vya siasa na Rais toka upinzani atapatikana pale wabunge wa upinzan watafikia 40% ya wabunge wote wa Tanzania.

Demokrasia ni uchaguzi wa watanzania, na hatutarudi nyuma kamwe. Kuna usemi usemao pindi ukishaionja Demokrasia basi hata kwa bunduki hakuna kiongozi anayeweza kuwarudisha wananchi nyuma. Lakini siamini eti Demokrasia yetu ijengwe na watu au mataifa toka nje, hili halitowezekana na kama likitokea basi Demokrasia hiyo itakuwa sio halisia. Kwa hiyo kwa wale wanaotegemea nchi za Magharibi au Marekani ndio wajuzi wa kujenga Demikrasia yetu, wanajidanganya kwani hilo halitatokea ispokuwa vurugu. Kwa hiyo napenda kutoa ujumbe kwa wale wanaopenda kukimbilia nje ya nchi na kulalama dosari zilizojitokeza katika uchaguzi eti ndio huko kuna majibu, wanafanya kosa kubwa sana. Tuna nafasi ya kukutana wenyewe na tuelezane dosari kama vile walivyofanya Zanzibar kati ya CCM na CUF. Na tumehakikisha kuwa inawezekana! Ni vigumu kumaliza dosari katika nchi masikini kama yetu ambayo Teknolojia, ueleo, elimu na miundo mbinu bado ipo katika zama za ujima.

Watanzania ni watu wanaopenda umoja na amani. Kwa maana hiyo Chama chochote kitachotaka kuingia madarakani kwa kutengua moja kati ya hayo, chama hicho machoni mwa watanzania ni kama nguvu ya soda. Kitavuma kwa muda mfupi na kitatokomea pole pole na pengine hata kufa. Ikiwa chama kina mlengo wa Kikabila, dini, au rangi basi nacho kitakufa ama kitashinda ubunge tu katika maeneo yale ambayo walengwa wako wengi. Lakini kamwe hakitashinda urais! Kinyume chake, vyama hivyo vitaipa nguvu CCM iendelee kushinda na kuwa maarufu kwa miaka dahli. Tusaidiane kuvionya vyama au watu waliopo ndani ya vyama hivyo.

Pamoja na kulingana na nchi nyingi za Afrika na Afrika mashariki, lakini ukuaji wa Demokrasia ya Tanzania hautalingana na nchi yeyote ya Afrika. Kuna wanaopenda kulinganisha na Kenya kwa yale yaliyowasibu katika uchaguzi uliopita, lakini napenda kuwaeleza watanzania kuwa huko sisi hatutafika kwa vile tupo katika mazingira tofauti. Demokrasia ya Tanzania itakuzwa na kuimarishwa kupitia Bunge na sio mpaka chama cha upinzani kipate urais.

Mwisho napenda kuwashukuru tena Viongozi wa JF, na nina wosia mkubwa kwa wana JF na waandishi wote wa habari. Sekta yenu ni muhimu sana katika kuigeuza jamii kwa mazuri au mabaya, hivyo ni muhimu sana kwenu kufuata maadili ya uandishi. Hii ikiwa na pamoja na kutoandika kiushabiki au upendeleo wa chama fulani maadam unakipenda.

Mungu ibariki Tanzania, kibariki chama tawala kiweze kutuongoza vyema mpaka 2015.

Crap!
 
Ndugu wana JF, Ndugu Watanzania wenzangu, mabibi na mabwana, vijana na wazee, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchaguzi huu mkuu. Shukurani za pekee ziwaendee viongozi wa JF, Wanachama wa JF, Vyama vyote vya siasa, wagombea wote toka udiwani mpaka urais.

Uchaguzi umekwisha, na jana tu tulikuwa tumegawanyika katika makundi, kama wana NCCR-Mageuzi, TLP, CHADEMA, CUF, CCM na kadhalika, Lakini leo sisi wote ni Watanzania. Watanzania kwa maana kusahau tofauti zetu za kivyama, kusahau majeraha ya kipindi cha kampeni na tudumishe ummoja ambao siku zote tumekuwa nao. Tukutane tena hapa JF bila ya kukumbushana mambo ya kampeni, tukutane Magomeni, mwanza, Zanzibar n.k na tupeane mikono kama zamani. Hii ndio Demokrasia na ni muhimu kuelewa kuwa mara kampeni zinapoisha basi hatuendelei nazo tena mpaka 2015 katika kipindi kile cha miezi 3. Vinginevyo tutasahau suala la ujenzi wa Taifa, na tukaendelea kupiga kampeni kwa kipindi cha miaka 5.

Kabla ya kuedelea nafikiri ni vyema nieleze nini ninachoamini mimi. Ninaamini katika Demokrasia, Ninaamini kuwa Demokrasia yetu itakuja si kwa 'Revolution bali kwa Evolution', Ninaamini kuwa Demokrasia ni Process inayochukua muda mrefu sambamba na elimu ya wananchi, uchumi na ueleo. Ninaamini kuwa CCM itapoteza viti vya ubunge Chaguzi baada ya chaguzi na kamwe haitavidharau vyama vya siasa na Rais toka upinzani atapatikana pale wabunge wa upinzan watafikia 40% ya wabunge wote wa Tanzania.

Demokrasia ni uchaguzi wa watanzania, na hatutarudi nyuma kamwe. Kuna usemi usemao pindi ukishaionja Demokrasia basi hata kwa bunduki hakuna kiongozi anayeweza kuwarudisha wananchi nyuma. Lakini siamini eti Demokrasia yetu ijengwe na watu au mataifa toka nje, hili halitowezekana na kama likitokea basi Demokrasia hiyo itakuwa sio halisia. Kwa hiyo kwa wale wanaotegemea nchi za Magharibi au Marekani ndio wajuzi wa kujenga Demikrasia yetu, wanajidanganya kwani hilo halitatokea ispokuwa vurugu. Kwa hiyo napenda kutoa ujumbe kwa wale wanaopenda kukimbilia nje ya nchi na kulalama dosari zilizojitokeza katika uchaguzi eti ndio huko kuna majibu, wanafanya kosa kubwa sana. Tuna nafasi ya kukutana wenyewe na tuelezane dosari kama vile walivyofanya Zanzibar kati ya CCM na CUF. Na tumehakikisha kuwa inawezekana! Ni vigumu kumaliza dosari katika nchi masikini kama yetu ambayo Teknolojia, ueleo, elimu na miundo mbinu bado ipo katika zama za ujima.

Watanzania ni watu wanaopenda umoja na amani. Kwa maana hiyo Chama chochote kitachotaka kuingia madarakani kwa kutengua moja kati ya hayo, chama hicho machoni mwa watanzania ni kama nguvu ya soda. Kitavuma kwa muda mfupi na kitatokomea pole pole na pengine hata kufa. Ikiwa chama kina mlengo wa Kikabila, dini, au rangi basi nacho kitakufa ama kitashinda ubunge tu katika maeneo yale ambayo walengwa wako wengi. Lakini kamwe hakitashinda urais! Kinyume chake, vyama hivyo vitaipa nguvu CCM iendelee kushinda na kuwa maarufu kwa miaka dahli. Tusaidiane kuvionya vyama au watu waliopo ndani ya vyama hivyo.

Pamoja na kulingana na nchi nyingi za Afrika na Afrika mashariki, lakini ukuaji wa Demokrasia ya Tanzania hautalingana na nchi yeyote ya Afrika. Kuna wanaopenda kulinganisha na Kenya kwa yale yaliyowasibu katika uchaguzi uliopita, lakini napenda kuwaeleza watanzania kuwa huko sisi hatutafika kwa vile tupo katika mazingira tofauti. Demokrasia ya Tanzania itakuzwa na kuimarishwa kupitia Bunge na sio mpaka chama cha upinzani kipate urais.

Mwisho napenda kuwashukuru tena Viongozi wa JF, na nina wosia mkubwa kwa wana JF na waandishi wote wa habari. Sekta yenu ni muhimu sana katika kuigeuza jamii kwa mazuri au mabaya, hivyo ni muhimu sana kwenu kufuata maadili ya uandishi. Hii ikiwa na pamoja na kutoandika kiushabiki au upendeleo wa chama fulani maadam unakipenda.

Mungu ibariki Tanzania, kibariki chama tawala kiweze kutuongoza vyema mpaka 2015.

Katika thread ndefu hii kuna mawazo mgando ambayo hayawajengi watanzania. Kitu cha msingi hapa Demokrasia isibakwe. Tuachane na madai kuwa mataifa ya nje yanaingiza demkrasia nchini mwetu, tuongelee ubakaji wa demokrasia unaoendelea nchini. Matokeo yanayotangazwa yakiwa yameguibikwa na utata mkubwa, takwimu za waoiga kura zilizojaa mamluki n.k. Tukitaka demokrasia nchini Tanzania ikue, lazima maamuzi ya watanzania yaheshimiwe.

Halafu suala la kusema JF ni ya waandishi wa habari, sijui ni kwanini unakuwa na mtizamo huo. Labda wewe ni mwandishi wa habari lakini kwa ufahamu wangu hapa ni nyumbani kwa wengi wapenda maendeleo na wale wenye mawazo mapana. Hata hivyo sishangai kuwa na wenye mawazo mgando na wale wapenda ufisadi maana ndivyo Mungu anavyotuumba na sisi mara zote hufanya uchaguzi mtizamo wetu kimawazo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom