Mkaruka
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 19,617
- 34,062
Kwenye maisha kila mtu ana power ya kurisk anavyoweza.Unaweza kuwa sahihi kuhusu Mbowe, lakini sijasikia hao wengine wa vyama ulivyotaja wakikoswakoswa na risasi za polisi wala kupelekwa Segerea.
Hii inaonyesha ufikri wako una kasoro, hata kama unajihisi uko huru kama ulivyoeleza mwanzo.
Naona huna tofauti na hawa wanasiasa unaowalalamikia, kwa sababu mambo yao ni sawa na haya yako, ya kukana kwamba hawapo kama unavyowaelezea wewe.
The more the risks, the more the rewards.
Mnyika wa 2010 siyo Mnyika wa 2020. Sasa hivi ni tajiri, hayuko tayari kufia uwanja wa mapambano wakati ameshapata maisha.
Zitto wa 2005 siyo Zitto wa 2020, sasa hivi ni tajiri na ana familia. Anachukua risks kwa tahadhali siyo kama enzi hizo.
Mbowe anaijua nguvu ya Dola, anajitahidi sana kufanya marishiano ya tahadhali ili aendelee kunufaika.
Mwaka 2010-2015, CDM ilikuwa inapata zaidibya 300M kila mwezi kwa miaka 5.
Mwaka 2015-2020, CDM imechuma 450M kila mwezi kwa miaka 5 ambazo ni kodi za Walalahoi bila JASHO.
Kwanini Mbowe asikipambanie chama chake kwa manufaa yake. Hata Mrema ambaye mara kibao yuko kwenye majukwaa ya CCM hawezi kutekeleza chama chake.
Mboww hawezi kurushiwa risasi eti kwasababu anapambania vijana hawana AJIRA, watu wamedhulumiwa ARDHI, KODI au wanawake hawana MAJI.
Ukioona anapambania kitu katikati ya hatari ya risasi ni lazima itakuwa inahusu MASLAHI yake kama Masuala ya UCHAGUZI kuporwa, kunyimwa fomu za Kugombea au Mikutano yake ya kisiasa KUZUIWA.
Kama wanasiasa wanacyoangalia mambo yao, sioni sababu ya mtu mwingine yoyote na yeye kutoangalia mambo yake.