Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Bwana Ridhiwani,
Ni matumaini yangu kwamba umzima wa afya popote pale ulipo. Ninaandika hii barua kwa huzuni kubwa nikitarajia ya kwamba yote yaliyomo utayashughulikia ipasavyo na haraka iwezekanavo.
Kwanza kabisa, hongera kwa kuwa mwana wa Sultani (mtoto wa Rais). Hii nafasi imekupa jeuri kubwa kiasi kwamba nchi unaiona kama yako. Kwa muda mrefu tumekustahi sana kutokana na tabia yako ya kuingilia vitu vingi visivyokuhusu na hata kutumia jina la baba yako kufanya ufisadi mwingi kama unavyofanya sasa.
Magari unayomiliki yote tunayafahamu vizuri yakiwa ni ya thamani kubwa huku ukiwadanganya watanzania unamiliki Toyota Camry tu. Ridhiwani, unazo Landcruizer VX V8 mbili. Toyota Camry, Toyota Harrier, Hummer, Mercedes ML, BMW X6, Pamoja na Range Rover Hata na mwenzio January Makamba mwenye ukwasi wa fedha na miradi za kutisha pia tuna data zake. Asidanganye watu anamiliki Pickup double Cabin wakati anayo BMW X5, Landcruiser V8 pamoja na Gari alilomnyang'anya shemeji yake Mr. Gray.
Ridhiwani, yale malori (Freightliner 100) uliyoficha kwa David Mosha yaliyotoka Marekani tunajua ukweli wake wote. Hii ni mifano tu na wala sio swala la leo. Swala la leo ni kuhusu uchaguzi wa UVCCM hapa Dodoma. Tangu juzi, vijana wengi waliotegemea kuchaguliwa kidemokrasia wameingiwa na wasiwasi kutokana na uroho wako.
Jinsi unavyozivuruga timu za mipira hasa yanga na Simmba ndivyo jinsi unavokivuruga CCM. Majuzi tu wanasimba wamelia sana baada ya wewe kuingia kati na kuwanyang'anya mchezaji wao kutoka Burudi ambaye umempeleka Yanga. Nchi yote ilinyamaza hakuna aliyekufatilia. Ila, nakuhakikishia kwamba, hatutaweza kunyamaza ukiendelea na hii tabia ya sasa hivi, hapa Dodoma kwenye uchaguzi wa UVCCM. Vijana wengi masikini wasio na mafisadi nyuma yao wanalalamika, kwamba ndoto zao za uongozi zinayeyuka kutokana na shinikizo za Ridhiwani.
Unalazimisha watu kumpigia kura mamluki wako, na wale wanaogombea nafasi kadhaa unajaribu kuwakatisha tamaa na hata kuwatolea vitisho wasigombee nafasi zao ili tu mtu wako apite. Umetoa hela nyingi na tayari tumesharodhesha majina ya vijana waliopokea hela zako. Ridhiwani, napenda kukukumbusha kwamba wewe siyo Rais. Rais ni baba yako. Hauna nafasi yoyote ya uongozi katika hii nchi. Tabia yako italeta machafuko. Hauwezi kuteua wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, mawaziri na hata wakurugenzi kana kwamba wewe ndiye rais. Unayemchukia mara moja anaishi maisha magumu na hata kupoteza ajira.
Usijisahau kwamba madaraka mliyo nayo ni ya milele. Hata wakina Seif-Al Islam walikuwa kama wewe na mwisho wao umeuona. Huku ndiko mnakotupeleka wana wa Sultani. Usidhanie na wala usijidanganye kwamba watanzania wanakuogopa. Tunakuomba ubadilike. Asante sana Kunisikiliza
Honorable MP (CCM): Dodoma
Ni matumaini yangu kwamba umzima wa afya popote pale ulipo. Ninaandika hii barua kwa huzuni kubwa nikitarajia ya kwamba yote yaliyomo utayashughulikia ipasavyo na haraka iwezekanavo.
Kwanza kabisa, hongera kwa kuwa mwana wa Sultani (mtoto wa Rais). Hii nafasi imekupa jeuri kubwa kiasi kwamba nchi unaiona kama yako. Kwa muda mrefu tumekustahi sana kutokana na tabia yako ya kuingilia vitu vingi visivyokuhusu na hata kutumia jina la baba yako kufanya ufisadi mwingi kama unavyofanya sasa.
Magari unayomiliki yote tunayafahamu vizuri yakiwa ni ya thamani kubwa huku ukiwadanganya watanzania unamiliki Toyota Camry tu. Ridhiwani, unazo Landcruizer VX V8 mbili. Toyota Camry, Toyota Harrier, Hummer, Mercedes ML, BMW X6, Pamoja na Range Rover Hata na mwenzio January Makamba mwenye ukwasi wa fedha na miradi za kutisha pia tuna data zake. Asidanganye watu anamiliki Pickup double Cabin wakati anayo BMW X5, Landcruiser V8 pamoja na Gari alilomnyang'anya shemeji yake Mr. Gray.
Ridhiwani, yale malori (Freightliner 100) uliyoficha kwa David Mosha yaliyotoka Marekani tunajua ukweli wake wote. Hii ni mifano tu na wala sio swala la leo. Swala la leo ni kuhusu uchaguzi wa UVCCM hapa Dodoma. Tangu juzi, vijana wengi waliotegemea kuchaguliwa kidemokrasia wameingiwa na wasiwasi kutokana na uroho wako.
Jinsi unavyozivuruga timu za mipira hasa yanga na Simmba ndivyo jinsi unavokivuruga CCM. Majuzi tu wanasimba wamelia sana baada ya wewe kuingia kati na kuwanyang'anya mchezaji wao kutoka Burudi ambaye umempeleka Yanga. Nchi yote ilinyamaza hakuna aliyekufatilia. Ila, nakuhakikishia kwamba, hatutaweza kunyamaza ukiendelea na hii tabia ya sasa hivi, hapa Dodoma kwenye uchaguzi wa UVCCM. Vijana wengi masikini wasio na mafisadi nyuma yao wanalalamika, kwamba ndoto zao za uongozi zinayeyuka kutokana na shinikizo za Ridhiwani.
Unalazimisha watu kumpigia kura mamluki wako, na wale wanaogombea nafasi kadhaa unajaribu kuwakatisha tamaa na hata kuwatolea vitisho wasigombee nafasi zao ili tu mtu wako apite. Umetoa hela nyingi na tayari tumesharodhesha majina ya vijana waliopokea hela zako. Ridhiwani, napenda kukukumbusha kwamba wewe siyo Rais. Rais ni baba yako. Hauna nafasi yoyote ya uongozi katika hii nchi. Tabia yako italeta machafuko. Hauwezi kuteua wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, mawaziri na hata wakurugenzi kana kwamba wewe ndiye rais. Unayemchukia mara moja anaishi maisha magumu na hata kupoteza ajira.
Usijisahau kwamba madaraka mliyo nayo ni ya milele. Hata wakina Seif-Al Islam walikuwa kama wewe na mwisho wao umeuona. Huku ndiko mnakotupeleka wana wa Sultani. Usidhanie na wala usijidanganye kwamba watanzania wanakuogopa. Tunakuomba ubadilike. Asante sana Kunisikiliza
Honorable MP (CCM): Dodoma