Barua ya Wazi kwa Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka (CC Halima Mdee) - Viwanja Kibada

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,455
29,134
Ndugu Waziri

YAH: UCHONGAJI WA BARABARA ZA MITAA - KIBADA
Husika na kichwa cha habari hapo juu, Natumai u-mzima wa afya, na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku za ujenzi wa taifa katika madaraka na majukumu yako kama Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mimi ni mmojawapo ya wamiliki wa viwanja vilivyopimwa na kugawiwa na Serikali, kilichopo kitalu (block) namba 10. Mradi huu wa viwanja vya serikali, kama ilivyo miradi mingine ya aina hii inatakiwa ipatiwe miundombinu yote kama Umeme, maji na barabara na Serikali yako, ambayo gharama zake hufidiwa katika gharama za maombi ambayo mmiliki wa kiwanja analipa wakati wa kuomba hapo mwanzo.

Hali iliyopo kibada kwa sasa inasikitisha kwa kweli ambapo Miundombinu ya Barabara na Umeme imewekwa kwa upendeleo/ubaguzi ikiishia kitalu (block) namba sita tu, tena upande mmoja tu wa kulia mwa barabara na kuicha sehemu zingine zikibaki bila miundombinu hii muhimu, hapo maji pia ndio hakuna kabisa. Hatuelewi kwanini mkandarasi wa Wizara/manispaa ameamua kuishia katikati ya kazi wakati viwanja hivi vilipimwa na kuuzwa kwa pamoja.

Kwa upande wa barabara, Hali hii inasababisha watu kuendelea kutumia njia za zamani ambazo zinapita kwenye viwanja vya watu ambao hawajaanza kujenga wakisubiri miundombinu iletwe. Njia hizi ambazo zinapita viwanjani mwa watu nyingi zina michanga hivyo hazipitiki kwa urahisi, huku wengine tukiingia kwnye matatizo na majirani zetu pale unapoamua kuziba njia ili uanze ujenzi. Hii inasababisha eneo lionekane kama "skwata", wakati kiukweli kama miundombinu yote ikipelekwa na pakajengwa pale, itakua ni mojawapo ya maeneo ambayo yanavutia kwa jiji la dar es salaam.

Kwa upande wa Umeme, inatupasa tufunge solar au jenereta hata kwa kwa eneo ambalo umeme haupo mbali sana na barabara, tuseme nusu kilometa kwani nguzo za umeme pamoja na usambazaji wake ambao ulitakiwa ufanywe na serikali haujafanyika. Ujenzi unaoendelea kibada ni wa nyumba za kisasa ambazo mchana zinavutia sana pamoja na uchache wake, lakini usiku ni hatari kwani nyumba ziko mbalimbali sana kwa kua wamiliki wengi wa viwanja wamegoma kuendelea na ujenzi kusubiri huo umeme na barabara ziwekwe ambao hatujui ni lini.

Hii inarudisha nyuma maendeleo ya eneo hili, ambapo eneo la pori ambalo halijajengwa ni kubwa kuliko eneo lililojenwa/endelezwa. Watu watabaki kuuziana tu viwanja kutoka umiliki wa mmoja kwenda kwa mwingine bila mtu kufikiria kujenga sababu ya eneo hilo kutelekezwa na serikali.

Naandika barua hii kukuomba uliangalie hili suala, ikiwezekana basi magari makubwa ya kuchonga barabara yapelekwe eneo hilo baada ya block 6 ili kutengeneza barabara za mitaani wakati unafanya juhudi kuwasiliana na Waziri muhusika wa mambo ya umeme Prof. Sospeter Muhongo ili aweke miundombinu ya umeme watu tuanze Ujenzi.

Natumai barua yangu hii utaipata na kuifanyia kazi ipasavyo na kwa muda muafaka.
Nakala kwa: Halima Mdee (Waziri Kivuli - Nyumba na Maendeleo ya Makazi)

Wako, Shark
 
Last edited by a moderator:
Hii ni sahihi kabisa kwani wakati wanautangaza mradi wa 20 plots walisema ya kwamba pesa unayolipa ni ya kuchangia miundombinu ambapo barabara zitangenezwa (kuchongwa) maji yatasogezwa karibu na umeme pia utasambazwa cha ajabu kilichofanyika ni sehemu ndogo tu hivi sasa ukiomba umeme unachoelezwa ugharamie manunuzi ya nguzo wengine tupo zaidi ya kilometa moja kutoka umeme ulipoishia tutaweza kweli au yale yalikuwa ni mapendekezo ya mtu binafsi? inavyooneka toka astaafu Katibu Mkuu aliyepita basi na mambo ya miundombinu yote katika mradi huu sio kibada peke yake ni kote yamesitishwa tueleweje tumezurumiwa au tumetapeliwa? tuondolee mateso haya mheshimiwa
 
Asilimia 80 ya viwanja block six vinamilikiwa na wafanyakazi wa wzr ya ardhi ......
 
Asilimia 80 ya viwanja block six vinamilikiwa na wafanyakazi wa wzr ya ardhi ......

Viwanja huwa wanagawana watu wa ardhi halafu wanatuuzia sisi tuliokosa tulipotuma maombi....magumashi matupu mjini hapa.
 
Mwandishi wa hii barua kama wewe sio fisadi baasi ulikipata kiwanja hiki kwa ufisadi kupitia mafisadi wanaostail kunyongwa. Kataa maneno yangu mbele ya hadhira na toa ushahidi kua wewe sio hivyo nilivyoandika.
Mimi niliomba viwanja huko wakati vinagawiwa na nina shazi la marafiki zangu kama 20 hivi tumeomba wote hatukupata. Huwa munagawana tu huko halafu munakuja kutuandikia ***** wenu hapa. SHWAINI
 
Muamndishi wa hii barua kama wewe sio fisadi baasi ulikipata kiwanja hiki kwa ufisadi kupitia mafisadi wanaostail kunyongwa. Kataa maneno yangu mbele ya hadhira na toa ushahidi kua wewe sio hivyo nilivyoandika.
Mimi niliomba viwanja huko wakati vinagawiwa na nina shazi la marafiki zangu kama 20 hivi tumeomba wote hatukupata. Huwa munagawana tu huko halafu munakuja kutuandikia ***** wenu hapa. SHWAINI

Sio lazima kutumia lugha ya matusi kuridhisha hisia zako. Wewe umejuaje kuwa alikipata moja kwa moja toka wizarani? Acha uvivu wa kufikiri na kuamua kuwa mpiga ramli. Mleta mada katoa genuine concern ya matatizo ya watu wenye viwanja vya mradi Kibada wewe unakurupuka na tuhuma pamoja na matusi juu. Haikuwa lazima kujibu kwa lugha hiyo isiyo na staha hata kama umejificha nyuma ya keyboard.
 
Acheni ubahiri kodisheni trackor mchonge barabara mkisubiria hii sirikali ya wapiga madesk mtangoja milele...
 
Sio lazima kutumia lugha ya matusi kuridhisha hisia zako. Wewe umejuaje kuwa alikipata moja kwa moja toka wizarani? Acha uvivu wa kufikiri na kuamua kuwa mpiga ramli. Mleta mada katoa genuine concern ya matatizo ya watu wenye viwanja vya mradi Kibada wewe unakurupuka na tuhuma pamoja na matusi juu. Haikuwa lazima kujibu kwa lugha hiyo isiyo na staha hata kama umejificha nyuma ya keyboard.

Wewe na wewe nae! Tusi liko wapi, na mtu anajifichaje nyuma ya keyboard! Wewe umejuaje kuwa hakukipata moja kwa moja toka wizarani? Hili swali lijibu mwenyewe nimekurudishia. Maana wewe ni secretary wa jamaa.
Hapo kwenye blue, narudia tena na tena. Kugawana mugawane nyinyi viwanja (wewe ukiwemo nadhani), barua mije mtu cc sisi mliotunyima. SHWAINI
 
Mkuu Shark, nikupongeze kwa jitihada zako hizi lakini ningefurahi sana kama ungeuelekeza huu ujumbe wizarani kwani mama anaweza asipite humu jamvini, naomba nikueleze na mimi ni muathirika pia kila siku lazima niwalipe vijana wa kusukuma gari langu pindi linaponasa kwenye mchanga wakati nikielekea mjengoni kitalu 17, sasa ninafikiri ni vizuri tufanye joint effort (wakazi wote) tupush ili kupata huduma kama umeme barabara na maji.

Mkuu Tripo9 nikukosoe kidogo na pia niungane na mawazo ya Mkuu Takalani Sesame kwani hata mimi nilikosa lakini nilinunua kwa mtu aliyepata...actually wale waliokuwa wakazi kabla ya mradi kuanza waliuziwa bei chee na baadae walikuja kuuza kwa bei ya wastani.
 
Mwandishi wa hii barua kama wewe sio fisadi baasi ulikipata kiwanja hiki kwa ufisadi kupitia mafisadi wanaostail kunyongwa. Kataa maneno yangu mbele ya hadhira na toa ushahidi kua wewe sio hivyo nilivyoandika.
Mimi niliomba viwanja huko wakati vinagawiwa na nina shazi la marafiki zangu kama 20 hivi tumeomba wote hatukupata. Huwa munagawana tu huko halafu munakuja kutuandikia ***** wenu hapa. SHWAINI

Duh, mbona unanishambulia moja kwa moja sana mkuu wangu Tripo9?
Mi nimenunua tu kwa mtu wa wizarani, yaweza kua ni kweli vingi viligawiwa kwa watu wa wizara kama alivyosema mdau pale juu ndio maana nami nikavipatia huko, but hiyo sababu hai-justify miundombinu kutoendelezwa.

Sio poa namna hiyo kaka!!
 
Last edited by a moderator:
Wewe na wewe nae! Tusi liko wapi, na mtu anajifichaje nyuma ya keyboard! Wewe umejuaje kuwa hakukipata moja kwa moja toka wizarani? Hili swali lijibu mwenyewe nimekurudishia. Maana wewe ni secretary wa jamaa.
Hapo kwenye blue, narudia tena na tena. Kugawana mugawane nyinyi viwanja (wewe ukiwemo nadhani), barua mije mtu cc sisi mliotunyima. SHWAINI

Kama unaona hujatukana hapo kwenye mchango wako, basi kamwite mzazi wako SHWAINI uone jinsi atakavyochekelea.

Pili mimi sijui kama alikipata moja kwa moja toka wizarani ndio maana nikahoji confidence yako ya kumtuhumu mtoa hoja kuwa 'walijigawia viwanja' na wewe ukakosa. Ulijuaje?

Tatu, naona ramli yako imekuonesha mimi ni secretary wake sio, endelea kuogelea kwenye dimbwi la uvivu wa kufikiri na uburudishe hisia zako.

NB: Nina kiwanja kigamboni na nimekinunua kwa mtu aliyeuziwa na mtu aliyegawiwa moja kwa moja toka kwenye mradi kwani alikuwa na shamba eneo la mradi.

Endelea kupiga ramli.
 
Kama unaona hujatukana hapo kwenye mchango wako, basi kamwite mzazi wako SHWAINI uone jinsi atakavyochekelea.

Pili mimi sijui kama alikipata moja kwa moja toka wizarani ndio maana nikahoji confidence yako ya kumtuhumu mtoa hoja kuwa 'walijigawia viwanja' na wewe ukakosa. Ulijuaje?

Tatu, naona ramli yako imekuonesha mimi ni secretary wake sio, endelea kuogelea kwenye dimbwi la uvivu wa kufikiri na uburudishe hisia zako.

NB: Nina kiwanja kigamboni na nimekinunua kwa mtu aliyeuziwa na mtu aliyegawiwa moja kwa moja toka kwenye mradi kwani alikuwa na shamba eneo la mradi.

Endelea kupiga ramli.

Mhaya bhana!
 
Mkuu Shark, nikupongeze kwa jitihada zako hizi lakini ningefurahi sana kama ungeuelekeza huu ujumbe wizarani kwani mama anaweza asipite humu jamvini, naomba nikueleze na mimi ni muathirika pia kila siku lazima niwalipe vijana wa kusukuma gari langu pindi linaponasa kwenye mchanga wakati nikielekea mjengoni kitalu 17, sasa ninafikiri ni vizuri tufanye joint effort (wakazi wote) tupush ili kupata huduma kama umeme barabara na maji.

Mkuu Tripo9 nikukosoe kidogo na pia niungane na mawazo ya Mkuu Takalani Sesame kwani hata mimi nilikosa lakini nilinunua kwa mtu aliyepata...actually wale waliokuwa wakazi kabla ya mradi kuanza waliuziwa bei chee na baadae walikuja kuuza kwa bei ya wastani.

Nimekupata kaka,
Ngoja nifanye kama ulivyoshauri. Hapa anaweza asipite yule mama.
 
Kama unaona hujatukana hapo kwenye mchango wako, basi kamwite mzazi wako SHWAINI uone jinsi atakavyochekelea.

Pili mimi sijui kama alikipata moja kwa moja toka wizarani ndio maana nikahoji confidence yako ya kumtuhumu mtoa hoja kuwa 'walijigawia viwanja' na wewe ukakosa. Ulijuaje?

Tatu, naona ramli yako imekuonesha mimi ni secretary wake sio, endelea kuogelea kwenye dimbwi la uvivu wa kufikiri na uburudishe hisia zako.

NB: Nina kiwanja kigamboni na nimekinunua kwa mtu aliyeuziwa na mtu aliyegawiwa moja kwa moja toka kwenye mradi kwani alikuwa na shamba eneo la mradi.

Endelea kupiga ramli.

Watu hawaelewi tu, kwa viwanja vilivyogawiwa miaka ya 2008 halaf mtu aje kushangaa mimi kua nacho anakua nae anashangaza sana.

Yaani kama hivi vya juzi tu vya Gezaulole tayari waliopewa washaviuza kwa wengine, sembuse vya kibada ambavyo vilitolewa zaid ya miaka mi4 nyuma.

Ni kweli tunaweza kushindwa kununua direct from serikalin, but kama kweli mtu unakitaka utatafuta tu njia ingine, ndo nchi yetu ilivyo, WHEN YOU ARE AT ROMA, DO AS A ROMAN!!
 
Jamani hivi hata hili mpaka serikali kweli? grader inakodishwa kwa sh laki 8 kwa masaa 8 na hilo ni suala la kujipanga nyie wenyewe ili mpate barabara..sasa hapo ni uamuzi wenu tu,kujichanga ila pia ukiamua kulipa mwenyewe pia inawezekana 8 hrs uakuta grader imepasua barabara ya kutosha kabisa ili mradi vipimo viwepo baade sasa uhangaikie maji,,, uzalendo ni wewe kuifanyia nchi yako yale Mazuri na sio nchi ikufanyie yote...
 
Back
Top Bottom